Skip to main content

Posts

Showing posts from August 3, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WAZIRI KIJAJI: NANENANE NI JUKWAA MUHIMU KUKUZA UTALII WA NDANI

 WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, amesema Maonesho ya Kitaifa ya Nanenane 2026 ni jukwaa muhimu la kuitangaza Tanzania kama kitovu cha utalii barani Afrika, huku yakitoa fursa ya kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa maliasili na kuhamasisha utalii wa ndani. Akizungumza leo baada ya kutembelea banda la Wizara ya Maliasili na Utalii katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma, Dkt. Kijaji amesema wizara imeandaa huduma na maonesho mbalimbali yanayowapa wananchi, hususan wanafunzi, nafasi ya kujifunza kuhusu rasilimali za taifa na kushuhudia baadhi ya wanyamapori hai ili kuongeza uelewa kuhusu urithi wa asili wa Tanzania. "Tupo hapa kwenye Maonesho ya Nanenane tukiwa tumewaletea wananchi huduma mbalimbali. Tunatoa elimu kuhusu uhifadhi na ustawi wa maliasili, lakini pia tumewaleta baadhi ya wanyamapori hai ili wananchi na wanafunzi wapate fursa ya kuwaona na kujifunza kuhusu utajiri mkubwa ambao Mwenyezi Mungu ameijalia Tanzania," ame...

WAKALA WA VIPIMO WAELEZA TIBA YA GESI PUNGUFU

 *Na.WMA-DODOMA*  WANANCHI  wametakiwa kuhakikisha wanapima mitungi ya gesi kabla ya kuinunua ili kujiridhisha kuwa wanapata kipimo cha gesi kinacholingana na fedha wanazolipa, huku wafanyabiashara wote wa gesi wakikumbushwa kutimiza matakwa ya kisheria ya kuwa na mizani iliyohakikiwa na Wakala wa Vipimo (WMA). Rai hiyo imetolewa na Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Singida, Willie Amosi, wakati wa Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma ambapo amesema matumizi ya gesi ya kupikia yameongezeka kwa kasi kufuatia jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati safi. Amesema jukumu la Wakala wa Vipimo ni kuhakikisha kila mtungi wa gesi unaouzwa kwa wananchi unakuwa na kipimo sahihi cha gesi kama kilivyoainishwa na mzalishaji, ili kumlinda mlaji dhidi ya hasara inayoweza kusababishwa na vipimo visivyo sahihi. "Wananchi wana haki ya kujiridhisha kuwa gesi wanayonunua ina uzito sahihi....

CP MKAMA AIPONGEZA MWANZA KWA USHIRIKIANO WA USALAMA

 Na: Dawati la Habari, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza. Kamishna wa Polisi Jamii, CP Alex Mkama , leo Agosti 4, 2026, ametembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na kupokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Amir Mkalipa , aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa. Akimkaribisha, Mkalipa amesema Mkoa wa Mwanza unaendelea kuwa salama na wenye utulivu, hali inayowawezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za kijamii na kiuchumi bila hofu. Amesema mafanikio hayo yanatokana na ushirikiano imara kati ya Jeshi la Polisi, vyombo vingine vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi. Aidha, amemhakikishia CP Mkama kuwa Mkoa wa Mwanza uko tayari kuendelea kupokea ushauri, maelekezo na miongozo kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi ili kuimarisha utekelezaji wa falsafa ya Polisi Jamii na kudumisha amani na usalama. Kwa upande wake, CP Mkama amesema ziara yake inalenga kutathmini utekelezaji wa shughuli za Polisi Jamii mkoani Mwanza, kupitia mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizopo na maeneo yanayohitaji...

NAIBU MTENDAJI SUMA JKT ATEMBELEA BANDA LA MALIASILI NANE NANE

📌Aipongeza Wizara kwa kushirikisha wadau wa mazao ya misitu na nyuki 📌Asema kazi ya uhifadhi inafanyika kwa weledi mkubwa *Na Neema Chalila Mbuja, Dodoma*  NAIBU Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT Brigedia Jenerali Shija Lupi leo Agosti 03, 2026 ametembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kujionea wadau mbalimbali wanaoshirikiana na wizara kwenye uzalishaji wa bidhaa za misitu na asali na kuipongeza wizara kwa kushirikiana na wadau hao. Brigedia Jenerali Shija amesema wadau hao wamekuwa wakifanya kazi nzuri katika kuhakikisha mazao hayo ya bidhaa za nyuki ikiwemo asali, miche ya miti na mazao ya misitu yanakuwa na soko ndani na nje ya nchi. Brigedia Jenerali Shija alipata wasaa wa kutembelea wanyamapori hai waliopo kwenye Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kama njia mojawapo ya kuutangaza utalii wa ndani.

BALOZI DKT. NCHIMBI: USHIRIKA WENYE UADILIFU NI MSINGI WA UCHUMI IMARA

 MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika kuimarisha usimamizi wa vyama vya ushirika nchini ili kuhakikisha vinaendeshwa kwa uwazi, uwajibikaji na uadilifu, akisisitiza kuwa ushirika wenye misingi hiyo ndiyo nguzo muhimu ya kukuza uchumi jumuishi na kuvutia uwekezaji. Dkt. Nchimbi ametoa kauli hiyo leo katika Siku Maalum ya Ushirika, iliyofanyika ndani ya Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane 2026 kwenye Viwanja vya John Malecela, Nzuguni mkoani Dodoma, ambapo pia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha sekta ya ushirika ili iwe kichocheo cha maendeleo ya kilimo na uchumi wa Taifa. Amesema Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) linapaswa kuendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa vyama vya ushirika ili kudhibiti ubadhirifu wa rasilimali, kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha na kuongeza uwazi katika uendeshaji wa vyama hivyo. "Ushirika wenye uadilifu unajenga iman...

BALOZI DKT. NCHIMBI APONGEZA MCHANGO WA TADB KUIMARISHA KILIMO NA VIWANDA VYA MAFUTA

 MAKAMU wa Rais Dk. Emmanuel Nchimbi ametembelea banda la Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) katika Maonesho ya 33 ya Nanenane na kujionea mchango wa benki hiyo katika kuimarisha uzalishaji wa kilimo, kuongeza thamani ya mazao na kuchochea maendeleo ya sekta ya kilimo nchini. Akiwa ameambatana na Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo, Makamu wa Rais alipokea taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Mipango, Ushauri na Mahusiano ya Taasisi wa TADB, Mkani Waziri, ambaye alisema benki hiyo imeendelea kutoa mikopo na huduma mbalimbali za kifedha zinazowawezesha wakulima, wafugaji, wavuvi na wawekezaji kuongeza uzalishaji, tija na usalama wa chakula nchini. Katika ziara hiyo, Mkurugenzi wa Kiwanda cha Mafuta ya Kula cha Trolle Meesle, Daniel Amulike, ameeleza namna ufadhili wa TADB ulivyowezesha kampuni yake kujenga kiwanda cha kisasa na kuongeza uzalishaji wa mafuta ya kula kwa kiwango kikubwa. "Baada ya kufadhiliwa na TADB, tumetoka kuzalisha tani 30 kwa mwezi hadi kufikia tani 624 za ...

TUMEANZA UTEKELEZAJI WA DIRA YA TAIFA 2050 TUKIWA NA MISINGI MIZURI YA KIUCHUMI - RAIS SAMIA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania imeanza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ikiwa na misingi mizuri ya kiuchumi, hali inayoweka mazingira bora ya kufikia malengo ya maendeleo yaliyowekwa kwa kipindi cha miaka 25 ijayo. Rais Samia ameyasema hayo leo Jumatatu Agosti 03, 2026 Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya uzinduzi wa nyenzo za utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na kushiriki katika mkutano wa mazungumzo maalum na sekta binafsi kuhusu utekelezaji wa dira hiyo. Amesema uchumi wa Tanzania umeendelea kuwa himilivu, mfumuko wa bei umedhibitiwa, uwekezaji umeongezeka na nchi imeendelea kujenga nafasi yake kama lango muhimu la biashara kwa nchi za Afrika Mashariki, Ukanda wa Maziwa Makuu na Kusini mwa Afrika. “Ni muhimu kutambua tumeanza utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050 tukiwa na msingi mzuri wa kiuchumi. Uchumi wetu umeendelea kuwa himilivu, mfumko wa bei unadhibitiwa, uwekezaji umeongezek...