Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kongole Rais Dkt. Samia, umewatendea haki wafanyakazi sekta zote


Na: Dkt. Reubeni Lumbagala

Wafanyakazi ni kundi muhimu katika jamii na nchi hasa kutokana na umuhimu wake katika kuchagiza mabadiliko chanya na maendeleo. Wafanyakazi wa sekta zote yaani sekta ya umma (serikali) na binafsi kwa pamoja wanashirikiana katika kusimamia na kutekeleza mipango mbalimbali ya taasisi na nchi kwa ujumla ambapo kufanikikiwa kwa mipango hiyo kunachochea maendeleo na ustawi wa Taifa.

Wafanyakazi wanapaswa kutimiza majukumu yao ya kila siku kama inavyopaswa katika kuwahudumia wananchi. Waajiri wao wanawajibika kuwapa haki zao kutokana na namna wanavyotimiza majukumu yao kwa mujibu wa taratibu na miongozo ya kazi zao. Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imethibitisha si kwa maneno pekee lakini kwa vitendo kuwa ni serikali inayojali wafanyakazi kwani inathamini mchango na kazi kubwa zinazofanywa na wafanyakazi katika maendeleo ya nchi.

Moja ya eneo nyeti kwa wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi ni maboresho ya mishahara yao. Mahitaji ya nyongeza ya mishahara inatokana na uhalisia wa gharama za maisha. Kutokana na gharama za maisha, upo umuhimu wa kupitia upya viwango vya mishahara na kuviboresha hasa kwa kuzingatia mwelekeo wetu wa ukuaji wa uchumi. Rais Dkt. Samia amejipambanua kwa maneno na matendo juu ya dhamira yake ya kuboresha hali za maisha ya wafanyakazi katika maeneo kadha wa kadha, mojawapo ni nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa sekta zote yaani wa sekta ya umma na binafsi.

Mwaka 2022 akiwa na mwaka mmoja tu tangu aingie madarakani, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023, Rais Dkt. Samia aliridhia mapendekezo ya kuongeza mshahara ikiwemo kima cha chini kwa watumishi wa umma kwa asilimia 23.3. Ongezeko hilo lilipelekea serikali kutumia Shilingi 1.59 trilioni, ikiwa ni ongezeko la asilimia 19.51, ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2021/2022. Hili ni jambo kubwa sana lililofanywa na Rais Dkt. Samia kwa wafanyakazi.

Sanjari na hilo, akihutubia maelfu ya wafanyakazi Mei 1, 2025, katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Singida, Rais Dkt. Samia aliendeleza neema kwa wafanyakazi baada ya kutangaza nyongeza ya kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi wa sekta ya umma kwa asilimia 35.1. Nyongeza hii ilianza kutumika rasmi Julai 1, 2025, ambapo sasa kima cha chini kimepanda kutoka Shilingi 370,000 hadi 500,000.

"Kwa mapenzi makubwa na kwa namna mlivyoiunga mkono serikali tulipowaomba mfunge mkanda na mkaamua kujituma na kufanya kazi kwa bidii na kufanya uchumi wetu ukue kwa asilimia 5.5 mwaka huu. Kwa kuwa mcheza kwao hutunzwa mimi na wenzangu, baada ya kuangalia uchumi ulivyopanda ninayo furaha kuwatangazia kwamba, katika kuzidi kuleta ustawi kwa wafanyakazi, mwaka huu serikali itaongeza kima cha chini kwa mshahara kwa watumishi wa umma kwa asilimia 35.1," alisisitiza Rais Dkt. Samia.

Neema ya nyongeza ya mshahara haijabaki kwa wafanyakazi wa sekta ya umma pekee, neema hiyo imewashukia pia wafanyakazi wa sekta ya binafsi. Oktoba 17, 2025, serikali kupitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete alisema serikali imeongeza kima cha chini cha mshahara wa wafanyakazi wa sekta binafsi kutoka Shilingi 275,060 hadi 358,322 likiwa ni ongezeko la asilimia 33.4 ongezeko hili litaanza kutumika rasmi Januari 1, 2026.

Kimsingi, ongezeko hili litagusa wafanyakazi wa sekta binafsi katika sekta za hoteli, kilimo, afya, mawasiliano, usafirishaji, madini, shule binafsi, nishati,  huduma za ulinzi binafsi, utamaduni, uvuvi, biashara, viwanda, kutaja kwa uchache. "Ofisi yangu itaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa amri hii, kutoa elimu kwa waajiri na wafanyakazi pamoja na kufanya tathmini ya mara kwa mara ili kuhakikisha utekelezaji wake unafanyika kikamilifu, ofisi yangu haitasita kuchukua hatua kwa waajiri watakaokaidi au kushindwa kutekeleza amri hii kwa makusudi," alisema Kikwete.

Kwa ujumla, Rais Dkt. Samia na serikali yake imefanya mengi mazuri kwa wafanyakazi wa umma na binafsi. Nyongeza ya mishahara ni sehemu mojawapo tu lakini wafanyakazi wameguswa katika maeneo mengi, mathalani, kupanda vyeo na madaraja, kulipwa madai yao ya mishahara na isiyo ya mishahara kwa wakati hasa baada ya kumalizika uhakiki wa madai yao. Kwa hakika, uboreshaji wa maslahi kwa wafanyakazi una tija kubwa hasa katika kuongeza mapato ya serikali, kuchochea mzungumo wa fedha nchini na kuchagiza ukuaji wa uchumi na maendeleo kwa ujumla.

Dkt. Reubeni Lumbagala ni mwalimu wa Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga.

Maoni : 0620 800 462.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...