Na Dawati la Habari Polisi Mwanza
Madereva wa boda boda watakiwa kuvaa kofia ngumu na kufata Sheria za usalama barabarani pindi wanapotumia pikipiki ili kuepukana na ajali ambazo zinaweza wapelekea kupoteza nguvu kazi ya taifa.
Hayo yamebainishwa Oktoba 24.2024 na Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Mwanza Mrakibu wa Polisi (SP) Sunday Ibrahim wakati akitoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha boda boda wa vituo vya kata za Nyegezi, Luchelele na Mkolani wilayani Nyamagana mkoani Mwanza.
Akizungumza na madereva wa boda boda hao kutoka kanda ya Mwanza kusini,Sunday amesema elimu hiyo imelenga kuwapa uelewa makundi mengine ya watumiaji wa barabara hususan bodaboda ili kuzuia ajali zinazoweza kuepukika.
Aidha, SP Sunday amesema, atahakikisha operesheni inayoendelea haimuacha mtu ambapo watakaobaini kutovaa Korea ngumu kinyume cha sheria watachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani.
" wengi mnasema abiria hataki kuvaa kofia ngumu afisa msafirishaji mzuri wa kisasa wa mwanza atampa elimu kabla ya kuondoka juu ya umuhimu wa kofia ngumu" amesema SP Sanduy.
Kwa upande wake mwenyekiti wa wa waendesha pikipiki wilaya ya Nyamagana Mohamed idi amewataka waendesha bodaboda hao kuacha kujichukulia sheria mikononi kwani yeyote anayekosea kuna sheria inatakiwa kumuhukumu hivyo, ni wajibu wa kila mmoja kumlinda mwezake ili kazi hiyo iendelee kuoneka ni njema na ni safi Kwa jamii.
"Kujichukulia sheria mikononi unaweza kupoteza haki yako hivyo tuache mamlaka zifanye kazi zake" amesema Mohamed Idd.
Naye koplo wa Polisi Rehema wa kikosi Cha usalama barabarani mkoa wa Mwanza amewataka madereva wa bodaboda kuzingatia Sheria za usalama barabarani kwa kuacha kupakia abiria zaidi ya mmoja katika bodaboda.
" sheria ya usalama barabarani inatukumbusha mara zote hasa unapoingia barabarani kwani alietengeneza chombo hiki amekipa uwezo wa kubeba abiria mmoja kwenye hiyo pikipiki maana yake ni nini anajua pikipiki hiyo itakapopata shida utapata namna ya kumudu hicho chombo" amesema Cpl Rehema.




