Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kanda ya Kaskazini, na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, amesema ni matamanio na mpango wa CHADEMA kushiriki kikamilifu uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 hivyo wanashukuru na kupongeza juhudi za Serikali kurejeshwa wagombea wa CHADEMA katika mitaa na vijiji mbalimbali nchini.
Lema ameyasema hayo leo, Novemba 13, 2024, katika mkutano wa CHADEMA Arusha. Lema ameendelea kusema kwamba ni kweli CHADEMA hawajaweka wagombea sehemu nyingi nchini, hivyo wagombea wachache kupata nafasi ya wagombea wao kurudishwa ni hatua ya kupongezwa na ishara ya utawala bora na Samia ameweza kutimiza ahadi yake ya kuimarisha demokrasia nchini.
CHADEMA wametoa pongezi hizo kufuatia maagizo ya Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mchengerwa kutoa muda zaidi wa kushughulikia malalamiko na kurudishwa kwa wagombea walioenguliwa kwa makosa madogo na waliokosa udhamini wa vyama vyao.
