George Michael Uledi.
Leo karibu Social Media platforms zote za Kitanzania zilikuwa zimebeba kauli,Maoni na MSIMAMO wa Chama cha Mapinduzi kuhusu kauli ya Chadema ya No Reforms No Election kupitia Katibu wa NEC, Itikadi Uenezi na mafunzo,ndugu Amos Makalla!
Sijajua kwanini CCM wameingizwa"king"(Provocation Trap)kirahisi MNO na Chadema this time na ni kama kauli hiyo ya Chadema inawasumbua sana CCM bila uwepo wa sababu za msingi!Bado sijaona "suppression maneuver" ambayo strategists wa Chama wameshafanya!
Matokeo yake badala ya watu wa CCM kufanya "suppression" wanajikuta wanaifanyia "promotion" slogan ya "no reforms no election"mbele ya Watanzania!Machadema huko yaliko yatakuwa yanacheka kweli kweli!
Wakati nawaza haya niliamua kufanya "mchezo" mdogo wa "brain arrest" huku nikiamua "kuingia na kukaa" ndani ya vichwa vya Mwenyekiti wa Chadema Taifa ndugu Tundu Lissu,Makamu Mwenyekiti Ndugu John Heche na Mzee Wilbroad Slaa angalau kwa dakika chache kujua nini hasa wanataka kufanya na kupata kupitia "mind game" hii "No Reforms No Election".
MASWALI MATATU YA MSINGI YA KUJIULIZA👇🏿👇🏿
I.Je,Chadema wanaweza kuzuia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025?Jibu ni hapana!
II.Je,Watanzania hawa wanaweza kuzuia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025?Jibu ni hapana!Chadema wamesema watatumia nguvu ya Umma including Wanachama wa CCM kuzuia Uchaguzi Mkuu huu!🤣🤣
III.Je,Mahakama zetu au Mahakama za nje ya Tanzania zinaweza kuzuia Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2025?Jibu ni hapana!
Kama majibu yote hapo juu ni hapana👆👆👆,nini "Majamaa"ya Chadema wanatarget mbele ya Uchaguzi Mkuu huu?
IPO HIVI.
CCM wanapaswa kwenda kusoma KITABU kimoja kizuri cha "The Politics of Provocation: Participation & Protest in Esrael cha Gadi Wolfsfeld 👆👆kitawapa mwanga jinsi gani ya kujua mchezo ambao CDM wanaifanya CCM 🤣🤣
Strategists wa CCM pia wanapaswa kujipiga brash na " Theory of Political Provocation" ya M .Karwat,wanaweza kujua jinsi ya kufanya "suppression" kibabe zaidi!
Provocation(Intentional Provocation),mara zote inakuwa na malengo makuu mawili(I)Bargain or(II) War/Protest.
Ujanja huu wa Chadema kuja na kauli kali ya No Reforms No Election ni "ujanja" wa kuwataka CCM waingie "king" kuja kwenye hatua ya pili ya Political Provocation ambayo ni (II)hatua ya Bargain🤣😛😛😛kabla au baada ya Uchaguzi Mkuu 2025.
Ili hatua ya tatu ya Political Provocation itokee(III)war or/protest, unahitaji uwe ni Chama cha Upinzani ambacho angalau kina uwakilishi wa angalau nusu ya Wabunge Bungeni!Bila hivyo hauwezi kufika hatua ya tatu ambayo CDM wanasema itatokea!Kuzuia Uchaguzi Mkuu!
Chadema hii HAIWEZI kuwashawishi hata Watanzania laki 200,000 kugomea Uchaguzi yaani Public Election Protest na ikawa reality!HAIWEZI!
USHAURI!
Serikali wasikubali kamwe kuingia kwenye hatua ya pili ya Political Provocation yaani (II) Bargaining dhidi ya Chadema!Yapo mabadiliko(Reforms )ambayo yamefanyika so far katika hatua za maridhiano na hata hatua za kikosi KAZI cha Profesa Mkandala na hata mabadiliko ndani ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi(INEC).
Mabadiliko hayo"Electoral Reforms"ambazo zimefanyika so far lazima yawe "tested" kwanza kupitia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kabla hatujaenda kwenye mabadiliko mengine mbeleni!
Narudia tena kusema "electoral Reforms is not an event rather it is a gradual processes".
Hatuwezi "kurisk" Usalama wa Nchi eti sababu tu tuwafurahishe Chadema dhidi ya maslahi ya Watanzania milioni 60+!
Haiwezekani!

Comments
Post a Comment