Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete amekutana na kuzungumza na Balozi wa Japan nchini Tanzania.
Balozi huyo ambaye pia ni Mwakilishi wa Japan katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Yusushi Misawa pamoja na ujumbe wake amepomtembelea waziri Kikwete katika Ofisi ya NSSF, Jijini Dar es Salaam.
Katika kikao hicho, wamejadili mambo mbalimbali ikiwemo kuwezesha vijana wa Kitanzania nafasi za kujifunza kazi na kuimarisha mafunzo pamoja na kuongeza ujuzi.



