Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Yericko Nyerere ampongeza Lissu na Kumchambua Mbowe


Na Yericko Nyerere

Uchaguzi umeisha, demokrasia imeshinda! Nafanya maachilio mema kutambua na kuthamini demokrasia ya kisiasa hasa katika ardhi ya ubwa. Nilisimama wima kumuunga mkono Mh Mbowe, tumeshindwa katika sanduku la kura kidemokrasia kabisa 

 Kwamsingi huohuo wa kidemokrasia ya siasa za vyama, Ninapongeza uongozi mpya chini ya Mwenyekiti Mh Tundu Lissu kwasababu umepatikana kwa njia ya kidemokrasia ya haki, uwazi na ukweli. Ndio demokrasia ina pande mbili, upande wa furaha na upande wa huzuni, muda wa huzuni umeisha sasa ni muda wa ushindi wa taasisi yetu.

Lakini, Niseme nini juu ya Mtu huyu Mh Freeman Mbowe? Hakika nitaandika kurasa milioni na bado sitamaliza kumuelezea na kumheshimisha. Wewe ni Kiongozi, Wewe ni Mwalimu, Wewe ni Baba, Wewe ni Kaka, Wewe ni Rafiki na wewe ni alama ya makuzi mema. Umejenga taasisi imara ya kidemokrasia, umeiishi demokrasia, na umeiishi kwa vitendo halisi kwa kuchagua kuwa ndio mlango wetu imara wa kuingia na kutokea!

Nimejiuliza sana, mimi moyo kama wako huo Mh Freeman Mbowe nitautoa wapi? Umedhalilishwa vya kutosha, Umetwezwa vya kutosha lakini ulitakaa kujibu udhalili huo na ulitukataza tusijibu kwa moto japo tuliumia, walau tukajibu kidogo kwa moshi, umesalitiwa na watu wako wa karibu hata tulipokwambia juu ya hili ulisema wazi acheni demokrasia iamue na kweli demkrasia imeamua! Ni nani mwenye moyo kama wako Mh Freeman Mbowe katika siasa za Afrika akaruhusu haya na akasimama na kuwashukuru makutano? Hakika sijamuona na sitamuona kwa karne zijazo.

Nitakukumbuka sana katika uongozi wako, ulitetea aseti za chama kwa nguvu kubwa, mfano hai ni pale mimi nilipovamiwa nyumbani kwangu Mbutu Kigamboni kwajaribio la kutekwa kwa mara ya kwanza wakafeli, ulisimama na mimi ukasaidia mapambano nisikamatwe kwa muda wa siku 60 za kuwindana usiku na mchana katika mikoa karibu yote Tanzania nilikokuwa nakimbilia, na baada ya hizo siku 60 nilitekwa pale Shoppers Plaza Mikocheni na kisha kufunguliwa kesi nane katika Mahakama ya Kisutu na Mahakama Kuu katika kipindi cha utawala awamu ya tano.

Ni wewe Mwenyekiti wa chama uliagiza mawakili 20 wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama sasa Mh Tundu Lissu na Mh Kibatala wakaongoza jopo hilo kwa miaka 7 mfululizo hadi nikashinda kesi 7 na moja kufungwa nikaenda kushindia kule Mahakama Mkuu. Ulikuwa moyo wa kipekee sana nilitambua na kuona unavyothamini aseti za chama, mimi mwanachama wa kawaida kupewa usaidizi mkubwa vile wa kisheria kwa miaka 7 mfululizo lilikuwa tukio kuu la kiuongozi. Niseme nini sasa? Naamini hujaondoka katika siasa bali unapumzika, tutakuhitaji mapema muda ukifika.

Uchaguzi umepita, Washindi wamepatikana, Chama kimeshinda, Tunalo jukumu moja tu kwasasa nalo ni kuwaunganisha Wanachadema, Binafsi nasimama kwenye ushauri wako Mh Freeman Mbowe kwa uongozi mpya wa Mwenyekiti Mh Tundu Lissu uliposema kwamba uongozi mpya uponye majereha, na kwamba uchaguzi huu umetuacha na majeraha makubwa hili hatupaswi kulipuuza kabisa. 

Jambo lingine muhimu ni kwamba Uongozi mpya usimamie kwa nguvu kubwa maazimio ya Chama kwamba Bila mabadiliko, hakuna uchaguzi mkuu wa taifa (no reform no election), na hapa niseme wazi ninahimiza hizi reforms kwanza kwa haraka kwakuwa muda tulionao kuelekea uchaguzi mkuu ni mdogo sana. Lakini lililo la muhimu ni reform hizi ziende sambamba na chama chetu kujiandaa katika uchaguzi wa mwezi October 2025. 

Itakuwa kosa la kimkakati na angamizo la chama chetu tukishindwa kupata reform hizo na tukashindwa kushiriki Uchaguzi huu kwani tutatimiza miaka 10 chama bila kushiriki uchaguzi na tutaruhusu chama kuondoka kwenye uongozi wa upinza na mbio za kushika dola lakini kubwa zaidi tutapoteza hata ruzuku tunayopata sasa ya 107M na mwisho uongozi mpya utakuwa umewaangusha wanachama walioahidiwa katika sera za Mh Lissu kwenye Uchaguzi kuwa katika uongozi wake ruzuku itaanza kushuka mikoani, wilayani majimboni, katani na katika mitaa/vijiji. 








Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...