Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Vita Kawawa wamepokea na kujadili Taarifa ya Wawakilishi wa Tanzania katika Umoja wa Mabunge ya Afrika, Carribeani Pasifiki na Jumuiya ya Ulaya (OACP/EU).
Aidha, Taarifa hiyo imewasilishwa na Mjumbe wa Umoja wa Mabunge ya Afrika, Carribeani Pasifiki na Jumuiya ya Ulaya (OACP/EU) kutoka Bunge la Tanzania, Mhe. Wanu Hafidh Ameir katika kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika tarehe 21 Januari, 2025 Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.