Taju Yalaani Vikali Vurugu katika Kuhatarisha Amani

GEORGE MARATO TV
0


 Taasisi ya Tanzania Jumuishi (TAJU) imelaani vikali vitendo vya baadhi ya watu waliosababisha vurugu na kuharibu mali pamoja na kuikosesha amani jamii ya watu wenye ulemavu nchini.

Hayo amebaisha mapema hii leo novemba 10, 2025, jijini Dar es salaam, Katibu wa Taasisi hiyo ya Tanzania Jumuishi (TAJU), Innocent Gabriel Siriwa, katika mkutano wa taasisi hiyo na vyombo vya habari  ambapo pia imevikumbusha vyama vya siasa na viongozi wa dini kutumia nafasi zao vizuri ili kulinda na kuhubiri amani nchini. 

Aidha, Innocent  amesema (TAJU) Inapinga vikali  wote wanaounga mkono kwa kusema kuwa kudai haki kwa njia ya amani hakuwezi kufanikisha upatikanaji wa haki huku ikiwataka watanzania kufuta mtazamo huwo kwani hauna tija na ni wa wakati wa ukoloni

Pia, amesema ili kulinda amani ya taifa la tanzania inapaswa watanzania kuacha kuiga mataifa madogo yanayofanya vurugu bila ufumbuzi wa matatizo ya kama Madagascar ikiwa pamoja na kutumia mitandao kuchagua mema na kuacha mabaya kwani sio yote yaliyopo mtandaoni yanafaa kuigwa

Katika hatua nyingine, aliewahi kuwa mgombea wa ubunge katika jimbo la mbagala kupitia chama cha AAFP na Mwenyekiti wa Taasisi ya (TAJU), Ndonge S. Ndonge ameipongeza tume huru ya taifa ya uchaguzi kwa utendaji mzuri wa majukumu yake katika uchaguzi kwa kutambua maslai ya wote katika utangazaji wa matokeo.

Hata hivyo Ndonge amewataka watanzania kudumisha ulinzi katika jamii na kwa kila mmoja  kutambua umuhimu wa haki ya mwenzie ili kuepuka mgongano wa kimawazo na kihisia jambo ambalo huweza kusababisha vurugu katika jamii ya watanzania.

Kwa upande wake aliyekuwa mgombea wa jimbo la Mkuranga, kupitia chama cha Democratic Party(DP) , Siwema Mketo aliyepata kura 702 amemtaka mbunge mteule Mh. Abdallah Ulega kutojisahau katika majukumu yake.







Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top