Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MBUNGE MWAKIOJA AINGILIA TATIZO LA VIJANA KUKOSA NIDA


 Na Mwandishi Wetu, Mkinga

MBUNGE wa Jimbo la Mkinga, mkoani Tanga, Twaha Mwakioja ameingilia kati tatizo la vijana wengi wanaoishi maeneo ya mpakani wilayani humo kukabiliwa na changamoto ya kukosa mikopo kutokana na kucheleweshewa namba za NIDA.

Hali hiyo ilibainishwa na Mjumbe wa Bodaboda, Ali Selemani Rasi, wakati wa kikao maalum kati ya Mbunge wa Jimbo la Mkinga, Mhe. Twaha Mwakioja, na waendesha pikipiki wa kijiwe cha Duga Maforoni kilichofanyika leo Juni 7, 2026.

Rasi alisema vijana wa Duga Maforoni wanakosa fursa za kupata mikopo inayotolewa na Serikali ya asilimia 10 kutoka kwenye mapato ya ndani ya halmashauri kwa kuwa hawana vitambulisho hivyo vya taifa.

"Mheshimiwa Mbunge, sisi vijana tunaoishi mipakani tuna tatizo kubwa la kukosa namba za NIDA ambazo zinatufanya tushindwe kupata mikopo ya vijana," alisema Rasi na kumuomba Mbunge awasaidie ili waweze kupata mikopo hiyo kama wenzao wengine nchini.

Akijibu malalamiko hayo, Mbunge Mwakioja alitoa agizo la kimkakati akisema kuwa kuanzia kesho taratibu zote zitakwenda kwa kasi ili kuwasaidia vijana hao wapate haki yao ya msingi. Alisema haiwezekani Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa mikopo kwa ajili ya kuwawezesha vijana, wanawake na makundi maalum huku vijana katika jimbo lake wakikwama.


"Jambo hili tunataka liende haraka sana. Ndani ya wiki mbili zijazo, nataka kila kijana awe amepata namba yake ya NIDA. Haiwezekani vijana wetu wakwame na wakose fursa za mikopo ya kiuchumi mtaani kwa sababu tu ya urasimu wa kukosa vitambulisho," alisisitiza Mbunge Mwakioja.

Malalamiko ya kukosa namba za NIDA kwa wananchi wa Wilaya ya Mkinga, hasa kata za Moa, Duga Sigaya, Mwakijembe na Duga Maforoni zilizopo mpakani mwa Kenya na Tanzania, yamekuwa mengi na utatuzi wake umekuwa ukienda taratibu kutokana na usalama wa mwingiliano mkubwa wa jamii zinazoishi katika maeneo hayo ya mipakani.

Katika kikao hicho kilichohudhuriwa pia na Diwani wa Kata ya Duga, Mhe. Jumaa Abdallah Rioba, Mbunge Mwakioja alikabidhi mabati ya jumla ya Sh. 600,000 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa banda la abiria, mradi uliopata kibali cha dharura kutoka TANROADS.


Mhe. Mwakioja alikubali ombi la risala ya vijana iliyosomwa na Haji Selemani, na kuahidi kuwanunulia TV ya kisasa, king'amuzi, pamoja na jokofu (friji) la kuuzia vinywaji ili kuwaongezea kipato, huku akiahidi kushirikiana na Diwani kutoa mafunzo ya usalama barabarani na leseni kama walivyoomba.

Hata hivyo, Mbunge aliweka sharti akitaka kituo hicho cha bodaboda Duga Maforoni kutumika kama kituo cha Amani na hifadhi ya mazingira, ambapo madereva hao watakuwa mabalozi wa kudhibiti utakatishaji na upitishaji wa dawa za kulevya kama mirungi, bangi na kokeini mpakani.

Suala lingine lililoibuka kwenye kikao hicho liliwasilishwa na kijana Mwanakombo Twaha Mbwana, aliyehoji hatma ya vijana 32 waliopata mafunzo ya Uaskari Misitu mkoani Mwanza lakini hadi sasa wapo mtaani hawajui hatma yao baada ya mafunzo hayo.

Mbunge Mwakioja aliahidi kuwasiliana moja kwa moja na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, ili kuona vijana hao wanawekwa kwenye daraja gani la ajira, huku akiwataka wananchi kuendelea kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Naye mwendesha bodaboda, Suna Mwasega, alimshukuru Mbunge kwa usimamizi wage thabiti na kuwa karibu na wananchi tofauti na mtangulizi wake, huku kikao hicho kikifungwa kwa hamasa kubwa na Duga Maforoni ikitakiwa kujiandaa na mkesha wa Mwenge wa Uhuru 2026 mara baada ya kumaliza kukimbizwa wilayani humo.

Katika hatua nyingine mbunge Mwakioja alisema serikali imetoa kiasi cha Shilingi milioni 980 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya na shule mpya ya sekondari katika mji wa Horohoro.

Mhe. Mwakioja alifafanua mbele ya umati wa wananchi kuwa, kati ya fedha hizo, jumla ya Sh. milioni 680 zitaenda moja kwa moja kwenye ujenzi wa kituo cha afya cha kisasa, huku Sh. milioni 300 zikitumika kujenga Shule ya Sekondari ya Horohoro Kijijini.

Hatua hiyo inatajwa na wadau wa maendeleo wilayani Mkinga kuwa ni ukombozi mkubwa kwa akina mama na watoto waliokuwa wakisafiri umbali mrefu kufuata huduma za kitabibu na elimu nchi jirani ya Kenya.

Kuhusu changamoto sugu ya upatikanaji wa maji safi na salama wilayani humo, Mbunge Mwakioja alishusha data za kiufundi kuhusu mradi mkubwa wa maji wa kimkakati kutoka Tanga hadi Horohoro wenye thamani ya Sh. bilioni 35.

Alieleza kuwa mradi huo kwa sasa umefikia hatua nzuri ambapo mafundi wapo site wakiendelea na kazi ya utandikaji wa mabomba makuu ili kusogeza huduma hiyo kwenye makazi ya watu.

"Ndugu zangu, hakika suala la maji tayari tumelipatia ufumbuzi wa dhati kitalamu. Hizi bilioni 35 zitafikisha maji ya uhakika hadi huku Horohoro mpakani, na kero hii ya muda mrefu inakwenda kubaki kuwa historia tu mtaani kwetu," alisema Mbunge Mwakioja huku akishangiliwa.

Uchunguzi wa MaratoTV unaonyesha kuwa ujio wa miundombinu hiyo mipya ya afya, elimu, na maji mpakani utachochea kwa kasi ukuaji wa uchumi wa wilaya ya Mkinga na kuongeza usalama wa jamii kutokana na upatikanaji wa huduma za kijamii za kiwango cha juu.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...