Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Ushirikiano kati ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Wakurugenzi wa Halmashauri chachu ya usimamizi wa miradi ya Umwagiliaji nchini-Waziri Bashe


 ðŸ“ŒNa NIRC ;DODOMA

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, amehimiza ushirikiano kati ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, katika kusimamia miradi ya Umwagiliaji nchini.

Amesema Tume inatekeleza mradi wa Mifumo Himilivu ya Chakula nchini(TFSRP) lengo ni kuongeza uzalishaji wa chakula kutosheleza ndani ya nchi na kuilisha dunia,hivyo kuwapo na ushirikiano na Halmashauri. 

 Aidha amesisitiza kuwa katika utekelezaji wa mradi huo Tume imenunua zaidi ya Magari 17 na mitambo kwaajili ya uchimbaji wa Visima 56,000 vya Umwagiliaji na kuboresha miundombinu ya Umwagiliaji kwa lengo la kufikia adhina ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuongeza uzalishaji wa chakula. 

“Magari hayo yanatarajiwa  kuwasili kuanzia Machi mwaka huu, ambapo mawili kati ya hayo yatakuwa na uwezo kuchimba visima virefu zaidi”, amesema Bashe

Waziri Bashe amesema Tayari serikali imeshatangaza kandarasi ya kuchimba visima hivyo na tumepata wakandarasi kwa ajili ya kuanza kufanya kazi. 

“Na tumesema kila kisima kimoja kiwe na uwezo wa kuhudumia ekari 40 za kilimo,”alisema

 Amesema hayo katika hafla ya Makubaliano na Wakurugenzi wa Halmashauri 19 nchini, juu ya Usimamizi, Uendeshaji na Matunzo ya Skimu za Umwagiliaji kati ya Tume na Vyama vya Umaagiliaji kupitia Mradi huo.

Alihimiza Wakurugenzi hao kuhakikisha kuwa wanatembelea wakulima mashambani na kufanya Maafisa Kilimo wafanye kazi yao ya kuhudumia wakulima.

“Ili kuinua kilimo, lazima awepo Afisa Kilimo anayemhudumia Mkulima kuongeza uzalishaji," alisema Bashe. 

 Aliongeza kuwa:”Kupitia mradi huu tunaendelea kufanya usanifu katika mikoa mbalimbali na tunampango wa kununua pampu 2,000 ambazo zitasambazwa maeneo ambayo yanavyanzo vya maji ambayo haviitaji kujengwa ili kuhakikisha maji hayo yanawafikia wakulima. 

Waziri Bashe alisema ili kufanikisha hali hiyo  na adhima ya Rais Dkt Samia ya kuongeza uzalishaji Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ihakikishe inawashirikisha wakurugenzi kwani ndio wanaishi na miradi pamoja na wakulima 

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Tume ya Umwagiliaji Raymond Mndolwa alisema serikali ilipata fedha za mkopo nafuu dola milioni 300 kwa ajili ya kutekeleza mradi katika kipindi cha miaka mitano. 

Alisema mradi huo utaenda kurekebisha maneo ya kilimo ili kuhakikisha skimu za wakulima zinawekewa mifumo sahihi kwa ajili ya uzalishaji. 

“Katika kutekeleza mradi huu tuliona ni muhimu kushirikiana na wakurugenzi wa halmashauri kwasababu wao ndio wapo kwa wananchi,”alisema 

 Aliongeza kuwa ;”Mradi huu utaenda kuchimba visima nchi nzima kupitia magari ambayo yameagizwa  na yataanza kuwasili hivi karibuni lengo ni kuhakikisha sera ya serikali ya kuongeza tija katika Kilimo cha Umwagiliaji ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi inafikiwa,”alisema 

Akifunga Hafla hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Mweli alisema  kuwa halmashauri  nyingi nchini zinategemea kilimo kwa zaidi ya 80% ya mapato yake hivyo ushirikiano wa kisekta katika kusimamia miradi ya Umwagiliaji ni muhimu.

“ Wizara imeandaa mwongozo wa namna ya kuongeza mapato kupitia kilimo na halmashauri kutenga ekari 1,000, kwa akili ya miundombinu ya Umwagiliaji, lengo ni  kuzalisha ajira,kuongeza uzalishaji na kupunguza tatizo la njaa na kufikia maono ya serikali kuilisha dunia,”alisema.

 Naye Mratibu wa Mradi huo Mhandisi Naomi Mcharo alisema mradi huo utatekelezwa nchi nzima ambapo kupitia sekta ya umwagiliaji mradi huo utagharamiwa kwa dola za kimarekani milioni 70 na Tume imeanza na  Wakurugenzi wa halmashauri 19 kutoka katika mikoa sita ambayo inalima zaidi kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji ili kuwajengea uwezo.












Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...