Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Fahamu Mambo Muhimu ya Kuzingatia Kabla ya Kununua Vifaa Vya Umeme wa Solar


Na Emmanuel Chibasa

Umeme wa solar ni aina ya umeme unaozalishwa kwa kutumia mionzi ya jua. Paneli za solar, ambazo hujulikana pia kama photovoltaic (PV) panels, zinakusanya mionzi ya jua na kuibadilisha kuwa umeme wa kutumia nyumbani, ofisini, au kwenye shughuli nyingine za kibiashara.

Mfumo wa umeme wa solar unajumuisha paneli za solar, battery za kuhifadhi umeme, na inverter ambazo hubadilisha umeme wa DC (Direct Current) kutoka kwenye paneli kuwa umeme wa AC (Alternating Current) unaotumika katika vifaa vya umeme vya kawaida.

Umeme wa solar unafaa kwa shughuli nyingi, hasa katika maeneo ambapo umeme wa gridi ya taifa haupo au unapatikana kwa ukawaida. Mfumo huu ni wa kuaminika na wa gharama nafuu, kwani unategemea chanzo cha nishati kisicho na mipaka—jua. Hivyo, umeme wa solar unafaa kwa matumizi mbalimbali kama vile mwanga wa nyumba, matumizi ya vifaa vya kielektroniki, na hata kwa biashara ndogo na mashamba.

Licha ya umeme wa solar kuwa nafuu na uhakika Kwa Matumizi Mbalimbali hasa Kwa Wananchi wa maeneo ya vijijini, Changamoto kubwa ni uelewa juu ya matumizi sahihi ya vifaa Toka Kwa wataalam Hali inayopelekea nishati hiyo Kutumiwa na watu Wachache 

Khamis Haule ni mkazi wa wilaya ya Musoma mkoani Mara mwenye familia ya watoto wanne na mfanya Biashara nataka anasema amekuwa akijitahidi kutafuta suluhisho tatizo la umeme nyumbani kwake na alijua kwamba umeme wa solar unaweza kuwa suluhisho bora.

Amesema ameshindwa kufanya mamuzi ya kunununua solar kutokana na kukosa  uelewa jinsi ya kuchagua vifaa sahihi na vinavyofaa katika shughuli mbalimbali tofauti na kupata mwanga kwenye nyumba yake kama anavyoona kwa watu wengine kutokana na kusikia baadhi ya watu wakilalamika vifaa kutokidhi Mahitaji kama walivyofikiri awali

Mbali na Khamis nimezungumza pia pia na Grace Matiku ambaye ni mama wa familia ili kupata kufahamu uelewa wake kuhusu matumizi ya umeme wa Solar  amesema kuwa binafsi anafahamu kuwa umeme wa solar unatumika majumbani kwa ajili ya kupata mwanga Kwa watu ambao hawana umeme lakini pia Kwa Wenye umeme wa tanesco kupunguza matumizi.

“ Mimi kwangu sijaweka solar lakini naona siku hizi watu wengi wananunua solar ili kusaidia mwanga katika taa za nje kwa ajili ya ulinzi lakini pia zinasaidia kupata mwanga na zile taa za barabarani, ila sijawahi kwenda dukani kujua zaidi juu ya matumizi zaidi ya kuona vifaa vyake vimepangwa na kuuzwa kwenye baadhi ya maduka” Amesema Grace.

Khamis na Grace ni miongoni mwa wananchi ambao pia wengi wao wamenunua vifaa vya solar bila kuwa na uelewa wa kutosha juu ya mambo gani wanapaswa kuzingatia kabla ya kufanya manunuzi ya vifaa au kutafuta wataalam ili waweze kuelimishwa zaidi.

Katika kusaidia kutatua changamoto hiyo nimezungumza Joachim Misana ambaye ni mtaalam wa solar na mwenye uzoefu  ili kufahamu ni mambo gani muhimu ya kuzingatia kabla ya kununua vifaa vya solar ikiwa ni pamoja na hatua muhimu za kuchagua paneli za solar na battery zinazofaa.

Amesema kabla ya kununua vifaa vya solar kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, biashara au kilimo kwanza mtu anahitaji kuelewa matumizi yake ya umeme kwa kuorodhesha vifaa vyote wanavyotumia na kiasi cha umeme vinavyotumia pamoja na kuonyesha jinsi ya kuhesabu matumizi yote kwa kutumia vigezo vya Watt na masaa ya matumizi huku akieleza hatua za kufuata katika matumizi yake

Hatua ya Kwanza  ameekezea jinsi ya kuchagua paneli za solar zinazofaa kwa kuzingatia ukubwa wa paneli ambapo amesema kuwa paneli kubwa zinakusanya mionzi ya jua kwa kiasi kikubwa na kwa muda mfupi zaidi na ukubwa na idadi ya paneli zinazohitajika zitategemea idadi na aina ya vifaa vya umeme vinavyotumika, muda wa matumizi, na kiwango cha mwangaza wa jua katika eneo.

Hatua ya Pili: Rashid alisisitiza mambo matatu muhimu ya kuzingatia wakati wa kuchagua paneli za solar kwa kuangalia matumizi ya Umeme kwa kuangalia  ni vifaa gani vya umeme vinavyotumika na kiasi gani cha umeme vinavyotumia, Kufahamu ukubwa na uwezo wa battery unayohitaji pamoja na kuangalia uwezo wa Solar Panel kwa kuangalia ni za ukubwa gani (au idadi ya paneli) zitakazozalisha umeme wa kutosha kuchaji battery kwa haraka.

Hatua ya Tatu amefafanua kuwa ili mtu aweze kumudu vyema mtumumizi ya solar anapaswa kufahamu pia jinsi ya kupima kiasi cha umeme kinachotumika kwa kila kifaa kwa kutumia kipimo cha Watt (W). Kwa mfano, kwa taa yenye nguvu ya 24W inayotumika kwa masaa manne (4), alieleza jinsi ya kuhesabu umeme inayotumiwa kwa jumla, ambayo ilikuwa 96Wh kwa masaa manne.

Hatua ya nne ni kuwa na uelewa wa jinsi ya kupima uwezo wa battery kwa kutumia kipimo cha Amp Hours (Ah) na Voltage (V).Huku akitolea  mfano wa battery yenye uwezo wa 17Ah na voltage ya 12V, na jinsi ya kuhesabu umeme itakazotoa kwa kutumia formula ya Watt: 17Ah x 12V = 204Wh na kueleza  kwamba battery hii inaweza kuwasha taa yenye nguvu ya 24W kwa masaa 8.5.

Na hatua ya Tano alieleza na kusisitiza umuhimu wa kujua kiasi gani cha umeme solar panel yako inaweza kuzalisha kwa muda gani na kusema  kwamba  mtumiaji anapaswa kufahamu uwezo wa solar panel kupima kwa kutumia Watts (W) na masaa ya mionzi ya jua. Kwa mfano, paneli ya 10W inayopokea mionzi ya jua kwa masaa nane (8) itazalisha 68Wh na pia mtumiaj anahitaji kuhesabu ni paneli ngapi zitahitajika ili kufikia mahitaji yao ya umeme.

Joachim anatoa wito kwa watumiaji wanaotaka kununua vifaa vya solar kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, biashara na kilimo, kwanza kuwashirikisha wataalam ili waweze kujengewa uelewa wa matumizi lakini pia kupata ushauri wa kuchagua solar panel pamoja na betri zitakazoendana na mahitaji husika.

Pia ameongeza kuwa kuwaona wataalam kunasaidia kufahamishwa namna ya matumizi na utunzaji wake kuliko kwenda dukani kununua vifaa kabla ya kupata ushauri kutoka kwa wataalamili kuhakikisha kwamba wanapata mfumo wa umeme wa solar utakaokidhi mahitaji yao ya umeme kwa ufanisi.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...