Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Maambukizi ya Njia ya Mkojo Yanavyowatesa Wengi Nchini


*Sababu,tahadhari na changamoto ya usugu wa dawa*


*Na Mwandishi wa Makala za Moto*

Maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) yameendelea kuwa changamoto kubwa ya kiafya kwa watu wazima, hususan wanawake, lakini pia wanaume kwa kiwango kidogo. 

Maelfu ya wagonjwa wanafika katika vituo vya afya kila mwezi wakilalamikia maumivu wakati wa kukojoa, haja ndogo ya mara kwa mara, uchafu au harufu mbaya ya mkojo, na hata homa kali.

Wengi wa waathirika hawa hupata maambukizi yanayosababishwa na bakteria anayeitwa Escherichia coli (E. coli), ambaye ameonekana kuhusika na zaidi ya asilimia 80 ya maambukizi ya njia ya mkojo duniani kote. 

Hali hii imekuwa ya kurudiarudia kwa baadhi ya wagonjwa, na hivyo kusababisha adha ya kudumu inayohitaji matibabu ya mara kwa mara, na kwa baadhi, mpaka vipimo vya maabara kama Culture and Sensitivity ili kupatikana dawa sahihi.


E. coli: Bakteria wa kawaida anayesababisha tatizo kubwa.


Kwa kawaida, E. coli ni bakteria anayeishi kwenye utumbo wa binadamu bila madhara yoyote. 

Hata hivyo, tatizo huanza pale anapohama kutoka sehemu ya haja kubwa na kuingia katika njia ya mkojo, kuanzia kwenye mrija wa urethra, kibofu cha mkojo hadi kwenye figo.

Hali hii hujitokeza zaidi kwa wanawake kwa sababu miili yao kimaumbile huwa na urethra fupi iliyo karibu na njia ya haja kubwa. Hii hurahisisha usafiri wa bakteria kutoka sehemu ya haja kubwa hadi kwenye njia ya mkojo, hasa iwapo usafi hautazingatiwa ipasavyo.

Pia, matumizi ya nguo za ndani zinazotengeneza joto na unyevu kama nailoni, kukaa na mkojo muda mrefu, au kushindwa kunywa maji ya kutosha kunachangia bakteria hawa kujijenga kwa haraka katika mfumo wa mkojo.


Usafi duni na tabia za ngono zembe nazo huchochea maambukizi hayo.


Katika mazingira ya kawaida, maambukizi haya huweza kuzuiwa kwa njia rahisi kama kuosha sehemu za siri kwa maji safi mara mbili kwa siku, na kuhakikisha usafi sahihi baada ya kujisaidia; kwa maana kujisafisha kutokea upande wa mbele kwenda nyuma (si kinyume chake).

Hata hivyo, uchunguzi umeonyesha kuwa maambukizi ya UTI huongezeka zaidi kwa watu wanaojihusisha na ngono isiyo salama.

Wanawake wanaoshiriki tendo la ndoa mara kwa mara bila kujikinga hujikuta wakipatwa na UTI kwa kurudiarudia. Hali hii hutokana na msuguano wa tendo lenyewe kuweza kusukuma bakteria waliopo sehemu ya nje ya uke kuingia kwenye urethra.

Kujamiiana na wapenzi mbalimbali, au kufanya ngono ya haja kubwa kisha kuendelea na ya kawaida bila kuosha au kubadilisha mpira wa kinga ama kondomu, kunaongeza uwezekano mkubwa wa kuingiza bakteria wa E. coli kutoka kwenye upande wa haja kubwa hadi sehemu za mbele.

Kukojoa mara moja baada ya tendo la ndoa husaidia kupunguza uwezekano wa maambukizi kwa kusafisha bakteria waliopenya urethrani. Wanawake hasa wanapaswa kufanya hivyo kila mara baada ya tendo hilo.


*Takwimu zinaonyesha ongezeko kubwa*


Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirika la Taifa la Takwimu (NBS), kati ya mwaka 2019 hadi 2023, visa vya maambukizi ya UTI viliongezeka kutoka wagonjwa 732,500 hadi 986,400. Hii ni sawa na ongezeko la asilimia 34 katika kipindi cha miaka mitano.

Takwimu hizo pia zinaonyesha kuwa zaidi ya asilimia 60 ya visa hivyo huhusisha wagonjwa wa jinsia ya kike. 

Mikoa yenye viwango vya juu vya maambukizi ni pamoja na Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na Mbeya.

Takwimu kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa E. coli husababisha zaidi ya asilimia 80 ya UTI zote duniani, na usugu wa vimelea hivi kwa baadhi ya dawa unaongezeka kwa kasi ya kutisha.


*Usugu wa dawa: changamoto ya matibabu*


Tatizo kubwa kwa sasa ni kwamba E. coli ameanza kuonyesha usugu dhidi ya dawa nyingi za kawaida ambazo zamani zilikuwa zikifanya kazi vizuri. Wagonjwa wengi hujitibu wenyewe kwa kutumia dawa za kujinunulia madukani wao wenyewe pasipo kwenda kwa madaktari (Over the Counter) lakini hawapati nafuu, na hatimaye hujikuta wakienda  hospitalini wakiwa katika hali mbaya zaidi.

Taarifa kutoka Maabara Kuu ya Taifa na Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) zimeonyesha kuwa dawa zifuatazo zimepoteza uwezo mkubwa wa kutibu UTI kutokana na usugu wa E. coli:

1. Amoxicillin – usugu wa zaidi ya 75%

2. Ampicillin, usugu wa zaidi ya 80%

3. Ciprofloxacin, usugu wa 65%

4. Trimethoprim-Sulfamethoxazole, usugu wa 70%

5. Nitrofurantoin, usugu wa karibu 35%

Kwa wagonjwa wenye historia ya UTI ya kurudiarudia, ni lazima wafanyiwe kipimo cha Culture and Sensitivity ili kubaini dawa ambayo itamfaa moja kwa moja kulingana na aina ya E. coli aliyepo mwilini mwake.


*Njia za kujikinga na UTI zinazojirudia*


Kwa kuwa kinga ni bora kuliko tiba, ni muhimu kuchukua hatua zifuatazo ili kuzuia maambukizi haya:

Osha sehemu za siri kwa maji safi mara mbili kwa siku.

Safisha baada ya haja kubwa kutoka mbele kwenda nyuma.

Kunywa maji mengi, angalau lita 1.5–2 kwa siku.

Kakojoe mara unapojisikia, usizuie mkojo kwa muda mrefu.

Kakojoe mara baada ya kujamiiana.

Vaa nguo za ndani  za pamba na pia epuka nguo za kubana kwa muda mrefu.

Tumia kinga ukiwa na mpenzi mpya au zaidi ya mmoja.Lakini pia kwa mujibu wa ushauri wa na maadili ya dini, tusiwe na mpenzi zaidi mmoja.Ukishaoa au kuolewa usitoke nje ya ndoa.

Epuka kutumia dawa pasipo ushauri wa daktari, lakini pia jenga tabia ya fanya kipimo kwanza.

Fanya uchunguzi wa mara kwa mara hasa kwa walioathirika mara nyingi

UTI zinazojirudia huathiri ubora wa maisha kwa kiasi kikubwa.

Zinapunguza uwezo wa mtu kufanya kazi, husababisha maumivu ya mara kwa mara, na kwa baadhi, huweza kusababisha maambukizi kwenye figo, jambo ambalo ni hatari kwa afya ya muda mrefu.

Watanzania wanapaswa kuacha kutumia dawa kiholela na badala yake kufuata utaratibu wa kitaalamu wa vipimo kabla ya matibabu. Serikali nayo inapaswa kuimarisha upatikanaji wa vipimo vya Culture and Sensitivity katika hospitali za mikoa na wilaya ili huduma hii isibaki kwa wenye uwezo tu.

Wakati dunia inakabiliana na tishio la usugu wa dawa, hatua binafsi na elimu kwa jamii ndiyo silaha madhubuti ya kupunguza ongezeko la maambukizi haya.


*_Mwandishi wa  Makala za Moto ameandika makala haya baada kufanya utafiti wa mwezi nzima katika akihojiana na Madaktari Bingwa mbalimbali wa Idara ya Magonjwa ya Njia ya Mkojo (Urolojia) wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.Pia amesoma machapisho mbalimbali ya Afya na Tiba_*

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...