Maelfu kwa mamia ya wananchi wameendelea kufurika kwenye viwanja vya Tanganyika Pakers Kawe jijini Dar es salaam tayari kumsikilizia Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan na,
Mgombea Mwenza Dkt. Emanuel John Nchimbi ambao pamoja na kuhutubia mkutano huo pia watatambulishwa rasmi kwa wananchi na wapiga kura wa Dar es Salaam na nchi nzima.










