Wachezaji saba wa klabu ya Chavuma Town Council ya nchini Zambia wamefariki dunia na wengine 12 kujeruhiwa kwenye ajali ya basi wakati kikosi hicho kikielekea kwenye mechi ya ligi ya daraja la tatu, Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo.
Rais wa Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), Patrice Motsepe ametuma salamu za rambirambi kwa familia na Shirikisho la Soka Zambia kwa vifo hivyo.
