Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wizara ya Kilimo Iziweshe Taasisi Kupata Zana za Kisasa - Waziri Mkuu


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo iweke utaratibu wa kuziwezesha taasisi zinazojihusisha na kilimo kwa kuzipatia zana za kisasa za kilimo ili kukuza sekta hiyo.

Amesema kufanya hivyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza tija katika shughuli za kilimo zinazofanywa na taaaisi hizo. “Mitambo hii ya kupandia, kuvunia pamoja na umwagiliaji ina gharama kubwa sana, lakini Wizara yetu ya Kilimo ikiweka utaratibu mzuri wa kuziwezesha hata kwa mkopo itazisaidia kuzalisha kwa tija.”

Ametoa agizo leo (Jumapili, Agosti 03, 2025) wakati akizungumza na wadau wa ushirika na wananchi waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Ushirika Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Ushirika, kwenye viwanja vya maonesho ya NaneNane, Nzughuni, jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wakulima kwa mwaka 2025.

Amesema taasisi kama Magereza, JKT ambazo zinafanya shughuli za kilimo zikipatiwa zana hizo kwa mikopo, zitawawezeshwa kuwa na teknolojia za kisasa jambo ambalo wasingeweza kulifanya kwa kutumia fedha zao.

Akizungumzia kuhusu ushirika, Waziri Mkuu amesema katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, yaani misimu ya kilimo ya 2023/2024 na 2024/2025, nchi imeshuhudia mafanikio makubwa yanayodhihirisha nguvu ya ushirika katika kuleta tija kwenye sekta ya kilimo na kuinua maisha ya wananchi. Amesema mafanikio hayo yametokana na juhudi za pamoja kati ya Serikali, vyama vya ushirika, na wanachama.

“Katika kipindi hicho, pembejeo za kilimo zenye thamani ya shilingi trilioni moja zimesambazwa kwa wakulima kupitia mfumo wa ushirika katika mikoa mbalimbali na pia, tani milioni 3.8 za mazao mbalimbali zenye thamani ya shilingi trilioni 6.2 zimeuzwa kupitia vyama vya ushirika.

Amesema hiyo ni dalili kwamba wakulima wameweza kupata masoko ya uhakika na bei nzuri kupitia vyama vyao na hivyo kuongeza kipato chao na kuimarisha uchumi wa maeneo yao. Ametumia fursa hiyo kusisitiza utoaji wa elimu kwa umma kuhusu dhana, historia na umuhimu wa ushirika katika kuimarisha maisha ya watu kiuchumi na kijamii.

Mapema, Katibu Mkuu wa Wizara Kilimo, Gerald Mweli alisema utendaji wa ushirika nchini uko salama na umebadilika sana hadi kufikia hatua ya baadhi ya vyama kuweza kununua mazao, kubangua na kuuza nje ya nchi.

Amesema kutokana na ufanisi unaoendelea kuonekana kwenye tasnia ya ushirika, Wizara hiyo hivi sasa inalenga kuongeza thamani na kwamba baada ya miaka mitatu ijayo, inatarajia kuona baadhi ya SACCOS zinageuka kuwa benki.

Katika hatua nyingine, Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Dkt. Benson Ndiege amemshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kusimamia urejeshaji wa mali za ushirika hali ambayo imechangia kuimarishwa kwa ushirika nchini.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu ulikuwa na hamu ya kuona ushirika unafufuka nchini. Timu uliyoiunda ya kufuatilia mali za ushirika ilifanya kazi nzuri. Sasa hivi baadhi zimeanza kufanya kazi, kwa mfano kiwanda cha Sola kilichopo Simiyu, viwanda vya KAKU, Mbogwe na Chato ambavyo tayari vimeanza kuchambua pamba,” alisema.

“Kutokana na kazi hiyo, na sisi tumejiongeza. Sasa hivi tumeanza kazi ya kutambua mali zote za ushirika na kuzisajili kwenye mfumo wa kielektroniki ili tujue iko wapi na ni ya nani. Hadi sasa tumeshasajili mali 4,990 zenye thamani ya shilingi trilioni moja. Tunataka kabla ya Desemba, 2025 mali zote ziwe zimeshasajiliwa.”

Alisema wameunda Mfumo wa Usimamizi wa Vyama vya Ushirika Tanzania (MUVU) ambapo hadi sasa, tayari wameshasajili wanachama milioni nne. “Ulitoa maelekezo tuwe na mfumo ambao kama tukitaka tuwatambue wanachama wetu iwe rahisi kufanya hivyo; tujue wako wapi, wanafanya nini na wahitaji pembejeo ya aina gani na ya kiasi gani.”

Kuhusu utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi za ghala, Dkt. Ndiege alisema hadi sasa, vyama vya ushirika vimeuza mazao yenye thamani ya sh. trilioni nne na idadi ya mazao imeongezeka na kufikia 14 kutoka matano ya awali. “Mikoa nayo imeongezeka, sasa tunao Songwe, Shinyanga na Geita ambao wanatumia mfumo huu,” aliongeza.










Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...