Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Askofu Mwamakula Amwaga Siri Kuhusu Jenista Mhagama


 


 *Ameandika Askofu Mwamakula* 🙏🙏🙏

Usilolijua Kuhusu Jenista Mhagama!

Nusu ya pili ya mwaka 2023 ilikuwa na joto la aina yake katika siasa za Tanzania. Fenomena ijulikanayo kama Boniface Anyisile Mwabukusi ilianza kuchomoza na kung'ara katika siasa za Tanzania kupitia sakata la Mkataba wa Bandari.

Mwabukusi, Dkt. Slaa na Mdude waliwekwa kizuizini kule Mbeya baada ya IGP kutangaza kuwa kuna watu walitaka kuipindua serikali ya Rais Samia. Askofu Mwamakula alijikuta akiwa katikati ya utetezi wa watu hao. Walitamkiwa makosa ya uhaini, lakini ghafla wakaachiwa wakiwa polisi bila ya kufikishwa mahakamani.

Alphonce Lusako Mwamwile na mawakili wenzake walifungua kesi ya kupinga mkataba huo. Mwabukusi na wenzake wakawa mawakili wao. Lakini kesi ilitupwa mahakamani kwa kile kilichoelezwa na jaji kuwa mahakama haikuwa na mamlaka ya kuingilia mamlaka ya Bunge.

Mwabukusi na wenzake kadhaa wakahamishia mapambano nje kwa kutangaza maandamano. Mwabukusi alianza kusakwa kama 'dhahabu ya Chunya' na wenye mamlaka. Lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida, Kikosi cha askari kama 15 walifika usiku wa manane katika makazi ya Askofu Mwamakula kule Itunge, Kyela wakidai kumsaka askofu kwa madai kuwa alikuwa kule kwa ajili ya kuandaa maandamano! Chubhaa!

Siku mbili baadaye, Jenista alituma ujumbe na kumualika Askofu Mwamakula bungeni. Ilibidi ndugu wa askofu wajadili kwa kina kumshauri kama aende au la. Lakini cha kushangaza sana Jenista alisema hawakujua kabisa kama kuna watu walikuwa wanamfuatilia askofu nyumbani  alipiga simu kwa RPC wa Mbeya kujiridhisha ili kama ni kweli: tuyaache hayo ni 'syapatali'! Na hatimaye Askofu Mwamakula alitinga Bungeni, alitambulishwa na Spika Dkt. Tulia Ackson ya kuwa ni mgeni wa Waziri Mkuu! 

Baadaye askofu na wenzake watatu: Rev. Dr. Fr. Charles Kitima (TEC) na Askofu Dkt. Kalikawe Lwakalinda Bagonza walikutana pia na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika Ofisi ya Waziri Mkuu katika kikao cha faragha. Waziri Mkuu aliyepatia salaam za Rais Samia. Kikao kile kilipoisha, Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu - Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. Jenista Mhagama alimuombwa Askofu Mwamakula ili abaki kwa ratiba ya kikao kingine pamoja naye kesho yake.

Kikao cha waziri na askofu kilikuwa na agenda mbili: mambo ya Kanisa na suala moja nyeti. Suala hilo nyeti lilimhusu Boniface Mwabukusi. Inaonekana serikali ilijua kuwa askofu alikuwa karibu na Mwabukusi. Askofu alitumia nafasi ile kwa ajili ya kushauri serikali isimuwinde  Mwabukusi kwa kuwa hakuwa na madhara kwa taifa. Alisisitiza kuwa wamuache awe anasema kwa kuwa ni haki yake lakini pia kama atazuiwa atakuwa na madhara zaidi. Kama watu katika jamii wataminywa bila kusema, jamii italipuka! Jenista alielewa na kuahidi kufanyia kazi kwa kuwashauri wenzake.

Jenista alisikiliza kwa makini lakini alitoa ombi moja kuwa askofu amueleze Mwabukusi aache kushambulia watu binafsi katika hoja zake. Lile halikuwa jambo gumu kwa askofu. Serikali kwa kiasi kikubwa iliacha au ilipunguza kumuwinda Mwabukusi na yeye alijikita katika kujenga hoja zake kwa staha zaidi bila kupunguza ukweli.

Kwa ujumla, kikao kile kilikuwa na umuhimu wa kipekee. Mazungumzo yetu na Jenista yalileta suluhisho fulani. Serikali iliweza kwa mara ya kwanza kuelewa jambo lililoifanya upunguze au iache kumfuatilia Mwabukusi kwani kwa kumtafuta kulileta taharuki kubwa na kuifanya serikali izidi kuchukiwa zaidi na wananchi.

Leo nimesikia taarifa za kifo chake. Kama njia ya kuenzi mambo muhimu tuliyowahi kujadili naye nimeamua kutoa ushuhuda huu. Na kama Mungu atanipa kibari nitaeleza mengine jinsi Jenista alivyoshiriki kutuliza mambo ambayo kama yangeangukia mikononi mwa baadhi ya 'vichaa wa mfumo' hali ingekuwa mbaya sana.

Katika mambo magumu sana, Jenista alitafuta ushauri na aghalabu alinitafuta. Wenzie wengi hawakumuelewa kwa kuwa karibu na mimi kwa kuwa walilishwa matango kutoka kule Madaba kuhusu mimi. Lakini wapo walionitahadharisha mimi pia kuhusu 'Mama wa Peramiho'! Sikuwa na la kuogopa kwa kuwa ukiwa mtetezi wa haki unatumia njia yoyote ya haki na ya heshima ili kuwasaidia unaowatetea lakini pia kuwafanya watesi wawaelewe watu wengine ambao wao wanawakandamiza. Nilitimiza wajibu wangu na ndio maana sikuwahi kuogopa kukutana naye.

Jenista alikuwa kama daraja muhimu sana na pia kwa sababu ya unyenyekevu aliokuwa nao. Kama mtu wa mfumo hawezi kukwepa mapera ya mfumo, lakini alikuwa na umuhimu wake. Ni muhimu watu wakajua kuwa panapokuwa na uhasama na makundi katika jamii ni lazima pia wapatikane watu wa kuvunja uhasama huo na hata kuyaunganisha makundi - hili ni jukumu la hatari sana na lililo gumu. Nilijitahidi kulifanya kwa gharama kubwa ikiwemo kutokueleweka!

Ninakulilia Jenista, umeondoka kabla ya kuona kile ambacho nilitamani ukione - Tanzania ile ambayo mtu atapata madaraka ya uongozi kwa njia ya haki, heshima ya kura itakaporudishwa. Uliniita dada, nilikuita kaka! Yule 'mdogo' wako amejawa na majonzi sana. Inaonekana wewe haukumuaga. Na yule 'kaka' yako ambaye ni Mchungaji wa Milima ya Uchagani ameshikwa na mshangao. Mungu akayakumbuke mema yako! Ulale salama Jenista! Nimejitahidi kwa upande wangu kuandika kile ambacho hakuna wa kukisema kuhusu wewe. Hata ningefika msibani kwako huko Dodoma au Peramiho, nisingeweza hata kupewa 'maiki' ili 'niropoke' maana unajua jinsi 'Wangindo' wanavyoogopa 'waropokaji' kama mimi. 


Nitaropoka mengine kwa faida ya 'Wapangwa' na 'Wanyasa'! Lakini wapo pia uliowasaidia ila hawakujua kwa kuwa uliwapambania kwa siri. Ndio dunia ilivyo dada! Tutaonana 'Madaba'!

Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula 

Itunge, Dar es Salaam; 11 Desemba 2025; Saa 9:26 alasiri

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...