Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

TANZANIA YA KIJANI: MAAMUZI YA LEO, URITHI WA KESHO


 Na Gideon Gregory - Dodoma 

Katika kipindi ambacho dunia inaendelea kukabiliwa na ongezeko la joto, uchafuzi wa mazingira mjadala kuhusu mazingira haupo tena kwenye uhifadhi pekee bali umehamia kwenye namna ambavyo mataifa yanajenga maendeleo yanayodumu. 

Takwimu za Umoja wa Mataifa za miaka ya hivi karibuni zinaonyesha kuwa shinikizo la mazingira linaongezeka kila mwaka na kufanya hatua za sasa kuwa msingi wa maisha ya vizazi vijavyo.

Ni katika muktadha huo ambapo maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka huu kwa Tanzania yamekuja na ujumbe wa “Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania” kauli inayobeba zaidi ya kampeni ya kupanda miti ili kurejesha uoto wa asili.

Akizungumza kwenye maadhimisho hayo yaliyofanyila Jijini Dodoma Mei 5,2026 Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi anabainisha kuwa mazingira yanamchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa taifa na ustawi wa wananchi. 

"Pale ambapo mazingira yametunzwa vyema basi uchumi na ustawi wa maisha ya watu pia huimarika, aidha mazingira ni muhimu katika kuhimili ongezeko la watu duniani madhalani kwa Tanzania inakadiliwa kuwa na watu zaidi ya milioni 67 ambapo ifikapo mwaka 2050 idadi inakadiliwa kufikia zaidi ya watu milioni 118,"anasema. 

Dkt. Nchimbi analitaja ongezeko hilo kubwa la watu kuhitaji uwepo wa rasilimali nyingi muhimu zinazotegemea mazingira kama vile maji, chakula, ardhi yenye rutuba inayofaa kwa kilimo, makazi, nishati na mfumo wa huduma za jamii, hivyo kwa kutambua umuhimu huo dira ya mwaka 2050 imejumuisha suala la mazingira na ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kama sehemu ya maendeleo ya kuelekea uchumi wa kipato cha kati ngazi ya juu.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, zaidi ya tani milioni 400 za plastiki huzalishwa duniani kila mwaka, huku karibu nusu yake ikitengenezwa kwa matumizi ya muda mfupi pekee na takribani asilimia 10 tu ndiyo hurejelewa (recycled). 

Kati hizo tani milioni 19 hadi 23 za taka za plastiki huingia kwenye mifumo ya maji kila mwaka, na bila hatua za haraka kuchukuliwa kiwango hicho kinaweza kuongezeka kwa karibu asilimia 50 ifikapo mwaka 2040.

Hatua ambayo Dkt. Nchimbi anayataja maadhimisho hayo kama jukwaa muhimu la kitaifa na kimataifa la kukumbushia wajibu wa kuunganisha nguvu za pamoja katika jitihada za kuhifadhi mazingira na kuhakikisha matumizi sahihi dhidi ya rasilimali nyingi ambazo nchi imejaliwa ikiwemo kutoa elimu juu ya uhifadhi wa mazingira. 

Kwa mujibu wa taarifa za Umoja wa Mataifa, uchafuzi wa plastiki leo haupo baharini pekee bali unaonekana kwenye udongo, maji na hata kupitia chembe ndogo za plastiki kwenye mazingira ya binadamu. Hii ndiyo sababu juhudi za mazingira sasa zinahusishwa moja kwa moja na afya, uchumi na ubora wa maisha.

Katika maadhimisho ya mwaka huu, mjadala wa kukijanisha Tanzania umeibuka kama zaidi ya kampeni ya kupanda miti, dhana yake ni kujenga mfumo wa maisha unaounganisha maendeleo, uchumi na uhifadhi wa mazingira kwa wakati mmoja.

Safari ya Tanzania ya kuelekea mwaka 2050 haitapimwa kwa ahadi zitakazotolewa leo pekee, bali kwa maamuzi yatakayofanywa, ambapo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mha. Hamad Masauni amesema kwasasa wameandaa mpango wa usimamizi wa mazingira kuelekea dira 2050 utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano.

"Mpango huu unalenga kuchochea matokeo makubwa ya kurejesha uoto wa asili, kuimarisha ustawi wa mfumo wa ikolojia pamoja na kutoa huduma za kiikolojia ambazo ni msingi muhimu za uzalishaji katika sekta mbalimbali za uchumi hatua ambazo wanaamini zitachangia kwa kiasi kikubwa katika kufanikisha malengo ya dira ifikapo 2050 ambayo yanalenga kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi 10 barani Afrika zenye ustawi wa mazingira na ustahimilivu mkubwa dhidi ya mabadiliko ya tabianchi,"anasema. 

Aidha, Mha. Masauni anasema kupitia mpango huo Serikali inatarajia kufanikisha malengo makuu mbalimbali ikiwemo kuhamasisha upandaji miti na utunzaji endelevu wa miti milioni 2 kila mwaka lakini kurejesha hekta milioni 5 za ardhi na misitu ambayo imeharibiwa na kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa. 

Katika Siku hii ya Mazingira Duniani, ishara za tahadhari ziko kila mahali, Miaka kumi na moja iliyopita imekuwa miaka kumi na moja yenye joto la juu zaidi kuwahi kurekodiwa, hatua ambayo wadau wa mazingira wanaitaja kama funzo la kuhakikisha mazingira yanaendelea kutunzwa.

Wanaeleza kuwa dunia kwasasa inaelekea kuzidi kwa muda kiwango cha nyuzi joto 1.5 ambapo kila sehemu ya ongezeko uleta madhara makubwa zaidi hasa kwa watu walio katika mazingira hatarishi zaidi.

"Jukumu letu ni kuhakikisha kuzidi huko kunakuwa kidogo iwezekanavyo na kwa muda mfupi na usalama mkubwa iwezekanavyo na kisha kupunguza haraka sana viwango vya joto, hilo linamaanisha kupunguza kwa kiasi kikubwa sana cha utoaji wa gesi chafuzi, kuharakisha mpito wa haki kutoka kwa matumizi ya nishati ya mafuta yasiyosafi kwenda kwenye nishati jadidifu ambayo ndiyo njia pekee endelevu ya kupunguza gharama na kuhakikisha usalama wa kweli wa nishati"wanasema.

Pia, wanaeleza kuwa ukanda wa Afrika Mashariki ndio ambao unaathirika zaidi na kuongezeka kwa joto tangu miaka ya 1960 mpaka sasa ambapo joto limekuwa likiongezeka kwa 0.7% mpaka 100.1% juu zaidi ya kiwango cha wastani wa kiwango cha dunia ambacho ni 0.1 mpaka 0.5 huku maeneo kama ya Kaskazini mwa Uganda na Kenya yakitajwa kuwa na joto la juu zaidi ambalo limepelekea maafa makubwa kwa watu wa maeneo hayo.

Mafanikio ya taifa la kijani hayatapimwa kwa idadi ya miche iliyopandwa, bali kwa uwezo wa wananchi kubadili matumizi ya kila siku kuanzia usimamizi wa taka, matumizi ya plastiki, uhifadhi wa vyanzo vya maji hadi upangaji wa makazi.

Hapa ndipo nafasi ya mwananchi wa kawaida inaanzia na kwa kijana anayechagua kutumia tena badala ya kutupa, kwa mfanyabiashara anayepunguza taka na kwa familia inayotunza matumizi ya maji hapo ndipo sera inaanza kuonekana kwenye uhalisia.

Tanzania inapozungumzia mwaka 2050, huenda swali lisiwe tumepanda miti mingapi bali ni tulijenga utamaduni wa kuishi kwa namna gani kuhakikisha mazingira yanalindwa, hivyo kukijanisha Tanzania si tukio la Juni 5 ila ni maamuzi ya kila siku inayofuata.


Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...