Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kampuni ya Meli Tanzania yaishukuru awamu ya sita utekelezaji miradi ya ujenzi wa meli


Na Mwandishi Wetu, Mwanza

Wakati Taifa likipanga kusherekea uhuru wa Tanganyika Desemba 9, Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) inaishukuru serikali ya awamu ya sita chini wa Uongozi mahiri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa kwenye taasisi yetu.

Akiongea jijini Mwanza jana, Mkurugenzi Mkuu wa TASHICO Eric Hamissi amesema kuwa uwekezaji huo unaohusisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo ndio ambao unaoijengea Kampuni hiyo uwezo wa kujiendesha kibiashara na kutanua wigo wa uendeshaji wake.

“Bila uwekezaji huu mkubwa, huu mchakato wa kubadilisha jina la Kampuni usingukwa na maana yoyote na badala yake ingekuwa ni kama kubadilisha chupa tu wakati mvinyo ni ile ile,” alisema.

Aliongeza: ““Ningependa kutumia fursa hii kuwashukuru wadau wote ambao wamekuwa wameshirikiana nasi kwa njia mbalimbali katika safari yetu hadi sasa.”

Hamissi alitabanaisha kuwa mara tu baada ya Uhuru, Shirika lilikuwa chini ya Uangalizi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki lakini Serikali iliendelea kutoa huduma ya usafiri kwa njia ya maji katika maziwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa kwa kutumia meli tatu (3) za MV. Victoria (1960) na M.V. Clarias (1961) katika Ziwa Victoria; na M.V. Liemba (1913) katika Ziwa Tanganyika.

“Hata hivyo, Serikali ilinunua meli mpya saba (7): Ziwa Victoria: M.V. Butiama, (1980), MT. Ukerewe (1983), M.V. Serengeti (1988), Ziwa Tanganyika: M.T. Sangara (1981), M.V. Mwongozo (1982) wakati kwenye Ziwa Nyasa ni M.V. Songea, M.V. Iringa,” alisema.  

Alisema kuwa MSCL ilianzishwa chini ya Sheria ya Makampuni sura 212, tarehe 08 Disemba 1997 kutoka Shirika la Reli (TRC). Lakini rasmi MSCL ilianza kazi tarehe 01, Agosti, 1999 ikiwa na meli 14 na boti moja,

“Hadi mwaka 2015, Kampuni ilikuwa inamiliki meli 14 ambazo kati ya hizo Meli 9 zipo katika Ziwa Victoria, Meli 3 na Boti 1 katika Ziwa Tanganyika na Meli 2 katika Ziwa Nyasa,” alisema.

Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa kwakuwa meli nyingi zilikuwepo kwa muda mrefu, hivyo zilichakaa na kupelekea nyingine kusimamishwa kutoa huduma kutokana ili kulinda usalama wa chombo na usalama wa maisha ya watu na mali zao ambapo mwaka 2017, Kampuni ilikuwa na meli tano tu zilizokuwa zinatoa huduma; Ziwa Victoria kulikuwa na MV.Umoja, MV Clarias wakati Ziwa Tanganyika kulikuwa na MV Liemba, MT Sangara na kwenye Ziwa Nyasa kulibaki na MV Songea.  

Hamissi alisema kuwa kutokana na kudorora kwa Kampuni katika utoaji wa huduma pamoja na umuhimu wake kwa wananchi wanaoishi katika maeneo ya maziwa makuu na uchumi wa nchi kwa ujumla, Serikali iliamua kufufua huduma za usafiri kwa njia ya maji kwa abiria na mizigo katika maziwa hayo.

“Mwaka 2018, Serikali ilianza kutenga fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa miradi mikubwa minne katika Ziwa Victoria na Mwaka 2022, Serikali iliielekeza Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kukabidhi meli tatu (3) za MV. Mbeya II, MV. Njombe na MV. Ruvuma kwa MSCL ambazo hadi sasa meli hizo zinaendelea kutoa huduma katika Ziwa Nyasa,” alisema.


AWAMU YA KWANZA YA MIRADI (2018 – 2023)

Alisema kuwa awamu hiyo ya kwanza ilihusisha miradi minne mojawapo ikiwa ni ujenzi wa Meli mpya ya MV Mwanza “Hapa Kazi Tu”, yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo katika Ziwa Victoria, wakati tulifanya ujenzi wa Chelezo - ambayo inatumika kama kitanda cha meli kabla haijashushwa katika maji wakati ikiundwa. na meli ya MV. Mwanza iliundwa kwenye Chelezo hii,

“Kwenye awamu hii tulifanya ukarabati wa Meli za MV Victoria – Iliitwa New Victoria Hapa Kazi Tu ambayo inasafiri kutoka Mwanza Kwenda Bukoba kupitia Kemondo na ilianza kutoa huduma mwaka 2020 pamoja na kulifanyika ukarabati wa MV Butiama – iliitwa New Butiama Hapa Kazi Tu inasafiri kila siku kutoka Mwanza kwenda Nansio, kisiwa cha Ukerewe,” alisema.


AWAMU YA PILI YA MIRADI (2023 – 2028)

“Awamu hii inahusika miradi nane (8) ampapo Ziwa Victoria miradi Minne (4) ambayo ni ujenzi wa meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 3,000 katika Ziwa Victoria, ukarabati mkubwa wa meli MV. Umoja inayobeba mabehewa katika Ziwa Victoria. Mkataba wa mradi huu ulisainiwa tarehe 15 Juni, 2021 na kukamilika Septemba, 2023. Kwa sasa meli inaendelea kusafirishamizigo tangu Oktoba 2023,” alisema.

Aliongezea kuwa katika awamu hii walifanya vilevile ukarabati wa meli ya uokozi na kuvuta matishari ya MT. Ukerewe katika Ziwa Victoria. Mkandarasi anaendelea na ukarabati pamoja na ukarabati mkubwa wa meli ya kubeba shehena ya mizigo (mafuta) ya MT. Nyangumi iliyopo Ziwa Victoria Mkataba wake ulisainiwa tarehe 17 Novemba 2023. 

Alisema kuwa kwenye Ziwa Tanganyika miradi minne (4) ilitekelezwa ambayo ni ukarabati wa meli ya kubeba shehena ya mafuta ya MT. Sangara katika Ziwa Tanganyika na ujenzi wa meli mpya ya kubeba shehena ya mizigo kiasi cha tani 3,500 katika Ziwa Tanganyika.

“Tuliweza vile vile kutekeleza ujenzi wa Kiwanda cha Kujengea Meli katika Ziwa Tanganyika pamoja na Ukarabati mkubwa wa meli ya MV. Liemba katika Ziwa Tanganyika. Mkandarasi ameshakabidhiwa mradi anaendelea nao vizuri,” alisema.

Alisema kuwa miradi hii ya awamu ya pili kwa ujumla inafikia Dola za Kimarekani 326,027,480.02 ambayo ni sawa na Shilingi 893,315,295,254.8 kwa kubadili dola kwa $1 = 2,740.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...