Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mkuu wa Mkoa Songwe Awataka Wananchi,Kamati ua Ulinzi na Usalama Kuwa Macho na Miradi ya Umwagiliaji *



NA MWANDISHI WETU

MKUU wa Mkoa wa Songwe Jabir Makame, amewataka wananchi wa mkoa huo na kamati ya Ulinzi na Usalama kuwa macho na kutocheka na yeyote anayehujumu  miradi ya Umwagiliaji.

Amesema fedha zinazowekezwa na Serikali katika miradi hiyo ni nyingi na Imelenga kupunguza umaskini kwa wakulima hivyo anayehujumu miradi ya Umwagiliaji anapaswa kuchukuliwa hatua kwa kuwa analihujumu Taifa 

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Jabir amesema hayo wakati wa hafla ya kumkabidhi mkandarasi eneo la ujenzi wa mradi wa skimu ya Umwagiliaji Naming’ongo uliopo kata ya Chitete mkoani humo.

Amesema mradi huwo wa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 24 utatekelezwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ambapo ndani ya mradi huo kutakuwa na ujenzi wa barabara za ndani, ajira zaidi ya 2000 huku wakulima zaidi ya 6000 wakiwa wanufaika wa eneo hilo.

“Wananachi na kamati ya ulinzi na usalama tuchukue hatua kwa watu wanaoharibu miundombinu ya Umwagiliaji, kamati yetu ichukue hatua ili kukomesha tabia hizo, shughuli za ufugaji zisizo rafiki na kuleta madhara katika vyanzo vya maji na kuharibu miundombinu zikomeshwe”, amesema.

Amewataka halmashauri ya wilaya hiyo kuhakikisha kunakuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi , ili mradi utakapokamilika uvutie uwekezaji katika maeneo ambayo yamepimwa na kuepusha uharibifu wa mazingira maeneo ya miradi yote ya Umwagiliaji.

Jabir amemtaka mkandarasi anayetekeleza mradi huo kuhakikisha kazi inaanza mara moja na vifaa vilivyopo eneo la mradi vifanye kazi kwa kuzingatia makubaliano yaliyofikiwa na kufanya kazi kizalendo, ili kuwezesha mradi huo kukamilika kwa muda wa  miezi 24, kuanzia Septemba mwaka 2025 hadi Septemba 2029.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Momba  Elias Mwandobo amesema, hatua ya mradi huo na miradi yote ya Umwagiliaji ni miradi ya kimkakati iliyolenga kugusa mwananchi mmoja mmoja na kubadilisha uchumi wa wilaya, mkoa na Taifa katika kuongeza uzalishaji wa chakula na kuwa na kilimo biashara.

“Tulikuwa na kilimo cha kupiga ramli kwa kutokuwa na uhakika wa mvua, miradi hii ya Umwagiliaji inatuletea kilimo cha uhakika hivyo Serikali imekusudia kuongeza tija ya uchumi kupitia kilimo.

“Wananchi wa Kasinde, Naming’ongo, Kamsamba na Msangano pia kuna miradi mikubwa ya Umwagiliaji, zaidi ya bilioni 50 zinawekezwa Wilayani hapa, haina kwa bahati mbaya imelenga kutumia Kilimo kuchochea uchumi na kuongeza uzalishaji, wananchi muwe tayari,”amesema.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Tume Raymond Mndolwa amesema utekelezaji wa miradi ya Umwagiliaji  inalenga kujibu nia njema ya uwekezaji uliofanywa na serikali ili kuiwezesha Tanzania kulisha Dunia.

Amesema  kati ya maeneo ambayo Tume inajenga miradi, ni pamoja na mabonde 22 ambapo Momba ni moja wapo na kuanzia sasa hadi Oktoba kutakuwa na kasi ya kukabidhi miradi kwa wakandarasi ili kufikia adhima ya Serikali katika sekta ya kilimo nchini.

“Mwaka 2023 Tume kulikuwa na ujenzi wa miradi 13 leo hii kuna miradi zaidi ya 700 inayotekelezwa,pia kulikuwa na ujenzi wa miradi mitano pekee wakati wa bajeti ya  mwaka 2022/23 leo hii kuna miradi  126 yenye  wakandarasi. Bajeti pekee imefikia Trilioni 1.2 na fedha ambazo Tume imepokea ni zaidi ya bilioni 492 na ndani yake kuna VAT, miradi 30 imekamilika huku zaidi ya 60 imefika zaidi ya asilimia 50 na fedha ni bilioni 492,  ni wazi matumizi ya fedha za Serikali yako vizuri na yanasimamiwa,”amesema.

Mndolwa amesema katika ujenzi huo kutakuwa na ghala la kuhifadhi nafaka na mashine za kuchakata mazao hayo.

Pia amemtaka Mkandarasi kutoa ajira kwa wazawa na  wananchi hao wawe waaminifu ili kuwa na mradi bora huku akisisitiza haja ya wananchi kulinda ardhi zao kwa kutokuuza maeneo na ameahidi kuwa Tume itashirikiana na Wilaya kupima, kutoa hati za mashamba na kuzimilikisha kwa wananchi.

Naye Mhandisi wa NIRC Mkoa wa Songwe John Chacha amesema mradi huo unaotekelezwa na Mkandarasi MBUYA’S CONTRACTORS COMPANY LTD, hatua utaongeza eneo la Umwagiliaji  kutoka hekta 1500 hadi kufikia hekta 5000. 

“Wakulima 6000 watanufaika moja kwa moja kwa kufanya shughuli za kilimo ndani ya skimu na watu zaidi ya 5000 ambao siwanufaika wa moja kwa moja, ikiwemo wafanyabiashara , watoa huduma ya zana za kilimo hivyo kuongeza tija katika uzalishaji wa mpunga kutoka tani 2.4 kwa hekta ya sasa hadi tani 25 kwa hekta

Amesisitiza kuwa hatua ya NIRC kujenga ghala na mashine za kuchakata mazao kumelenga kuongeza ukuaji wa viwanda vya kuchakata na kuongeza thamani ya mpunga, ili kuinua maisha ya wananchi ambao ni wakulima wa Chitete.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Skimu hiyo, Kredo Siwiti ameishukuru Serikali kupitia Tume na Wizara ya Kilimo kwa kuwekeza fedha zaidi ya shilingi bilioni 24, ambazo wananchi wa Kata ya Chitete watanufaika na kuwa na Kilimo Chenge tija.










Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...