Na Shomari Binda-Musoma
BINGWA wa mashindano ya Mathayo Cup 2024 jimbo la Musoma mjini ataondoka na zawadi ya ng'ombe na milioni moja.
Jumla ya timu 16 kutoka Kata za manispaa ya Musoma zinawanio zawadi hiyo na nyingine zitakazlkwa mbunge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo.
Akifungua mashindano hayo baada ya kukabidhi jezi na mixpira kwa timu shiriki mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka amesema mbunge Mathayo amefanya jambo kubwa katika kuinua michezo.
Amesema mji wa Musoma unatakiwa kuchangamka kupitia matukio mbalimbali yakiwemo ya kimichezo kama alivyofanya mbunge Mathayo.
Chikoka amesema mashindano hayo yameonekana yatakuwa na ushindani kutokana na hamasa ya zawadi na maandalizi ya timu.
" Nimshukuru sana mbunge Mathayo kwa kuanzisha mashindano haya yamekuja kuchangamsha mji wa Musoma.
"Zawadi ni kubwa zilizoandaliwa na mbunge tukapambane na kucheza kwa nidhamu katika kipindi chote cha mashindano", amesema.
Kwa upande wake Meya wa manispaa ya Musoma Patrick Gumbo amesema kama waatibu watasimamia mashindano hayo kuhakikisha yanafanyika kwa ufanisi.
Amesema nidhamu ni muhimu kuzingatiwa kwa kila timu ili kuweza kufikia malengo kusudiwa ya mashindano hayo.
Michezo ya ufunguzi iliyofanyika novemba 3 Mwigobero ilifungwa bao 1-0 na Mukendo huku Iringo ikishindwa kufungana na Kitaji.
Mashindano hayo yataendelea leo kwa michezo miwili Kamnyonge dhidi ya Makoko na Mwisenge na Buhare



