Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo Kusaya amewataka washiriki kuzingatia mafunzo na kwenda kusimamia matumizi ya mfumo huo katika kuinua taaluma ya Mkoa wa Mara.
"Hali ya Taaluma inategemea takwimu sahihi, ambazo zitaonyesha hali halisi iliyopo na kuwezesha kutatua changamoto kama zipo" amesema Kusaya.
Ameushukuru Mradi wa Shule Bora kwa kufadhili mafunzo kwa Maafisa wa ngazi mbalimbali na hususan mafunzo ya ukusanyaji wa takwimu ambayo amesema yanasaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia na taaluma kwa ujumla.
Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Ndugu Ayoub Mbilinyi amesema mafunzo hayo yametokana na maelekezo ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara baada ya kupokea taarifa za mafunzo ya mfumo huo yaliyotolewa kwa baadhi ya Maafisa wa Mkoa wa Mara.
Ndugu Mbilinyi amesema baada ya mafunzo hayo kwa wasimamizi wa elimu ngazi ya Halmashauri watayapeleka kwa wasimamizi wa elimu ngazi ya Kata na shule na Mkoa utaanza kupokea takwimu kupitia mfumo huo.

.jpg)




