Kada kijana wa chama Cha mapinduzi CCM Jack Kangoye,ameshiriki kupata chakula pamoja na watu wenye ulemavu Desemba 28-2024 nyumbani kwake mjini Tarime mkoani Mara.
Kada huyo ambaye amekuwa akitoa misaada mbalimbali kwa makundi mbalimbali ya jamii ametumia nafasi hiyo kusikiliza maitaji mbalimbali ya jamii hiyo.
Amesema ameona changamoto nyingi zinazowakabili watu wenye ulemavu hivyo amebeba jukumu hilo na kutoa ahadi kuwa wakati wa sikukuu ya Pasaka mwaka 2025 atakuwa ametatua baadhi ya changamoto hizo.