Na Philipo Hassan/ Dar es salaam
Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amewakabidhi TANAPA Malori matano na mitambo mitano yenye thamani ya Dola milioni 2.4 sawa na shilingi Bilioni 6.4 za Kitanzania, tukio hilo limefanyika leo Disemba 2, 2024 katika Ukumbi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (Mpingo House) jijini Dar es salaam.
Vifaa hivyo viliyonunuliwa kupitia mradi wa Dharura kwa Uhifadhi na Utalii Tanzania (Emergency Recovery Support for Biodiversity in Tanzania) kupitia benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KFW).
Akizungumza katika makabidhiano haya Balozi Dkt. Chana alieleza kuwa vifaa hivyo vitaboresha shughuli za Uhifadhi pamoja na miundombinu katika Hifadhi za Taifa Serengeti na Nyerere kwa malengo ya kupunguza athari zilizosababishwa na janga la UVIKO-19 kwenye Utalii na Uhifadhi.
Dkt. Chana alisema “Nawaagiza Bodi na Wakuu wa Mashirika ya TAN











Comments
Post a Comment