Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt.Mpango Ataka Afrika Kubuni Njia Bora Uendelezaji Rasilimali za Nishati ili Kukidhi Mahitaji


 

📌 *Asema upatikanaji wa Nishati Afrika bado ni mdogo kulinganisha na Mabara mengine*

📌 *Asisitiza uendelezaji wa vyanzo vya Nishati uzingatie mustakabali wa vizazi vijavyo*

📌 *Afungua Kongamano na Maonesho ya Petroli kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAPCE’25)*


Makamu wa Rais, Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango amesema kuwa matumizi ya nishati katika Bara la  Afrika hasa Kusini mwa Jangwa la Sahara  bado ni madogo ikilinganishwa na maeneo mengine kama Bara la Amerika, Asia na Ulaya hivyo kuna umuhimu wa kubuni njia bora za kuzitumia rasilimali zilizopo ikiwemo Mafuta na Gesi Asilia ili kuwawezesha wananchi kustawi kiuchumi na kijamii huku suala la utunzaji wa mazingira likizingatiwa.

Amesema hayo tarehe 5 Machi, 2025 wakati akifungua rasmi Kongamano na Maonesho ya Petroli ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAPCE’25) ambalo litafanyika kwa muda wa Siku Tatu jijini Dar es Salaam.

“Katika kipindi ambacho maendeleo ya nishati endelevu yana mchango mkubwa katika mustakabali wa mazingira, uchumi na jamii zetu na katika kipindi ambacho Dunia inakabiliwa na changamoto za mabadiliko ya tabianchi bado tunahitaji  kutumia rasilimali zetu zilizopo, ikiwemo mafuta na gesi asilia lakini bila kuhatarisha mustakabali wa vizazi vijavyo ili kukidhi mahitaji ya kinishati.” Amesema Dkt. Mpango

Ameeleza kuwa, Afrika Mashariki imebarikiwa na rasilimali nyingi za nishati, ikiwemo mafuta na gesi asilia  ambapo  Tanzania imegundua gesi asilia, Uganda, Kenya na Sudan Kusini wamegundua mafuta, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wana gesi ya methane, huku Kenya na Tanzania zikiwa na rasilimali za nishati jotoardhi hivyo rasilimali hizo lazima  zitumike ili kupunguza pengo la nishati na kuharakisha maendeleo.

“Tunatambua kuwa ulimwengu unakabiliwa na changamoto za mabadiliko ya tabianchi yanayosababisha madhara makubwa kama vile vipindi visivyotabirika vya mvua, mafuriko, mitetemeko ya ardhi na kuongezeka kwa joto. Tanzania, kama mataifa mengine, imejitolea kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa  ili kupambana na mabadiliko ya tabianchi na kufanikisha azma ya kutozalisha hewa ya kaboni ifikapo mwaka 2050. Hata hivyo, tunapaswa kuweka uwiano kati ya ukuaji wa uchumi na uendelevu wa vyanzo vyetu  kwa kutatua changamoto za leo huku tukijiandaa kwa changamoto za kesho.” Amesema Dkt. Mpango

Dkt. Mpango ameeleza kuwa, suala la kuhama kutoka kwenye nishati chafu kwenda kwenye nishati safi haliepukiki  kwani ni mkakati muhimu wa kupunguza uchafuzi wa mazingira duniani hata hivyo uwekezaji katika nishati hiyo unahitaji mtaji mkubwa na utaalamu wa hali ya juu ambapo inakadiriwa kuwa Afrika inahitaji kati ya Dola Trilioni 1 hadi 2 kufanikisha malengo ya  ya kuelekea kwenye nishati safi ifikapo mwaka 2030 hivyo kuna umuhimu wa kutengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji na kuwa na ushirikiano kati ya sekta binafsi na sekta ya umma.

Katika Mkutano huo wa EAPCE’25, Dkt, Mpango amesema kuwa anaamini Viongozi na Watalaam watabadilishana mawazo na uzoefu kuhusu kufungua fursa za uwekezaji katika nishati endelevu bila kusahau  nafasi ya rasilimali za mafuta katika upatikanaji wa nishati ya kutosha huku akisisitiza  ushirikiano wa kikanda kuelekea kwenye matumizi ya nishati safi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa, kadri uchumi unavyokua kwa kasi mahitaji ya nishati hasa Gesi Asilia yanaongezeka hivyo Serikali inaendelea na jitihada za kuendeleza miradi ya mkondo wa juu wa petroli kwa lengo la kugundua na kuendeleza  vyanzo vipya  vya rasilimali za Mafuta na Gesi Asilia.

“ Nampongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu  Hassan kwa jitihada zake za kuendeleza mkondo wa juu wa petroli ambapo chini ya uongozi wake uzalishaji wa  gesi umeimarika katika vitalu vya Songosongo na MnaziBay ambavyo ni muhimu katika uchumi wa gesi.”Amesema Dkt.Biteko

Dkt.Biteko ametaja baadhi ya mafanikio katika Sekta ya Mafuta na Gesi Asilia nchini kuwa ni pamoja na  uendelezaji wa gesi asilia iliyogunduliwa  katika  eneo la  Ntorya kitalu  cha Ruvuma kwa kutoa leseni uendelezaji wake kwa kampuni ya ARA Petroleum na kuongezeka kwa ushiriki wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) katika kitalu cha Mnazibay kutoka asilimia 20 hadi 40.

Naye Waziri wa Nishati wa Uganda, Mhe. Ruth Nankwabira Seitamo, ameeleza kuhusu umuhimu wa fedha zinazopatikana katika  Sekta ya Mafuta  na Gesi Asilia  kunufaisha Sekta nyingine  huku akitolea mfano kuwa nchini Uganda wameanzisha Mfuko wa Petroli ambao unahudumia sekta nyingine ikiwemo barabara, elimu, afya lengo likiwa ni kuhakikisha kila mtu anafaidika na sekta husika.

Amesema sekta ya Mafuta na Gesi ni muhimu katika kuelekea kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia hali itakayowezesha pia kupunguza uharibifu na misitu ambapo amempongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa kuwa kinara wa Nishati Safi ya Kupikia Duniani.

Veronica Nduva, Katibu Mtendaji Jumuiya ya Afrika Mashariki amepongeza Tanzania kuendesha mkutano huo kwa mafanikio na kueleza kuwa unaendana na malengo ya Jumuiya ya EAC ya kuhakikisha kunakuwa na uendelezaji wa rasilimali za Mafuta na Gesi Asilia unaozingatia utunzaji wa mazingira.







Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...