Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Ni Bajeti yenye matumaini kwa wananchi


Na Saidina Msangi, WF, Dodoma

WAZIRI wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amewasilisha Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali, ambapo ameliomba Bunge ridhaa ya kukusanya na kutumia jumla ya shilingi trilioni 56.49 kwa Mwaka wa Fedha 2025/26.

Dkt. Nchemba ameomba ridhaa hiyo bungeni jijini Dodoma, wakati akiwasilisha mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2025/26, ambapo bajeti hiyo inatarajiwa kugharamiwa na mapato ya ndani ya shilingi trilioni 40.47, misaada shilingi trilioni 1.07 na mikopo ya shilingi trilioni 14.95.

‘‘Kati ya mapato ya ndani yanayotarajiwa, mapato ya kodi ni shilingi trilioni 32.31, mapato yasiyo ya kodi shilingi trilioni 6.48, na mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa shilingi trilioni 1.68. Aidha, mikopo inajumuisha shilingi trilioni 6.27 kutoka vyanzo vya ndani na shilingi trilioni 8.68 kutoka vyanzo vya nje’’, alifafanua Mhe. Nchemba.

Alieleza kuwa makadirio ya matumizi ya Serikali ya shilingi trilioni 56.49 kwa mwaka 2025/26 yanajumuisha Stahiki za watumishi na michango ya pensheni (Serikali Kuu) shilingi trilioni 9.17 pamoja na ununuzi wa bidhaa na huduma shilingi trilioni 5.58

Aliongeza kuwa matumizi mengine ni malipo ya riba za mikopo shilingi trilioni 6.49; na ruzuku kwa taasisi za Serikali, mashirika ya umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa shilingi trilioni 22.17 na shilingi trilioni 7.72 kugharamia malipo ya mtaji kwa deni la ndani na nje.

‘‘Katika Mwaka wa Fedha 2025/26 Serikali inatarajia kuongeza kasi ya ukuaji wa Pato Halisi la Taifa kufikia asilimia 6.0 mwaka 2025 kutoka ukuaji wa asilimia 5.5 mwaka 2024, kuendelea kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kuhakikisha kuwa unabaki kwenye wigo wa tarakimu moja ya wastani wa asilimia kati ya 3.0 - 5.0 katika muda wa kati’’, alifafanua Mhe. Nchemba.

Aidha, Dkt. Nchemba alisema Serikali inatarajia kuongeza Mapato ya ndani kufikia asilimia 16.7 ya Pato la Taifa mwaka 2025/26 ikilinganishwa na asilimia 15.8 mwaka 2024/25 na mapato ya kodi kufikia asilimia 13.3 ya Pato la Taifa mwaka 2025/26 kutoka asilimia 12.8 mwaka 2024/25.

Dkt. Nchemba alisema vipaumbele vya bajeti ya mwaka 2025/26 ni pamoja na kuendelea kutekeleza na kukamilisha miradi ya kielelezo na ile ya kimkakati, kuimarisha sekta za uzalishaji zenye matokeo chanya katika kukuza uchumi, kuimarisha rasilimali watu hususan katika sekta za huduma za jamii na kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji nchini ili kuvutia ushiriki wa sekta binafsi katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.

‘‘Maeneo mengine mahsusi ya vipaumbele ni pamoja na ugharamiaji wa Deni la Serikali; mishahara na stahiki za watumishi wa umma, pamoja na ujenzi na ukarabati wa viwanja vya michezo kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya AFCON 2027. Aidha, nipende kuwafahamisha Watanzania kuwa Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 tutaugharamia kwa fedha zetu za ndani’’, alisema Mhe. Nchemba.

Aidha, Dkt. Nchemba alisema katika mwaka 2025/26, Serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ukusanyaji wa mapato ikiwemo kuendelea kuhamasisha umma kuhusu kutoa na kudai risiti za malipo za kielektroniki za EFD na kuboresha utaratibu wa ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo vinavyosimamiwa na mamlaka za udhibiti.

‘‘Serikali itaendelea kuboresha Mfumo wa TAUSI ili kuhakikisha vyanzo vyote vya mapato vya Mamlaka za Serikali za Mitaa vinajumuishwa katika mfumo huo, kuongeza ufanisi wa mifumo ya ukusanyaji wa mapato ya mashirika, taasisi za umma na wakala za Serikali ili kuhakikisha gawio na michango stahiki inawasilishwa kwa wakati na kuendelea kutekeleza Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (MKUMBI)’’, alifafanua Mhe. Nchemba.


MABORESHO YA MIFUMO YA KODI

Dkt. Nchemba alisema Serikali inalenga kufanya maboresho ya mfumo wa kodi, ikiwemo baadhi ya viwango vya kodi, tozo na ada zinazotozwa chini ya sheria mbalimbali pamoja na kuboresha taratibu za ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya Serikali ili kuwa na mfumo wa kodi ambao ni tulivu na wa kutabirika unaolenga kuchochea shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ndani ya nchi.

Mapendekezo ya kurekebisha mfumo wa kodi kwa mwaka 2025/26 yanatarajiwa kuiongezea Serikali jumla ya shilingi milioni 4,260,023.77 ambapo baadhi ya mapendekezo hayo ni kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye viuatilifu vinavyotambulika kwa HS Codes 3808.61.00, 3808.62.00 na 3808.69.00, ili kuwapa unafuu wakulima ya kupata dawa za kuua wadudu mashambani na hivyo kuongeza uzalishaji wa mazao nchini.

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye miamala ya ununuzi wa bima mtawanyo inayofanywa baina ya kampuni za bima na zile za bima mtawanyo ili kuongeza ushindani wa kampuni za ndani, kukuza Sekta ya Bima na kuhamasisha matumizi ya bima katika kukabiliana na majanga nchini.

Kutoza kodi ya ongezeko la thamani kwa kiwango cha asilimia 0 kwenye bidhaa za nguo zinazotengenezwa kwa kutumia pamba inayolimwa nchini kwa kipindi cha mwaka mmoja ili kuleta unafuu kwa wakulima wa pamba na viwanda vinavyotengeneza nguo nchini.

Kutoza kodi ya ongezeko la thamani kwa kiwango cha asilimia 0 kwenye mbolea inayozalishwa ndani ya nchi kwa kipindi cha miaka mitatu ili kuleta unafuu kwa wakulima na walaji hasa katika kipindi hiki ambacho dunia imetoka kwenye mdororo wa kiuchumi duniani.

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye mafuta ya kula yanayozalishwa ndani ya nchi kwa kutumia mbegu zinazozalishwa nchini kwa muda wa mwaka mmoja ili kuendelea kuleta unafuu wa bei ya mafuta ya kula nchini.

Kufuta Msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani unaotolewa kwenye ununuaji na uingizaji wa gaming supply. Hatua hii inalenga kuleta usawa katika utozaji wa kodi kwa kuwa michezo mingine kama vile mpira wa miguu ipo katika wigo wa utozaji wa kodi ya ongezeko la thamani. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 322,022.5.

Kuweka sharti la msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani kwenye matairi ya trekta yanayotumika kwenye shughuli za kilimo yanayotambulika kwa HS Code 4011.70.00; dam liners zinazotambulika kwa Heading 39.20; forks (HS Code 8201.90.00); reki (HS Code 8201.30.00); na shoka (HS Code 8201.40.00) kutolewa baada ya kupata ridhaa ya Waziri mwenye dhamana ya masuala ya kilimo.

Kufuta msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani kwenye lami zinazotambulika kwa HS Code 2713.20.00 na 2715.00.00 ili kuendana na azma ya Serikali ya kupunguza misamaha isiyo na tija ili kulinda mapato ya Serikali na kupunguza matumizi yanayohusiana na utoaji wa misamaha ya kodi. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 85,606.2.

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye magazeti yanayozalishwa nchini pekee ili kupunguza gharama za magazeti hayo na hivyo kuwezesha upatikanaji wa taarifa muhimu. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 1,274.4.

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye gesi asilia inayouzwa kwenda kwenye vituo vya kushindilia gesi kwa ajili ya matumizi ya magari ili kuweka unafuu kwa wawekezaji, kuvutia uwekezaji wa vituo vya kusambazia gesi asilia iliyosindikwa kwenye magari na kupunguza utegemezi wa mafuta na uzalishaji wa hewa ya ukaa.

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye matanki na mitungi ya gesi ya kupikia zinazotambulika kwa HS Code 7311.00.10 pamoja na mitambo ya kuondoa hewa ukaa yenye HS Code 8417.80.00 inayotumika katika uzalishaji wa mikaa mbadala. Hatua hii inalenga kupunguza gharama za upatikanaji wa bidhaa hizi ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Kujumuisha masoko mtandao na huduma za masoko za kimtandao kwenye wigo wa tafsiri ya neno wakala wa huduma za kimtandao ili kutanua wigo wa kodi kwa kuweka ufafanuzi utakaopelekea kutatua changamoto zilizopo katika utozaji na usimamizi wa kodi ambapo tafsiri iliyopo sasa haijumuishi huduma hizo katika utozaji kodi. Hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 116,073.4.

Kuweka unafuu wa kutoza kodi ya mapato kwa kundi la pikipiki ya miguu miwili, pikipiki ya miguu mitatu (Bajaji) na magari ya kubeba mizigo yenye uzito usiozidi Kilogramu 500 ikiwemo Guta kwa kuweka utaratibu mpya wa kukadiria kodi ya mapato kwenye vyombo hivyo. Maboresho ya viwango vya kodi elekezi yanalenga kuweka unafuu wa kodi kwa kundi husika na hivyo kurahisisha utekelezaji wa sheria.

Kupunguza tozo ya ushuru wa huduma kutoka utaratibu wa sasa wa kutoza kiwango kisichozidi asilimia 0.3 ya pato ghafi kwenda kiwango mfuto cha asilimia 0.25 ya pato ghafi. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za ufanyaji biashara na uwekezaji nchini pamoja na kuendana na masharti ya Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (MKUMBI).

Kupunguza kiwango cha ada ya ushuru wa hoteli (hotel levy) kutoka asilimia 10 hadi asilimia 2. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za ufanyaji biashara na uwekezaji nchini.

Kufuta ada za upakiaji (loading) na upakuaji (offloading) zinazotozwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa zinazohusiana na usafirishaji wa mizigo. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za ufanyaji biashara na uwekezaji nchini ili kuendana na masharti ya Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara nchini (MKUMBI).

Kupunguza ada ya usajili wa pikipiki za biashara kutoka shilingi 340,000 hadi shilingi 170,000 kwa miaka mitatu ambapo ada husika italipwa wakati wa usajili wa awali pekee. Kupunguza ada ya leseni ya uendeshaji wa pikipiki, bajaji na guta kutoka shilingi 70,000 hadi shilingi 30,000.


KUGHARAMIA BIMA YA AFYA

Serikali inapendekeza kuanzisha vyanzo mbadala vya mapato ili kupunguza nakisi ya kibajeti kwa kufanya marekebisho katika sheria mbalimbali. Aidha inapendekezwa asilimia 70 ya mapato yatakayoongezeka ipelekwe kwenye Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI (ATF) na asilimia 30 ipelekwe kwenye Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa Wote. Marekebisho hayo ni kama ifuatavyo:

Kufanya marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 147 ili kuongeza ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji vya kilevi vinavyozalishwa na vinavyoingizwa kutoka nje ya nchi kama ifuatavyo: shilingi 20 kwa bia zinazotambulika kwa Heading 22.03; shilingi 30 kwa mvinyo unaotambulika kwa Heading 22.04, 22.05, na 22.06; shilingi 50 kwa spirits na vinywaji vingine vinavyotambulika kwa Heading 22.08.

Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 147 ili kuongeza kiwango cha ushuru wa bidhaa kwenye huduma za mawasiliano ya kielektroniki kutoka asilimia 17 hadi asilimia 17.5.

Kufanya marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Barabara na Mafuta, SURA 220 ili kutoza kiasi cha shilingi 10 kwa kila lita ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa pamoja na kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Madini, SURA 123 ili kutoza kiwango cha asilimia 0.1 kwenye thamani ya soko ya madini.

Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Michezo ya Kubahatisha, SURA 41 ili kuongeza kiwango cha kodi kwenye zawadi ya ushindi (Winning tax) kwenye michezo ya kubashiri matokeo (sports betting) kutoka asilimia 10 hadi asilimia 15; na kwenye michezo ya kasino ya ardhini (land based casino) kutoka asilimia 12 hadi asilimia 15.

Kutoza magari na mashine (heavy machines) zinazoingizwa kutoka nje ya nchi kama ifuatavyo: Shilingi 50,000 kwa magari yenye ukubwa wa injini (CC) kati ya 0 -1000; Shilingi 100,000 kwa magari yenye ukubwa wa injini (CC) kuanzia 1001-1500; Shilingi 150,000 kwa magari yenye ukubwa wa injini (CC) kuanzia 1501-2500; Shilingi 200,000 kwa magari yenye ukubwa wa injini (CC) kuanzia 2501 na zaidi; Shilingi 250,000 kwa mashine (Excavators, Bulldozers, Fork Lifts) zenye Heading 84.29 na 84.27.

Kutoza shilingi 500 kwa kila tiketi inayotolewa na mtoa huduma za usafirishaji kwa njia ya treni na kutoza shilingi 1000 kwa kila tiketi inayotolewa na mtoa huduma za usafirishaji kwa njia ya anga. Hatua hizi kwa pamoja zinatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa shilingi milioni 586,404.9.


KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA

Ili kuiwezesha nchi kuwa na sera bora za biashara na kuweka mazingira mazuri ya ufanyaji biashara baina ya wazawa na wageni, Serikali inatarajia kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Utoaji wa Leseni za Biashara ikiwemo:

Kufuta kifungu cha 3(4) kinachozipa nguvu mamlaka za utoaji wa leseni za biashara kufunga biashara pale ambapo wafanyabiashara wamekiuka masharti ya Sheria husika. Lengo la hatua hii ni kuwaondolea kero wafanyabiashara na pia kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kutofunga biashara.

Kuongeza kifungu cha 8(7) ambacho kinampa mamlaka Waziri mwenye dhamana na masuala ya biashara kuainisha shughuli za kibiashara ambazo hazipaswi kufanywa na wageni. Utaratibu wa utekelezaji wa kifungu hiki utafanywa kupitia Amri (Order) itakayotolewa na Waziri ambayo itakua na orodha ya shughuli za kibiashara ambazo hazipaswi kufanywa na wageni.

Dkt. Nchemba alisema bajeti hii inaendeleza na kukamilisha utekelezaji wa miradi, Kuchochea uchumi shindani na shirikishi, kuimarisha uzalishaji wa bidhaa viwandani na utoaji huduma, kukuza uwekezaji na biashara, kuchochea maendeleo ya watu na kuendeleza rasilimali watu ili kuhakikisha ufikiwaji wa malengo ya Dira 2025.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...