Skip to main content

Posts

Showing posts from August 2, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

SERIKALI YAENDELEA KUWEKEZA KATIKA KUANDAA WATAALAMU WA SEKTA YA UCHUKUZI

Serikali imeendelea kuimarisha Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) ili kiweze kuzalisha wataalamu wenye ujuzi wa kukidhi mahitaji ya sekta ya uchukuzi, sambamba na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanyika katika miundombinu ya usafirishaji nchini. Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji Mhandisi Dkt. Prosper Mgaya. amesema chuo hicho kilianzishwa mwaka 1975 kama kitengo cha Shirika la Usafirishaji la Taifa, kabla ya kupandishwa hadhi mwaka 1982 kuwa taasisi ya elimu ya juu yenye jukumu la kutoa mafunzo, kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu katika sekta ya uchukuzi. Amesema baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977, Tanzania ilikabiliwa na uhaba wa wataalamu wa sekta ya usafirishaji, hali iliyoifanya Serikali kuimarisha chuo hicho ili kiweze kuzalisha wataalamu wa usafiri wa barabara, reli, anga na majini. Aidha, ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea ku...

MWENGE WA MWITONGO WATOA TUMAINI KWA TAIFA

Wazee wa Kabila la Wazanaki wamesema kuwaka kwa mwanga mkali na tulivu kwa Mwenge wa Mwitongo mara baada ya kuwashwa ni ishara ya mwaka wenye baraka, amani na mafanikio kwa Taifa la Tanzania. Wakizungumza katika hafla ya kuwashwa kwa Mwenge huo nyumbani kwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mwitongo, Agosti 2, 2026, wazee hao wamesema kwa mujibu wa mila na desturi za Wazanaki, Mwenge huo hubeba ujumbe maalumu kuhusu mwenendo wa taifa kila unapowashwa. "Kwa miaka mingi tumekuwa tukishuhudia kuwa endapo kuna dalili zisizo njema kwa taifa, Mwenge huu huonesha ishara zake mara baada ya kuwashwa. Leo tumeshuhudia ukiwaka vizuri sana bila hitilafu yoyote. Hii ni ishara njema na tunaliombea taifa letu liendelee kuwa na amani, umoja na maendeleo," wamesema baadhi ya wazee walioshuhudia tukio hilo. Wazee hao waliipongeza Serikali kwa kuendelea kuenzi urithi wa kihistoria wa Mwitongo, wakieleza kuwa utamaduni huo unaendelea kuimarisha historia ya Taifa na kumuenzi Baba w...

WAZIRI WA FEDHA BALOZI KHAMIS AITAKA TADB KUELEKEZA UWEKEZAJI KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI

 Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, ameielekeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kuelekeza uwekezaji wake katika maeneo ya kimkakati yatakayochochea mageuzi ya sekta ya kilimo na kuharakisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Akizungumza Agosti 2, 2026, baada ya kutembelea banda la TADB katika Maonesho ya Kitaifa ya Kilimo Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma, Balozi Khamis alisema maendeleo ya sekta ya kilimo ndiyo msingi wa ukuaji wa uchumi wa taifa na ustawi wa wananchi. Amesema Serikali imeendelea kuonyesha dhamira yake ya kuimarisha sekta hiyo kwa kuongeza mtaji wa TADB kutoka shilingi bilioni 60 hadi zaidi ya shilingi bilioni 400, hatua itakayoiwezesha benki hiyo kuongeza uwezo wa kufadhili miradi ya kilimo, mifugo, uvuvi na misitu kwa kiwango kikubwa zaidi. "Mafanikio ya sekta ya kilimo yatachangia kwa kiasi kikubwa kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Hivyo, TADB inapaswa kuelekeza uwekezaji k...

TUZO KUBWA ZA VIWANDA TANZANIA ZAREJEA

…… PMAYA ya 19 sasa kufanyika Agosti 24 Na Mwandishi Wetu Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) limetangaza kuwa Tuzo za Rais za Wazalishaji Bora wa Mwaka (PMAYA) kwa mara ya 19, jukwaa kubwa zaidi nchini Tanzania kwa kutambua mafanikio ya Viwanda, litafanyika Agosti 24 mwaka huu. Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa CTI, Hussein Sufian alisema Kaulimbiu ya mwaka huu, " Green Elegance — Celebrating Sustainable Manufacturing Practices," inaonesha mabadiliko katika kile ambacho PMAYA inatambua: si tu uzalishaji wa Viwanda, bali pia uendelevu, uwajibikaji, na ustahimilivu unaosimamia uzalishaji huo. Alisema jioni hiyo itashuhudia zulia la kwanza la kijani (Green Carpet) nchini Tanzania, likichukua nafasi ya zulia la kawaida la rangi nyekundu, ikiashiria dhamira ya pamoja ya sekta katika kuelekea ukuaji endelevu wa viwanda. "Kwa miaka kumi na tisa, PMAYA imekuwa ikieleza hadithi ya viwanda vya Tanzania katika hali yake bora zaidi. Mwaka huu, tunaeleza hadithi ...

MBUNGE MAVUNDE AWAINUA WAKINA MAMA WA KATA YA KIWANJA CHA NDEGE*

▪️Awasaidia kusajili SACCOS ya wakina mama ▪️Achangia Tsh 10m ▪️Wakina Mama wampongeza Rais Samia kwa mikopo nafuu 📍Mtumba, Dodoma Mbunge wa Jimbo la Mtumba Mhe.Anthony Mavunde ameendelea kuwa bega kwa bega na Wananchi wake kwa kutimiza ahadi zake alizowaahidi Wananchi hao katika kuwainua kiuchumi na kuwajengea uimara katika shughuli za kiuchumi. Jana tarehe 1 Agosti 2026, Mbunge Anthony Mavunde amefanya kikao na wakina mama wa kata ya Kiwanja cha Ndege na kuwataka kuendeleza umoja na mshikamano ili kujenga SACCOS imara ambayo mwisho wa siku itasaidia kubadilisha maisha ya wakina mama hao. Akiwa kama Mlezi wa SACCOS hiyo Waziri Mavunde ambaye ndiye Mbunge wao amewasaidia Tsh 10,000,000 ili kufanikisha usajili wa SACCOS hiyo na kuwasogezea fursa mbalimbali ikiwemo mikopo nafuu inayotolewa na serikali ya awamu ya sita chini ha uongozi  wa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Wananchi wote wa Tanzania, akiamini kwamba kupitia SACCOS hiyo wataweza ...

DKT. MWIGULU: KUWEKEZA KWENYE UTAFITI NI NJIA SAHIHI YA MAGEUZI YA KILIMO.

 ▪️Awataka watumishi kutimiza wajibu wao_ Dodoma, Agosti 2, 2026 WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewahimiza watendaji wa Serikali kuwahudumia kikamilifu Watanzania ili miradi inayojengwa na Serikali itoe matokeo chanya. “Tunachokijenga hapa, si jengo pekee, bali tunajenga mazingira bora ya utendaji wa mfuko. Kupitia uwekezaji huu tunachochea na tunaharakisha utekelezaji wa dhamira ya dhati aliyoionesha Mheshimiwa Rais kumsaidia mkulima mdogo kwa kuwezesha kupata mikopo.” “Watumishi wote wanapaswa kutimiza wajibu wao kwa bidii ili uwekezaji huu uwe na manufaa kwa Taifa. Tusiweke ofisi nzuri halafu huduma zikawa duni, tutakua hatujafikia malengo yaliyokusudiwa, ofisi nzuri lakini mwananchi akija kupata huduma anaambiwa njoo kesho, njoo kesho, majengo haya hayatakuwa na maana,” amesema Waziri Mkuu. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili Agosti 2, 2026) Iyumbu jijini Dodoma wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa makao makuu ya ofisi za Mfuko wa Udhamini wa Pembejeo za Kilimo (A...

BMT YATAJA FURSA 12 ZA AFCON 2027, WATANZANIA WAHIMIZWA KUJIANDAA MAPEMA

Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limetangaza fursa 12 zitakazotokana na Tanzania kuwa mwenyeji mwenza wa Mashindano ya Mataifa ya Afrika AFCON 2027 ambazo zitafungua zaidi milango ya maendeleo ya uchumi, ajira, biashara, utalii na uwekezaji nchini. Akizungumza kuhusu fursa hizo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa BMT, Bw. Aminiel Aligaesha, amesema AFCON 2027 ni tukio la kihistoria litakalofanyika kwa mara ya kwanza Ukanda wa Afrika Mashariki na likiwa linatimiza miaka 70 mwakani tangu kuanzishwa kwake. Kwa mujibu wa Bw. Aligaesha, fursa ya kwanza ni kuongezeka kwa biashara na shughuli za kiuchumi, ambapo hoteli, nyumba za kulala wageni, migahawa, maduka pamoja na wauzaji wa bidhaa zenye nembo za mashindano watanufaika kutokana na ongezeko la wageni na mashabiki. Aidha, amesema sekta ya benki na huduma za kifedha itanufaika kupitia ongezeko la miamala ya kifedha, huduma za kubadilisha fedha za kigeni, udhamini wa matukio na utoaji wa bidhaa maalum za kifedha kwa wa...

MWENGE WA UHURU WAFIKA KWA BABA WA TAIFA BUTIAMA NA KUWASHA MWENGE WA MWITONGO

 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndugu Wazo Michael Mwang'onda amewasha Mwenge wa Mwitongo Nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kutumia Mwenge wa Uhuru katika tukuo ambalo limefanyika Agosti 2 mwaka 2026 katika kijiji Butiama eneo la Mwitongo. Wakiwa Mwitongo, Mwenge wa Uhuru umepokelewa na familia ya Baba wa Taifa wakiongozwa na Chifu wa kabila la Wazanaki Japhet Wanzagi ambaye ni kiongozi wa familia ya Chifu Burito Nyerere na msimamizi wa familia ya Baba wa Taifa. Katika tukio hilo pia limeshuhudiwa na mkuu wa Mara kanali Evans Mtambi na viongozi wengine wa Serengeti na vyama vya Siasa.