Kumalizika kwa mkataba huo kumetokana na maendeleo mazuri ya mradi wa bwawa la kufua umeme la Julius nyerere ambalo mpaka sasa Jumla ya megawatimegawati 940 zimeungwa kwenye Grid ya taifa
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kurugenzi ya mawasiliano na uhusiano Tanesco Makao makuu imewahakikishia wateja kuwa hali ya upatikanaji wa nishati ya umeme itaendelea kuimarika kwa kuzingatia vyanzo mbalimbali vya uzalishaji umeme.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa kwa sasa uwezo wa uzalishaji umeme kwa kutumia mitambo ya gesi asilia na mitambo inayotumia maji ni mkubwa kuliko mahitaji ya umeme hapa nchini
Serikali kupitia wizara ya nishati na Tanesco imeahidi kuendelea kusimamia kikamilifu sekta ndogo ya umeme ili kuhakikisha kunakuwa na huduma bora,endelevu na ya uhakika.

