Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Ccm inatoa Somo Duniani Uimara Wake, Kujibadilisha Kuendana na Wakati


_Kudijitilize Chama, kurekebisha Katiba kuendana na mahitaji ya sasa._


Na Bwanku M Bwanku.

Moja ya sifa kubwa inayoweza kuifanya taasisi yoyote duniani kuendelea kuishi, kuwa imara na kushawishi kundi kubwa la watu basi ni uwezo wake wa kubadilikabadilika kulingana na muda na mahitaji ya wakati uliopo wa watu inaowahudumia. Lazima ubadilike kwenda na muda (dynamic) na sio kung'ang'ania ujima (static).

Mtaalamu wa masuala ya taasisi (Organizational Structure) Mjerumani Max Weber aliwahi kusema kwamba taasisi isiyobadilika na inayokumbatia uhafidhina (conservative) inajiandalia kifo chake yenyewe.

CCM ni moja ya Chama kikongwe na kikubwa sana sio tu Afrika bali duniani kikishiba utajiri mkubwa wa kihistoria na kitaasisi. Ni Chama cha Pili kwa ukubwa, cha muda mrefu na kikongwe zaidi Barani Afrika baada ya Chama Cha True Whig Cha Liberia kikiwa na miaka 48 toka kiasisiwe Februari 05, 1977 baada ya kuunganika kwa Vyama viwili vya Tanganyika African National Union (TANU) cha Tanganyika kilichokuwa chini ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar kilichokuwa chini ya Sheikh Amaan Abeid Karume.

Inasifika na kufahamika kama Chama Kikuu Cha Ukombozi Kusini mwa Afrika hasa kwa mchango wake mkubwa wa kusaidia Mataifa mengi sana Kusini mwa Afrika kupata Uhuru wake na kujikomboa kutoka kwa Wakoloni. Miaka ya 1977's, CCM ikiwa chini ya Hayati Mwalimu Nyerere kama Mwenyekiti wake kilisaidia sana kwa hali na mali Mataifa mengi ya Afrika kama Zimbabwe, Msumbiji, Zambia, Angola, Afrika Kusini na mengine mengi kupigania na hatimaye kupata Uhuru wake kutoka kwa Wakoloni.

Kwa ukubwa wa kitaasisi na kihistoria na umri wa miaka 48 ulionao, suala la CCM kubadilikabadilika kuendana na wakati, mahitaji ya muda husika na kuangalia watu inaowahudumia ni jambo lisilopingika ili kuifanya taasisi iendelee kuaminika zaidi kwa watu. 

CCM imeendelea kubadilikabadilika kuendana na mahitaji ya muda husika, ilipoonekana wajumbe wanaopiga kura za maoni ni wachache sana hivyo kuchochea rushwa CCM ilifanya Marekebisho ya Katiba yake kwenye Mkutano Mkuu wa CCM Taifa wa Januari 18 na 19, 2025 na kuongeza idadi ya wapiga kura za maoni ili kutoa wigo mpana kwa wanaCCM kuchagua mtu anayekubalika. 

Pia, ilipoonekana majina matatu ni machache kupigiwa kura za maoni hasa kwa kuangalia jinsi wanaCCM wengi wenye sifa tofauti tofauti walivyojitokeza kuchukua fomu, CCM imebadilika haraka na kufanya Marekebisho ya Katiba yake na kuongeza idadi ya majina kuwa zaidi ya matatu.

Na wiki hii, jana Jumamosi Julai 26, 2025 CCM imeandika historia ya kuwa Chama cha kwanza Afrika kufanya Mkutano Mkuu wake Maalum uliofanya maamuzi mazito yanayokiletea mageuzi makubwa Chama kupitia njia ya mtandao kikikutanisha Wajumbe wake 1915 kati ya 1931 wa Mkutano Mkuu kutoka mikoa yote 31 ya Tanzania. 

Hili si tu limefanya mageuzi makubwa ya kidijitali kukutanisha wanaCCM nchi nzima kwa njia ya mtandao lakini Mkutano Mkuu huu Maalum umefanya mabadiliko madogo ya Katiba ya CCM ili kuendana na nyakati hizi tulizonazo. Nimeandika hapa, uhai na uimara wa taasisi yoyote ile duniani basi ni uwezo wake wa kubadilika haraka kulingana na wakati, watu inaowahudumia na mahitaji ya muda husika na sio kukumbatia uzamani. 

Kwa Mujibu wa Mwenyekiti wa Chama hiki na Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Mkutano Mkuu wa CCM uliofanyika Mei 28 na 29 mwaka huu alisema hadi kufikia Mei 29 mwaka huu, idadi ya wanachama wa chama hicho ni Milioni 13, 000, 670. Wanachama hawa wote wako kwenye kanzidata ya pamoja kwenye mfumo wake wa CCM APP na wote wanatambulika popote walipo na wanapewa kadi ya kisasa ya kielektroniki.

CCM ni moja ya Chama kinachoongoza kwa kua na wanachama wengi Barani Afrika na ina utajiri mkubwa sana wa wanachama humo ndani kuna wasomi wakubwa, maprofesa, madaktari na kila aina ya wanachama wenye sifa tofauti na wanaotaka kutumikia wananchi kwa njia mbalimbali au kushiriki maamuzi muhimu ndani ya Chama. 

Ili kuendana na mahitaji ya sasa na kuhakikisha kila mwanaCCM anakua sehemu ya maamuzi muhimu ndani ya Chama, ikafanyia marekebisho kidogo kwenye Katiba yake ili kuongeza wigo wa idadi ya wanachama wanaopiga kura kuamua wagombea ubunge na udiwani.

Katika dhana ileile ya kubadilika haraka kwenda na muda na mahitaji ya watu unaowahudumia, kwenye Mkutano Mkuu wa CCM wa Januari 18 na 19, 2025 uliofanyika ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma palifanyika Marekebisho ya Katiba ya CCM kwenye Ibara ya 47 (1), 60 (1) na 73 (1) ambapo Wajumbe wanaopiga kura za maoni waliongezwa kutoka wale wa mwanzo. Lakini pia marekebisho mengine yalikua yale ya kurudisha majina matatu tu kwa ajili ya kupigiwa kura za maoni.

Mfano, lipo Jimbo lilikua na wapiga kura za maoni labda 800 lakini kwa mabadiliko haya Wajumbe walifika zaidi ya Elfu 10. Vivyo hivyo kwa upande wa udiwani wapiga kura za maoni waliongezwa na kuwa wengi zaidi. Hii inapunguza rushwa kwani Wajumbe wachache ilikua rahisi kwa wachache wasio waadilifu watafuta uongozi kwa fedha na rushwa kuwafikia lakini leo jimbo lina mpaka wapiga Elfu 10 hapo hata mtoa rushwa lazima achemke.

Wajumbe sasa wa kupiga kura za maoni wengi zaidi na mabadiliko hayo yanakwenda katika utaratibu wa kuchuja wagombea na itapandisha ngazi ya juu wagombea watatu labda kamati itaona vinginevyo. Lengo likiwa kuongeza ushiriki wa wanachama kufanya maamuzi, kutanua wigo wa demokrasia kwa wanaCCM, kuimarisha muundo wa ngazi ya shina pamoja na kudhibiti vitendo vya rushwa.

Baada ya kupitisha mabadiliko yale ya kuruhusu majina matatu tu kwenda kupigiwa kura za maoni, pamekua na maoni mengi ya wanachama na wananchi kuhusu uchache wa majina ya kupigiwa kura za maoni hasa ukizingatia CCM ina utajiri mkubwa sana wa wanachama na tumeona jinsi makundi mengi ya wasomi, watumishi, wanamuziki, wachekeshaji, waigizaji yalivyojitokeza kuchukua fomu kuomba nafasi za ubunge na udiwani mwaka huu 2025.

Katika kubadilikabadilika kwenda na wakati, tena CCM imerudi kwenye Mkutano Mkuu wa CCM kufanya marekebisho madogo ya Katiba yake ili kwenda na nyakati na aina ya watu inaowahudumia. 

Na marekebisho ya Katiba kwenye upande wa majina ya watu walioomba kugombea ubunge na udiwani ambapo licha ya majina ya wagombea wanaoteuliwa ngazi ya Kamati za Siasa za Wilaya na Mkoa kubaki matatu kwa kila Jimbo na Kata, kwa marekebisho haya madogo ya Katiba, Kamati Kuu itakuwa na uwezo wa kubadilisha maamuzi endapo itaamua vinginevyo.

Akisoma marekebisho hayo kwenye Mkutano Mkuu Maalum uliofanyika kwa njia ya mtandao Jana Julai 26, 2025 Jijini Dodoma, Katibu wa NEC- Organizesheni Issa Haji (Gavu), amesema Marekebisho yaliyofanyika na kubarikiwa na Mkutano Mkuu huu ambao ndicho chombo chenye mamlaka kufanya hivyo ni Marekebisho ya Katiba ya CCM Ibara ya 105 ibara kuu ya 7 F kwa kuongeza maneno  "isipokuwa kama Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa itaamua vinginevyo."

Hivyo Ibara ya 105 ibara kuu ya 7 F ya CCM inapendekezwa isomeke kama ifuatavyo "Kufikiria na kuteua majina ya Wana CCM wasiozidi watatu kwa kila Jimbo la uchaguzi walioomba nafasi ya Ubunge na Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi ili wakapigiwe kura isipokuwa kama Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa itaamua vinginevyo."

"Kwa upande wa udiwani inapendekezwa kufanya marekebisho kwenye ibara ya 91 6C  kwa kuongeza maneno isipokuwa kama Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa itaamua vinginevyo hivyo mapendekezo yatasomeka "kwa upande wa udiwani itafikiria na kuteua majina ya Wana CCM wasiozidi watatu kwa kila Kata ili wakapigiwe kura za maoni isipokuwa kama Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa itaamua vinginevyo."

Marekebisho haya yote yamepitishwa na Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum uliofanyika kwa njia ya mtandao kwa asilimia 99.8 na sasa yanatumika rasmi. 

Marekebisho haya yote ya Katiba ya CCM yanakifanya Chama kuendana na hali ya sasa ya Chama ili kutoa fursa kwa wanaCCM wengi zaidi. Na hii inadhihirisha CCM inavyotoa darasa la kubadilikabadilika haraka kuendana na mahitaji ya wakati husika na watu inaowahudumia.

Ukubwa wa historia yake, kitaasisi kubadilikabadilika kulingana na wakati na mahitaji ni jambo lisilopingika kwa CCM ili kuendelea kuimarika na kuaminiwa zaidi na kwenye hili imethibitisha kwa vitendo.











*MAKALA HII IMEANDIKWA NA NDUGU BWANKU M BWANKU. KWA MAONI, USHAURI ANAPATIKANA KWA EMAIL bwanku55@gmail.com

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...