Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara Mhe.Ghati Zephania Chomete Leo tarehe 10 Machi, 2026 ameungana na mamia ya waombolezaji waliojitokeza kushiriki Mazishi ya Marehemu Sunzy Mwita Chambiri aliyekuwa Mtumishi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TMDA) Makao Makuu Dodoma.
Mazishi hayo yamefanyika katika Kijiji cha Wegero, Kata ya Buswahili, Wilayani Butiama, Mkoani Mara na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Chama, Serikali, Watumishi wa TMDA, Ndugu, Jamaa na Marafiki.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa, Jina lake lihimidiwe. AMINA
Mhe.Ghati Chomete (Mb),
Viti Maalum Mkoa- Mara,
Butiama (Wegero) -Mara,
Machi 10, 2026.




