Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali Yaagiza Magereza Kupewa Ruzuku ya Nishati Safi ya Kupikia



📌 Dkt. Biteko atoa mabati 300 ujenzi wa darasa Chuo cha Mafunzo

📌 Magereza yapongezwa kutumia Nishati Safi ya Kupikia

📌 Dkt. Samia apongezwa kwa kuimarisha vyombo vya ulinzi na usalama


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameilekeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kutoa ruzuku kwa Jeshi la Magereza ili kutekeleza maelekezo ya Serikali kuhusu matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia na kuhakikisha  Magereza yote yanaondokana na Nishati isiyo safi.

Dkt. Biteko ametoa agizo hilo leo Machi 28, 2025 jijini Dar es salaam katika hafla ya kufunga Mafunzo ya Uongozi  Ngazi ya Juu  Namba 27 - 2024/2025  katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCTA).

“ Magereza yote 129 yamehama katika matumizi ya kuni na sasa yanatumia nishati safi ya kupikia. Naielekeza REA ile ruzuku tunayopanga kuitoa kwa wazalishaji mbalimbali kwa ajili ya vifaa vya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia Magereza wapewe kipaumbele,” amesema Dkt. Biteko.

Amewapongeza wahitimu hao wa Mafunzo ya Uongozi  Ngazi ya Juu  Namba 27 - 2024/2025 na kusema kuwa ni mategemeo ya Serikali na jamii kuona wanakuwa chachu ya mabadiliko katika utendaji kazi na kuimarisha mshikamano katika Jeshi la Magereza.

“ Mkuu wa Chuo ametuthibitishia kuwa mmefanya vizuri katika mafunzo yenu. Na mmekidhi vigezo vya kupandishwa cheo na Mamlaka husika kuwa Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Magereza. Hongereni sana kwa hatua hii kubwa, pamoja na pongezi hizi naomba niwakumbishe kupandishwa cheo ni kuongezewa majukumu,” ameeleza Dkt. Biteko.

Pamoja na hayo amewataka wahitimu hao kuwasikiliza na kuwatendea haki kwa askari walio chini yao sambamba na kuwawajibisha wavivu na kuwatia moyo wachapakazi.

Vilevile, Dkt. Biteko ametoa rai kwa wahitimu hao kujiendeleza kielimu na kufanya kazi kwa bidii ili Jeshi la Magereza kuwa la mfano na kutoa huduma bora kwa Watanzania ili kufikia matarajio ya Serikali.

 “Kamishna wa Jeshi la Magereza endelea kuwaunganisha na kuweka pamoja askari, Serikali inatambua kazi unayofanya na mchango wako kwa Taifa, Serikali inatambua mchango wa Chuo hiki kwa askari wote, amesema Dkt. Biteko.

Akizungumzia Haki Jinai, Dkt. Biteko amesema “ Niuombe uongozi wa Jeshi,kuendelea na jitihada za kuboresha utendaji kazi ndani ya Jeshi katika nyanja mbalimbali na utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Rais ya Kuboresha Haki Jinai ili kulifanya Jeshi liendane na wakati kwa kuzingatia mabadiliko ya sayansi na teknolojia.“

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amechangia mabati 300 kwa ajili ya  ukamilishaji wa ujenzi wa darasa katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Mhe. Vicent Mbogo amempongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha vyombo vya usalama ikiwemo Magereza. Pia amempongeza Mkuu wa Magereza kwa kuwa na ubunifu wa kuwapeleka wafungwa katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) ambapo huwasaidia kupata ujuzi mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo amemshukuru Mkuu wa Jeshi la Magereza, Kamishna Jenerali Jeremiah Katungu kwa kusaidia mkoa wa Dar es salaam kuendelea kuwa salama.

“ Tunamshukuru Kamishna Jenerali kwa mchango mkubwa anaoutoa katika mkoa wetu wakati wa shughuli mbalimbali, hata Maafisa hawa waliohitimu leo wamekuwa na mchango katika kusaidia usalama wa Mkoa huu,” amesema Mhe. Mpogolo.

Mkuu wa Jeshi la Magereza, Kamishna Jenerali Jeremiah Katungu amesema hali ya magereza nchini ni shwari na kuwa Jeshi hilo limeendelea kutekeleza mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai.

Amesema Magereza 66 yana huduma za Mahakama Mtandao na kuwa tayari wamepokea shilingi milioni 668.8 kwa ajili ya kujenga Magereza Mtandao katika Magereza yote nchini ili kusaidia upatikanaji haki kwa wakati.

“ Nawashukuru na kuwapongeza wahitimu wote, utendaji wenu wa kazi uakisi yale yote mliyojifunza katika nyanja mbalimbali na Jeshi halitaacha kuchukua kwa yeyote atakayekiuka,” amesema Kamishna Jenerali Katungu.

Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCTA), SACP Wilnton Kahumuza amesema Mafunzo hayo ya Uongozi Ngazi ya Juu Na. 27 yalianza Novemba 30, 2024 yakiwa  na idadi ya wanafunzi 203. 

Ameendelea kusema Mafunzo hayo yalilenga kuwapatia wanafunzi ujuzi mbalimbali ili kuleta ufanisi katika utekelezaji wa  majukumu mbalimbali ndani ya Jeshi kwa kadri itakavyohitajika.

“ Wahitimu wanaohitimu leo wamefanya mafunzo ya darasani na wanastahili kupandishwa cheo kwa masomo waliyosomea,” amesema SACP Kahumuza.

Pia, amewashukuru wahitimu hao kwa kuonesha  kujituma na kuwa na moyo wa kuchanga fedha shilingi 7,703,200 kwa ajili ya kujenga mnara wa tenki la maji na kununua tenki lenye ujazo wa lita 5,000.





Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...