Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Hakuna Maendeleo Yanayowezekana Bila Amani na Mshikamano wa Kitaifa - Dkt. Biteko


📌 Asisitiza uwekezaji katika elimu inayozingatia sayansi, teknolojia na ubunifu

📌 Awasihi Watanzania kuziishi falsafa za Mwl. Nyerere

📌 Chuo cha Mwl. Nyerere cha adhimisha miaka 103 ya kuzaliwa kwa Mwl. Nyerere


Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewaasa Watanzania kuendeleza fikra za Mwl. Nyerere kwa kuwekeza katika sekta za elimu, kilimo, viwanda, teknolojia na biashara ndogo ndogo zinazotegemewa na wananchi wengi ili kukuza uchumi jumuishi. 

Aidha, Serikali na sekta binafsi zinapaswa kushirikiana ili kuhakikisha uwekezaji unaleta tija kwa wananchi wa kawaida.

Dkt. Biteko amesema hayo leo Aprili 11, 2025 jijini Dar es salaam wakati aliposhiriki katika Kongamano la Kumbukizi ya Kuzaliwa Kwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

Amesema Kongamano hilo lenye mada inayosema Maono ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Elimu, Uwekezaji na Ujenzi wa Taifa lenye Amani kwa Maendeleo ya Watu ni fursa ya kufanya tafakuri kwa baadhi ya mambo ambayo Baba wa Taifa aliyaamini, aliyaishi na anaendelea kukumbukwa nayo.

“Maono ya Mwalimu kuhusu uwekezaji kwa maendeleo yalilenga kuimarisha uchumi wa Taifa kwa misingi ya usawa na uwajibikaji wa pamoja. 

Alisisitiza kuwa uwekezaji lazima uwalenge wananchi na kuhakikisha kwamba rasilimali za Taifa zinatumika kwa manufaa ya wote. Alipinga mifumo ya kiuchumi inayozalisha matabaka na ukosefu wa haki, huku akihimiza ujamaa na kujitegemea,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa Mwl. Nyerere alitamani kuona elimu inampa mwanafunzi maarifa ya kumwezesha kuchangia maendeleo ya jamii yake na sio ya kumtenga na mazingira yake. Aidha, jamii inapaswa kujiuliza ikiwa sasa elimu inawajenga Watanzania kuwa raia wenye uwezo wa kutatua matatizo yao na kuchangia maendeleo yao na ya Taifa kwa ujumla.

Amebainisha kuwa katika dunia ya sasa yenye ushindani mkubwa wa kiteknolojia na kiuchumi, ni muhimu kuwekeza katika elimu inayozingatia maendeleo ya sayansi, teknolojia, ubunifu na stadi za maisha ili kujiletea maendeleo ya kweli.

Akizungumzia umuhimu wa amani, Dkt. Biteko amesema kuwa hakuna maendeleo yanayowezekana bila amani na mshikamano wa kitaifa. 

“Kupitia misingi ya utaifa na umoja, aliweza kujenga Taifa lenye mshikamano thabiti licha ya tofauti za kikabila, kidini, na kijamii. Leo taifa letu linanufaika na amani, umoja na upendo wa kindugu ambavyo Baba wa Taifa alivijenga kwa juhudi kubwa,”amesema Dkt. Biteko.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi wa Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania Bara, Mhe. Stephen Wasira ameelezea sifa na jitihada mbalimbali alizofanya Mwalimu Nyerere wakati wa harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika kutoka kwa wakoloni.

“Aliunganisha nchi zetu kwa sababu aliamini Afrika lazima iwe moja, aliaamini katika umoja, leo tunakumbuka miaka 103 ya kuzaliwa kwake, kiongozi ambaye aliongoza Taifa hili kwa miaka 24,” amesema Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo.

Naye, Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere, Prof. Haruni Mapesa amesema kuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hakuwa kiongozi wa kitaifa pekee bali kimataifa na aliyeweka misingi muhimu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Amesema Chuo hicho kilianzishwa na Mwl. Nyerere na baadaye kuwa Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere na kina dira ya kuwa kitovu cha utoaji wa elimu bora na kuendeleza amani nchini.

Amebainisha kuwa Chuo hicho cha Mwl. Nyerere kimekuwa na desturi ya kufanya makongamano hayo kila mwaka kwa lengo kuenzi, kuzungumza na kupigia debe mawazo na falsafa na misingi yake katika Taifa.

“ Mwalimu aliamini  kuwa elimu ni nyenzo kuu ya uongozi na alisisitiza elimu ya kujitegemea. Leo tunapomuenzi tujiulize je tunazifuata falsafa zake za elimu kuwaandaa vijana kwa ajili ya maendeleo ya Taifa au kuwa watafuta ajira,” amesema Prof. Haruni.

Pamoja na hayo, ametaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana chuoni hapo katika kipindi cha uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ni maboresho makubwa ya miundombinu ya kujifunza na kufundishia.

Licha ya maboresho hayo, Prof. Mapesa amesema Chuo hicho kinaendelea na ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo ya maktaba ya kisasa itakayo hifadhi machapisho mbalimbali yenye tija kwa Taifa.

Ameongeza kuwa Chuo hicho kinatimiza lengo la Mwl. Nyerere la kuhakikisha watoto wa Kitanzania wanapata elimu ya sayansi ya jamii, uzalendo na uongozi katika maeneo mbalimbali waliyopo, na kuwa sasa wana wahadhiri wenye shahada ya uzamivu wafikao 59 na wengine wakiendelea na masomo na ndani ya kipindi cha miaka miwili watakuwa na wahadhiri wenye shahada ya uzamivu 100.

Aidha, kupitia Kongamano la mwaka huu kumekuwa na mashindano ya insha kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari  juu ya Mchango wa Mwalimu Nyerere kuhusu Elimu ya Kujitegemea katika Maendeleo ya Taifa. 

Lengo la mashindano hayo ni kuwafanya vijana kuendelea kujifunza kuhusu falsafa za Baba wa Taifa na kuzitumia ambapo Dkt. Biteko alikabidhi zawadi kwa washindi pamoja na yeye kutunukiwa tuzo na Chuo hicho. 





Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...