Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) katika utendaji wa Mahakama ni eneo muhimu linalopaswa kupewa kipaumbele ili kuharakisha upatikanaji wa haki na kuongeza ufanisi. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 22 Juni 2026, alipokutana na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Jaji George Masaju, aliyefika Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha. Amesema Mahakama ya Zanzibar ina fursa ya kujifunza kutokana na mafanikio yaliyofikiwa na Mahakama ya Tanzania katika matumizi ya Tehama, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata haki kwa wakati na kupunguza gharama za kiutendaji. Rais Dkt. Mwinyi amepongeza ushirikiano uliopo baina ya Mahakama ya Zanzibar na Mahakama ya Tanzania na kusisitiza umuhimu wa kuuendeleza ili kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya pamoja kwa manufaa ya wananchi. Aidha, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeweka mkazo katika matumizi ya Tehama na uimarish...
Marato tv - Sauti ya Jamii