Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Butiku-Rais Samia Amefanya Mambo Makubwa,Aungwe Mkono


-Ampa asilimia 85 kiutendaji

-Ashangaa wanazungumzia ukubwa wa deni la taifa bila kujivunia miradi iliyopo

-Atoa heko kwa CCM  kumteua kuwa mgombea wake 

-Awaonya Chadema,asema hakuna mwenye mamlaka kuzuia uchaguzi


Na George Marato-gmtv

Mwenyekiti wa taasisi ya Mwalimu Nyerere mzee Joseph Butiku,amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo,ikiwemo inayolenga kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi hapa nchini.

Mzee Butiku ameyasema hayo ofisini kwake jijini  Dar es Salaam katika mahojiano maalum,ambapo amesema kazi kubwa ya utekelezaji wa miradi hiyo hasa ya sekta ya nishati,maji,elimu,afya,Reli na barabara katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia imewaziba midomo baadhi ya watu.

Amesema kuwa hakuna ubishi kuwa Rais Samia ameonesha utashi na mapenzi makubwa kwa taifa lake hasa katika kukamilisha miradi mikubwa ya kimkakati ukiwemo wa Reli,Bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere na ujenzi wa madaraja makubwa likiwemo la Busisi.



Amesema mbali na kutekeleza miradi hiyo mikubwa,serikali ya awamu imesimamia vema katika suala la haki na usawa kwa kila mtanzania na kutoa uhuru wa watu kujieleza na kwamba,bado kuna tatizo kwenye eneo la maadili ambalo pia linahitaji nguvu ya pamoja kati ya serikali na wananchi.

"Hili la maadili hatuwezi kumtwisha mzigo Rais wetu,hili letu,wewe ni baba au mama una wajibu wa kutoa maelezi katika familia yako,tukifanya hivi hata vitendo vya rushwa vitakwisha,....mtoto anatoka chuo kikuu ananza kazi tu ananunua gari ya kifahari na kujenga nyumba nzuri,wewe mzazi unashangilia badala kumuuliza pesa hizo kwa mwaka mmoja tu amezitoa wapi kama sio mwizi" alisema mzee Butiku

Kwa sababu hiyo mzee Butiku amewaomba watanzania kuendelea kumpa ushirikiano  Rais Samia na serikali yake ili iweze kutimiza wajibu wake wa kuwaletea wananchi maendeleo wanayokusudia.

"Mimi si mtu wa kusifia sifia viongozi hasa Rais kwani ni wajibu wake kufanya hivyo,lakini kwa kazi hii kubwa anayoifanya Rais wetu(Samia) katika usimamizi na ujenzi wa miradi hii mikubwa nasema wazi kabisa nampongeza sana,amefanya kazi kubwa kwa taifa letu"alisema Butiku na kuongeza.

"Zamani kwenye uongozi tulikuwa tunatoa maksi(alama) si hizi zenu za siku hizi,kwa sababu hii na kuridhishwa kwangu na kazi anazofanya Rais wangu, nampa alama 85,nasema wazi kibisa,nampa 85 anastahili kabisa na hizo kumi na tano zilizobaki ni zetu nasi tufanye kumsaidia Rais"alisema.

Kuhusu kukuwa kwa deni la   taifa,mzee Butiku amesema hawezi kushangaa kuongezeka kwa deni hilo kutokana na miradi mikubwa iliyojengwa nchini.

Alisema miradi mingi ilihitaji fedha nyingi ili iweze kukamilika na si kosa kwa serikali kukopa na kujenga miradi kama hiyo ya reli,bwawa la mwalimu Nyerere na madaraja makubwa ambayo yataleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi.



"Kosa ambalo serikali inafanya haitaki kuwaambia wananchi kuwa deni hili linatokana na hiki na hiki,serikali imefanya mambo makubwa sasa lazima ikope ili kutekeleza hayo na lazima serikali itoe elimu kwa wananchi wajue fedha hizo hazijakopwa na Samia (Rais)kwenda kujenga nyumba yake,zimekopwa na serikali zimeingia kwenye miradi ikiwemo ya treni hii tunayofurahia ndio matunda yake"alisema mzee Butiku

Hata hivyo mzee Butiku alishauri serikali  kuharakikusha miradi ya makaa ya mawe na ule wa chuma cha Liganga ambayo amesema inaweza kulisaidia sehemu kubwa taifa hili.


"Pamoja na miradi hiyo ambayo ingeweza kutuingizia fedha za kigeni lakini pia tuna wajibu kama Watanzania kufufua viwanda vya nguo,tulime mazao kwa wingi yakiwemo ya Pamba,katani  mbaazi na mengine,haya yanaweza kutuingizia fedha nyingi za kigeni na hivyo kuiuza uchumi wetu.




Katika mahojiano hayo mzee Butiku ambaye pia ni kada mtiifu wa chama cha mapinduzi CCM,ametoa maoni yake kuhusu kuteuliwa kwa Rais Samia kugombea Urais kupitia chama  hicho amesema jambo hilo limefanyika kwa wakati mwafaka na kupongeza uamzi wa mkutano mkuu wa CCM.

"CCM  ina taratibu zake za kumpata mgombea wake  wa Urais,siku ile mimi nilipewa mwaliko bahati mbaya sikuwa sawa kiafya hivyo sikwenda Dodoma lakini niliona kwenye runinga,mambo yote yalikuwa wazi,hoja ilipotolewa,viongozi hawakuiubali pale walijua wangekiuka taratibu,walihairisha mkutano ule kwa muda wakaenda kufuata taratibu na baada ya hapo uamuzi  ukafanyika hivyo ccm haijakosea hata kidogo kwa  jambo hilo"alisema Butiku.

Mzee Butiku ametumia mahojiano hayo pia kuonya kikundi au watu wenye nia ovu kutaka kuzuia uchaguzi mkuu wa madiwani,wabenge na Rais huku akisema hakuna mwenye mamlaka wa kufanya hivyo.

Amesema kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imatoa nafasi kila baada ya miaka mitano wananchi wanapata haki ya kuchaguzi viongozi wao,hivyo hakuna mwenye mamlaka ya kuwapora haki hiyo wananchi.

"Nimesikia mara No reform no Election,hii haikubaki hata kidogo,hakuna mwenye mamlaka ya kuzuia uchaguzi,kama wanadhani kuna mifumo haipo sawa wakae wazungunze na kama jambo ni kubwa baada ya uchaguzi jambo hilo lirekebishwe kakini kamwe hakuna mtu au taasisi ya kuzuia uchaguzi huu sasa"akisema mzee Butiku.



Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...