Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Samia Atimiza Ndoto ya Miaka 50 ya Taifa ya Kuwa na Umeme wa Uhakika Kutoka Bwawa La Mwalimu Nyerere


 _Rasmi mashine zote 9 za kuzalisha umeme Megawatts 2,115 zimekamilika, ndoto ya miaka 50 Rais Samia ameitimiza kwa miaka 4 tu kutoka kuukuta mradi ukiwa chini ya 33% hadi kuumaliza 100%._


Na Bwanku M Bwanku.

Moja ya mradi mkubwa wa kimkakati uliokua ukitekelezwa kwenye nchi yetu ni mradi wa kufua umeme kwa kutumia njia ya maji maarufu kama Mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere kwenye Mto Rufiji kule mkoani Pwani (Julius Nyerere Hydroelectric Power Project- JNHPP).

Mradi huu ni wa 4 kwa ukubwa barani Afrika na umegharimu Trilioni 6.5 ukiwa na mashine 9 ambazo zote kwa pamoja zinazalisha Megawatts 2,115. 

Kihistoria, mradi huu ulibuniwa na kuasisiwa mwaka 1975 takribani miaka 50 iliyopita na Rais wa Awamu ya kwanza wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuanza kutekelezwa na Serikali ya Awamu ya 5 chini ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na sasa kukamilishwa kwa haraka na Serikali ya Awamu ya 6 chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Waziri wa Nishati na Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dotto Biteko Jana Aprili 05, 2025 alitembelea mradi huo na kulitangazia Taifa kwamba rasmi sasa mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere umekamilika rasmi na mashine zote 9 za kuzalisha umeme zimekamilika.

"Tumekuja leo tukiwa na furaha kubwa kwamba mitambo yote tisa imekamilika inazalisha umeme na nina furahi kuwajulisha Watanzania kuwa ile ndoto na shauku ya kuwa na umeme wa uhakika kutoka kwenye chanzo hiki kikubwa barani Afrika imekamilika, kazi iliyobaki ni kuimarisha miundombinu ya kuwafikishia watanzania umeme

"Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Misri kuuzindua rasmi." Waziri Biteko ameyasema hayo Jana April 5, 2025 baada ya kutembelea Mradi huo akiwa ameambatana na Mawaziri ambao ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Hamadi Masauni

Kwa Mujibu wa Wizara ya Nishati, mahitaji ya umeme kwenye nchi yetu hadi sasa ni wastani wa Megawatts 1908.15. 

Kwasasa toka tupate Uhuru mwaka 1961, nchi yetu nzima kutoka kwenye vyanzo vyetu vyote vya kuzalisha umeme vya Kinyerezi, Kidatu, Mtera, Nyumba ya Mungu, Songosongo na kwingine, tunazalisha Megawatts wastani 1800 na zisizodi 2,000 lakini bwawa la Mwalimu Nyerere pekee yake linakwenda kutupa megawatts 2,115 za umeme wa uhakika tena wa maji ambao ni wa gharama nafuu zaidi kuliko aina yoyote ile ya umeme duniani ukiachana na umeme wa jua, upepo, nyuklia, makaa ya mawe, mafuta na gesi. 

Umeme wa bwawa hili pekee yake unatosha Taifa zima na kwahiyo kwasasa ukichanganya na umeme tunaozalisha kwenye vyanzo vingine nilivyovitaja pale juu maana yake Tanzania rasmi ina utoshelevu wa umeme kwa matumizi yake ya majumbani, viwanda na kwingine na hivyo tuna ziada ya umeme kufikia zaidi ya Megawatts 1,800. 

Na sasa kutokana na nchi kuwa na uwezo wa kuzalisha umeme kwa kiwango kikubwa sasa Serikali iko katika mchakato wa kukamilisha mazungumzo na nchi ya Zambia na Malawi kwa ajili ya kuwauzia umeme ili Taifa lipate mapato yatakayoenda kufanya shughuli zingine za maendeleo na tayari njia ya umeme ya kuunganisha nchi hizo imeanza kujengwa. 

Rais Samia anaweka histora ya kuua upungufu na mgao wa umeme kwa Watanzania uliotokana na kuwa na uzalishaji mdogo wa umeme.

Hivi sasa mitambo yote 9 ya kuzalisha umeme imekamilika na inafanya kazi. Kwa mujibu wa Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wanaosimamia mradi huu, wakati Rais Samia Suluhu Hassan anaingia madarakani Ijumaa Machi 19, 2021, mradi huu ulikuwa umefikia asilimia 33 tu ukiwa umetekelezwa kwa takribani miaka 4 lakini mpaka sasa kwa miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan mradi umekamilika wote.

Kwa mujibu wa Waziri wa Nishati na Naibu Waziri Mkuu, Dkt. Dotto Biteko amesema upungufu wa umeme uliokuwepo siku za hivi karibuni hasa mwishoni mwaka 2023 ulikua kati ya Megawatts 300 hadi 400 lakini mitambo yote 9 ya mradi itazalisha Megawatts 2,115 hivyo kuua kabisa upungufu wa umeme nchi hadi kuwa kiwango kikubwa cha ziada ya umeme cha kuuza nje ya nchi.

Miaka minne tu ya uongozi wa Rais Samia umekamilisha ndoto za miaka 50 ya Taifa kuwa na umeme wa uhakika tena wa maji ambao ni nafuu zaidi. Hatua zote muhimu zikikamilika ikiwemo kujaza maji kwenye bwawa hili kubwa sana, kujenga tuta kuu pamoja na hatua muhimu zaidi ya kuwasha Mitambo na kuingiza moja kwa moja umeme kwenye Grid ya Taifa ili kuondoa changamoto ya upungufu wa umeme iliyokuwepo huko nyuma. 

Huu ni mradi mkubwa wa kimkakati ambao kukamilika kwake kunalihakikishia Taifa utoshelevu wa umeme na sio utoshelevu pekee yake bali unafuu wa umeme kwani umeme wa maji ndiyo umeme nafuu zaidi kuliko yote duniani.

Umeme unaozalishwa na maji ndio umeme wa gharama nafuu na rahisi zaidi kuliko umeme wowote ule duniani. Uniti 1 ya umeme inayozalishwa na maji ni shilingi 36 tu lakini umeme unaozalishwa na nyuklia Uniti 1 ni shilingi 65, umeme wa upepo shilingi 103.5, wa jua shilingi 103.5, wa makaa ya mawe Uniti 1 shilingi 114, wa joto ardhini 118, umeme wa gesi Uniti 1 shilingi 147 na wa mafuta ndio wa gharama kubwa zaidi ambao wenyewe Uniti 1 gharama yake ni juu sana kati ya shilingi 440 hadi 600.

Hii maana yake ni kwamba kukamilika kwa mradi huu wa Mwalimu Nyerere tutakuwa na Megawatts za umeme zaidi ya 3,000 na moja kwa moja kujihakikishia kama Taifa umeme wa kutosha na kuua hadithi za mgao wa umeme na uhaba wake, utakaolifanya Taifa kupitia wananchi na wawekezaji sasa kufanya shughuli zake za uzalishaji na zingine bila changamoto yoyote ile.

Kuwa na umeme wa uhakika kama huu wa maji tunaozalisha pale Rufiji, tayali unavutia viwanda na shughuli nyingi za kiuchumi ikiwemo wawekezaji wengi zaidi kuja kujenga viwanda hapahapa. Mwekezaji yeyote anayefikiri kwenda kuwekeza sehemu yoyote ile duniani lazima awe na uhakika wa nishati kwasababu kiwanda ni nishati.


Chini ya Serikali ya Rais Samia hakuna kinachosimama wala kukwama.

Kukamilika kwa mradi huu mkubwa kabisa wa kufua umeme unaleta ukombozi mkubwa sana wa kiuchumi hasa wakati huu nchi yetu ikiwa kwenye ujenzi wa uchumi wa viwanda, shindani na wenye kuleta maisha bora kwa watu ambao kwa kiwango kikubwa unategemea sana nishati ya umeme ya kuwezesha viwanda kupata nishati ya kutosha ili iweze kuzalisha vya kutosha na muhimu zaidi kwa gharama nafuu.

Unapokuwa na umeme wa uhakika, lakini sio wa uhakika tu tena na wa gharama nafuu ya bei kama huu wa maji tunaozalisha Rufiji, tayali unavutia wawekezaji wengi zaidi kuja kujenga viwanda hapahapa. Suala la uhakika wa umeme na nafuu yake ni mambo ya msingi sana na ya kwanza kabisa kwa mwekezaji yeyote anayefikiri kwenda kuwekeza sehemu yoyote ile duniani kwasababu kiwanda ni nishati.

MAKALA HII IMEANDALIWA NA KUANDIKWA NA BWANKU MUSA BWANKU AMBAYE NI AFISA TARAFA WA TARAFA YA KATERERO ILIYOPO BUKOBA MKOANI KAGERA. ANAPATIKANA KWA EMAIL bwanku55@gmail.com

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...