Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Walimu Semeni Shida Zenu, Msijione Duni - Dkt. Biteko


 

📌 Serikali yatumia mabilioni kulipa madeni ya walimu

📌 Asema walimu ni nguzo ya Taifa

📌 Kliniki ya Walimu neema kwa walimu nchini

📌 CWT yapongezwa kwa kushirikiana na Serikali kutatua changamoto za walimu


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka walimu nchini kuwasilisha changamoto zao na Serikali ipo tayari kuzipatia ufumbuzi na imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kuboresha maslahi yao na pamoja mazingira bora ya kazi.

Dkt. Biteko ameyasema hayo Februari 26, 2025 mkoani Geita wakati aliposhiriki katika ‘Samia Teacher’s Mobile Clinic - Geita’ inayolenga kusikiliza na kutatua kero za walimu Mkoani Geita.

“ Walimu semeni shida zenu na wakati wote msijione duni, oneni namna Serikali inavyoweza kutatua changamoto zenu. Nataka niwakumbushe Watanzania kuwa  ninyi ni nguzo ya taifa letu, zoezi hili linamfanya mwalimu mwenyewe kukutana na watoa huduma Serikalini ili kujua nini kitafanyika juu ya changamoto yake,” amesema Dkt. Biteko.

Ameendelea kusema kuwa Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan itaendelea kutatua changamoto za walimu na kwa kuwa nchi zote zilizoendelea zimewekeza katika elimu.

Ametaja jitihada mbalimbali zilizofanywa na Serikali katika kipindi cha miaka minne kuwa Serikali imelipa malimbikizo ya mishahara ya walimu wa shule za msingi na sekondari kwa walimu 5,061 yenye thamani ya jumla ya shilingi  4,753,349,209.00.

Kwa upande wa madeni ya uhamisho mkoani Geita, Serikali imelipa jumla ya shilingi 2,207,540,900.00 kwa walimu 1,024.

“ Serikali imeendelea kupandisha walimu madaraja kwa wakati na mserereko kwa walimu waliocheleweshwa. Katika mwaka wa fedha 2023/24 jumla ya walimu 10,839 walipandishwa kawaida na walimu 509 walipandishwa madaraja ya mserereko baada ya kubainika kuwa wamecheleweshwa madaraja yao,” amesisitiza Dkt. Biteko.

Amesema ukokotoaji wa gharama za mabadiliko ya gharama za kuwabadilishia walimu hao madaraja ni shilingi  5,471,025,529.00 kwa walimu waliopanda kawaida. Aidha, zilitumika shilingi 368,771,480.00 kwa walimu waliopanda kwa mserereko. Pia, jumla ya walimu 876 wamebadilishiwa muundo wa utumishi wao katika kipindi cha miaka minne baada ya kujiendeleza na kuwasilisha vyeti vyao kwa waajiri.

Akizungumzia madai ya walimu waliokwenda likizo, Dkt. Biteko amesema katika kipindi cha miaka minne, Serikali imeweza kulipa jumla ya shilingi 4,255,813,700.00 kwa walimu 11,783. Pia imelipa shilingi 25,690,000.00 kwa walimu ikiwa ni gharama za matibabu pale ambapo bima ya afya haihusiki katika  matibabu  au ikiwa ni gharama za posho ya mtumishi pindi anapohudhuria matibabu katika hospitali za rufaa.

Aidha, Serikali imeendelea kujenga mazingira wezeshi kwa ajili ya kujifunzia na kufundishia ambapo kwa kipindi cha mwaka 2021 hadi 2024 mkoa wa Geita umejengewa shule mpya 154, kati ya hizo za msingi ni  74 na za sekondari ni shule 80.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amewataka wakurugenzi na wakuu wa wilaya kuanzisha kliniki ndogo za kusikiliza changamoto za walimu katika maeneo yao.

“ Niwapongeze CWT kwa kufanya hivi na kutumia raslimali kwa ajili ya kutetea maslahi ya walimu. Kifanyeni chama chenu kiwe imara, kiwahudumie walimu na sisi Serikali hatutaacha kusikiliza chochote kitakachotoka katika chama chenu,” amesema Dkt. Biteko.

Pamoja na hayo Dkt. Biteko amekitia moyo kikosi kazi cha maafisa waandamizi kutoka Ofisi mbalimbali Serikalini wanaosikiliza na kutatua kero za walimu kufanya kazi hiyo kwa bidii na hatimaye kupata matokeo chanya.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi amekipongeza kikosi kazi kwa  kufanya kazi nzuri ya kutatua changamoto za walimu kwa kushirikiana na CWT.

“ Baada ya kazi kukamilika itaweka misingi kwa watumishi wa umma kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia miongozo iliyopo,” amesema Mhe. Katambi.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT), Bw. Joseph Misalaba amesema kuwa zoezi la kliniki hiyo ni matokeo ya kufanyika kwa ziara mwaka 2024 mkoani Mwanza iliyohusisha maafisa utumishi ambayo ililenga kukutana na walimu wenye chamgamoto sa kiutumishi na kuzitatua.

“ Walimu wengi wemejitokeza na changamoto za kiutumishi na idadi kubwa ya walimu waliojitokeza ambayo imetupatia tafsiri walimu wengi wana changamoto za kiutumishi ambazo zingestahili kutatuliwa na waajiri wao katika maeneo yao. amesema Bw. Misalaba.

Ametaja baadhi  ya changamoto hizo ni madai mengi ya malimbikizo ya mishahara ambayo hayajaingizwa katika mfumo, uwepo wa walimu waliomba kubadilishiwa miundo maombi ambayo hayajafanyiwa kazi kwa wakati.

Aidha, Kliniki hiyo inaratibiwa na Chama Cha Walimu Tanzania kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Fedha, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Tume ya Utumishi wa Walimu - TSC 

Aidha, timu ya maafisa waandaizi  kutoka katika Ofisi za Serikali imefanyakazi katika mikoa 20 hadi sasa.









Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...