Tamasha la Rorya fursa festival 2024 kufanyika novemba 6-10 mwaka huu

GEORGE MARATO TV
0


Wilaya ya Rorya mkoani mara imeandaa Tamasha la Rorya fursa festival mwaka 2024 kwa ajili ya kutangaza fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii zilizopo wilayani humo.

Tamasha hilo litafanyika kuanzia novemba sita hadi kumi mwaka huu mjini shirati.

Ofisi ya Mkuu wa wilaya Rorya inakaribisha wananchi wote pamoja wadau mbalimbali kushiriki kwenye tamasha hilo litakalozinduliwa na Mkuu wa wilaya hiyo Dokta Khalfan Haule.

Miongoni mwa matukio muhimu yatakayopamba Tamasha la Rorya fursa festival ni pamoja na fursa za kilimo,uvuvi,ufugaji,michezo na utalii pamoja na mbuzi,kondoo,samaki na nyama choma.


Tamasha hilo litahimitishwa na mashindano ya mbio za mitumbwi katika eneo la mwalo wa sota,mashindano ya kuchoma nyama,maonesho ya fursa pamoja na kutoa vyeti kwa wawekezaji,wajasiriamali pamoja na idara zote wilayani Rorya.


Kauli mbiu ya Tamasha hilo ni Rorya na Uwekezaji endelevu kwa uchumi wa viwanda

 


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top