Na Mwandishi Wetu, Mwanza
Wakati Taifa likipanga kusherekea uhuru wa Tanganyika Desemba 9, Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) inaishukuru serikali ya awamu ya sita chini wa Uongozi mahiri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa kwenye taasisi yetu.
Akiongea jijini Mwanza jana, Mkurugenzi Mkuu wa TASHICO Eric Hamissi amesema kuwa uwekezaji huo unaohusisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo ndio ambao unaoijengea Kampuni hiyo uwezo wa kujiendesha kibiashara na kutanua wigo wa uendeshaji wake.
“Bila uwekezaji huu mkubwa, huu mchakato wa kubadilisha jina la Kampuni usingukwa na maana yoyote na badala yake ingekuwa ni kama kubadilisha chupa tu wakati mvinyo ni ile ile,” alisema.
Aliongeza: ““Ningependa kutumia fursa hii kuwashukuru wadau wote ambao wamekuwa wameshirikiana nasi kwa njia mbalimbali katika safari yetu hadi sasa.”
Hamissi alitabanaisha kuwa mara tu baada ya Uhuru, Shirika lilikuwa chini ya Uangalizi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki lakini Serikali iliendelea kutoa huduma ya usafiri kwa njia ya maji katika maziwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa kwa kutumia meli tatu (3) za MV. Victoria (1960) na M.V. Clarias (1961) katika Ziwa Victoria; na M.V. Liemba (1913) katika Ziwa Tanganyika.
“Hata hivyo, Serikali ilinunua meli mpya saba (7): Ziwa Victoria: M.V. Butiama, (1980), MT. Ukerewe (1983), M.V. Serengeti (1988), Ziwa Tanganyika: M.T. Sangara (1981), M.V. Mwongozo (1982) wakati kwenye Ziwa Nyasa ni M.V. Songea, M.V. Iringa,” alisema.
Alisema kuwa MSCL ilianzishwa chini ya Sheria ya Makampuni sura 212, tarehe 08 Disemba 1997 kutoka Shirika la Reli (TRC). Lakini rasmi MSCL ilianza kazi tarehe 01, Agosti, 1999 ikiwa na meli 14 na boti moja,
“Hadi mwaka 2015, Kampuni ilikuwa inamiliki meli 14 ambazo kati ya hizo Meli 9 zipo katika Ziwa Victoria, Meli 3 na Boti 1 katika Ziwa Tanganyika na Meli 2 katika Ziwa Nyasa,” alisema.
Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa kwakuwa meli nyingi zilikuwepo kwa muda mrefu, hivyo zilichakaa na kupelekea nyingine kusimamishwa kutoa huduma kutokana ili kulinda usalama wa chombo na usalama wa maisha ya watu na mali zao ambapo mwaka 2017, Kampuni ilikuwa na meli tano tu zilizokuwa zinatoa huduma; Ziwa Victoria kulikuwa na MV.Umoja, MV Clarias wakati Ziwa Tanganyika kulikuwa na MV Liemba, MT Sangara na kwenye Ziwa Nyasa kulibaki na MV Songea.
Hamissi alisema kuwa kutokana na kudorora kwa Kampuni katika utoaji wa huduma pamoja na umuhimu wake kwa wananchi wanaoishi katika maeneo ya maziwa makuu na uchumi wa nchi kwa ujumla, Serikali iliamua kufufua huduma za usafiri kwa njia ya maji kwa abiria na mizigo katika maziwa hayo.
“Mwaka 2018, Serikali ilianza kutenga fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa miradi mikubwa minne katika Ziwa Victoria na Mwaka 2022, Serikali iliielekeza Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kukabidhi meli tatu (3) za MV. Mbeya II, MV. Njombe na MV. Ruvuma kwa MSCL ambazo hadi sasa meli hizo zinaendelea kutoa huduma katika Ziwa Nyasa,” alisema.
AWAMU YA KWANZA YA MIRADI (2018 – 2023)
Alisema kuwa awamu hiyo ya kwanza ilihusisha miradi minne mojawapo ikiwa ni ujenzi wa Meli mpya ya MV Mwanza “Hapa Kazi Tu”, yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo katika Ziwa Victoria, wakati tulifanya ujenzi wa Chelezo - ambayo inatumika kama kitanda cha meli kabla haijashushwa katika maji wakati ikiundwa. na meli ya MV. Mwanza iliundwa kwenye Chelezo hii,
“Kwenye awamu hii tulifanya ukarabati wa Meli za MV Victoria – Iliitwa New Victoria Hapa Kazi Tu ambayo inasafiri kutoka Mwanza Kwenda Bukoba kupitia Kemondo na ilianza kutoa huduma mwaka 2020 pamoja na kulifanyika ukarabati wa MV Butiama – iliitwa New Butiama Hapa Kazi Tu inasafiri kila siku kutoka Mwanza kwenda Nansio, kisiwa cha Ukerewe,” alisema.
AWAMU YA PILI YA MIRADI (2023 – 2028)
“Awamu hii inahusika miradi nane (8) ampapo Ziwa Victoria miradi Minne (4) ambayo ni ujenzi wa meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 3,000 katika Ziwa Victoria, ukarabati mkubwa wa meli MV. Umoja inayobeba mabehewa katika Ziwa Victoria. Mkataba wa mradi huu ulisainiwa tarehe 15 Juni, 2021 na kukamilika Septemba, 2023. Kwa sasa meli inaendelea kusafirishamizigo tangu Oktoba 2023,” alisema.
Aliongezea kuwa katika awamu hii walifanya vilevile ukarabati wa meli ya uokozi na kuvuta matishari ya MT. Ukerewe katika Ziwa Victoria. Mkandarasi anaendelea na ukarabati pamoja na ukarabati mkubwa wa meli ya kubeba shehena ya mizigo (mafuta) ya MT. Nyangumi iliyopo Ziwa Victoria Mkataba wake ulisainiwa tarehe 17 Novemba 2023.
Alisema kuwa kwenye Ziwa Tanganyika miradi minne (4) ilitekelezwa ambayo ni ukarabati wa meli ya kubeba shehena ya mafuta ya MT. Sangara katika Ziwa Tanganyika na ujenzi wa meli mpya ya kubeba shehena ya mizigo kiasi cha tani 3,500 katika Ziwa Tanganyika.
“Tuliweza vile vile kutekeleza ujenzi wa Kiwanda cha Kujengea Meli katika Ziwa Tanganyika pamoja na Ukarabati mkubwa wa meli ya MV. Liemba katika Ziwa Tanganyika. Mkandarasi ameshakabidhiwa mradi anaendelea nao vizuri,” alisema.
Alisema kuwa miradi hii ya awamu ya pili kwa ujumla inafikia Dola za Kimarekani 326,027,480.02 ambayo ni sawa na Shilingi 893,315,295,254.8 kwa kubadili dola kwa $1 = 2,740.



Comments
Post a Comment