Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt. Biteko Asema Tanzania ina Usalama wa Chakula, Awapongeza Wakulima


📌 Asema Serikali inatambua Vyama vya Ushirika ni muhimu kuunganisha nguvu za wananchi na kujiendeleza kiuchumi

📌 Mauzo ya nje ya kahawa na tumbaku 2023/2024 yaongezeka hadi Dola za Marekani 19,300,000

📌 Maono ya Rais Samia yaanza kuonekana sekta ya kilimo yachangia GDP asilimia 26

📌 Aziagiza Wizara za Fedha na Kilimo kupata ufumbuzi wa bei za mazao

Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewapongeza wakulima nchini kwa jitihada zao za kuzalisha mazao kwa wingi na hivyo  kusaidia nchi kuwa na usalama wa chakula  ikiwa ni pamoja na kuwezesha sekta ya kilimo kuwa na mchango mkubwa katika Pato la Taifa. 

Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo Julai 5, 2025 jijini Dodoma wakati akifunga Kongamano la Siku ya Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani.

“Leo sekta ya kilimo ina mchango mkubwa kwenye uchumi wa nchi yetu, tunazungumza mchango wa GDP wa asilimia 26, tunazungumza mazao ambayo yanatupa  usalama wa chakula katika nchi yetu, nchi zingine zinahangaika kupata chakula sisi watu wetu wana uhakikia wa kupata chakula mitaani kwa sababu wakulima wamewezeshwa kufanya biashara ya kilimo, ” amesema Dkt. Biteko 

Amebainisha kuwa takwimu zinaonesha  utendaji wa vyama vya ushirika  umeendelea kuimarika kila wakati mauzo ya nje   yameongezeka. Ambapo kwa mwaka 2024/2025 jumla ya vyama vya ushirika 1,084 viliuza kahawa na tumbaku moja kwa moja nje ya nchi kiasi cha Dola za Marekani 344,800,000 ikilinganishwa na Dola za Marekani 325,500,000 kwa mwaka 2023/2024 sawa na ongezeko la Dola za Marekani 19,300,000.

Dkt. Biteko amefafanua kuwa Vyama vilivyopata Hati safi ya Ukaguzi kutoka Shirika la Ukaguzi la Vyama vya Ushirika (COASCO) vimeongezeka kutoka vyama 339 mwaka 2021/2022 hadi kufikia vyama 631 mwaka 2023/2024 sawa na ongezeko la vyama 292 ambayo ni asilimia 86.13

Aidha, Vyama vilivyopata Hati isiyoridhisha vimepungua kutoka Vyama 1,198 mwaka 2021/2022 hadi kufikia Vyama 263 mwaka 2023/2024 sawa na upungufu wa vyama 935 ambayo ni asilimia 78.

Ametoa rai kwa Vyama kuwawezesha wanawake kwa kuweka mikakati mbalimbali ili idadi ya Vyama vya Ushirika vya Wanawake iongezeke kutoka Vyama 50 vilivyopo sasa.

Licha ya mafanikio hayo katika sekta ya kilimo, Dkt. Biteko ameziagiza Wizara za Fedha na Kilimo kupatia ufumbuzi masuala ya bei ya mazao ya wakulima, pembejeo na mahitaji ya msingi ya wakulima ili kuendelea kufanya kilimo chenye tija.

 “Serikali ya awamu ya Sita inatambua kwamba Ushirika ni nyenzo muhimu ya kuwasaidia wananchi katika kuunganisha nguvu zao na kujiendeleza kiuchumi. Hivyo, Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi na jitihada zote zenye lengo la kuhakikisha kuwa Vyama vya Ushirika vinasonga mbele kiuchumi na kijamii, ” amesisitiza Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa Vyama vya Ushirika vimekuwa na mchango mkubwa katika kujenga uchumi wa nchi ndio sababu Rais  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameipa msukumo mkubwa sekta ya kilimo. Pia amempongeza Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kwa kuhakikisha sekta hiyo inatimiza maoni ya Rais Samia ya kuwainua wakulima kiuchumi na kukuza uchumi wa nchi.

Vilevile, amempongeza Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege kwa kuwasema wakulima nchini na hivyo kuboresha  utendaji kazi wa Vyama vya Ushirika huku akivitaka Vyama hivyo kuwa na viwanda vya uchakataji wa mazao  ili kuongeza thamani ya bidhaa na kuongeza wigo wa masoko.

Naye, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada mbalimbali za  kuboresha sekta ya kilimo nchini ikiwa ni pamoja na kuongeza bajeti za Wizara ya Kilimo, kutoa zuruku za  mazao na kuanzisha kwa Taasisi mbalimbali ikiwemo COPRA zinazolenga kutetea maslahi ya wakulima nchini.

Aidha, Mhe. Bashe amebainisha kuwa utekelezaji wa miradi ya Serikali katika maeneo ya vijijini kama vile uwepo wa umeme katika vijiji vyote nchini na barabara unachochea maendeleo vijijii na hivyo hutoa fursa kwa wakulima kuanzisha mashine za uchakataji mafuta mfano ya alizeti na kusafirisha mazao yao.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule amesema kuwa mkoa huo sasa una Vyama vya Ushirika 244 na kwa sasa wananchi wamejua umuhimu wa vyama hivyo  hususan  lengo namba saba la kuvitaka kushirikiana na jamii.

Akitoa taarifa ya miaka mitatu kuanzia mwaka 2022/23 hadi 2024/25 ya hali ya Vyama vya Ushirika nchini, Mrajisi wa Vyama vya Ushirika nchini, Dkt. Benson Ndiege ametaja mafanikio kadhaa yaliyopatika ikiwa ni pamoja na kuanzisha Benki ya Ushirika katika mikoa minne nchini.

Naye, Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika (TFC), Bw. Tito Haule amesema kuwa Maadhimisho hayo kwa mwaka 2025 wanaushirika nchini wanaungana na wadau wengine duniani hivyo kufanya kuwa Maadhimisho ya 102 tangu kuanzishwa.

Bw. Haule ametaja baadhi ya malengo ya mwaka wa Ushirika 2025 kuwa ni pamoja na kutoa fursa kwa Vyama Vya Ushirika kuonesha bidhaa zao kwa jamii na kuhabarisha umma juu ya mchango wa Vyama hivyo na kuhimiza uwepo wa sera na desturi.

Aidha, amesema baadhi ya mafanikio ya Vyama Vya Ushirika nchini ni ongezeko la idadi ya  wanachama  kutoka milioni 6.9 mwaka 2021/22 hadi kufikia milioni 10, kuongeza ajira za kudumu na mikataba kwa vijana na kuchangia pato la kodi kwa Serikali hadi shilingi bilioni  9.5 mwaka 2020/22 na shilingi bilioni 12.5 mwaka 2023.

Pia, ameishukuru Serikali kwa kuongeza mtaji wa shilingi bilioni 5 katika Benki ya Ushirika na kuimarisha Vyama Vya Ushirika kwa kuongeza matumizi ya TEHAMA.



Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...