WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, amesema Maonesho ya Kitaifa ya Nanenane 2026 ni jukwaa muhimu la kuitangaza Tanzania kama kitovu cha utalii barani Afrika, huku yakitoa fursa ya kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa maliasili na kuhamasisha utalii wa ndani. Akizungumza leo baada ya kutembelea banda la Wizara ya Maliasili na Utalii katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma, Dkt. Kijaji amesema wizara imeandaa huduma na maonesho mbalimbali yanayowapa wananchi, hususan wanafunzi, nafasi ya kujifunza kuhusu rasilimali za taifa na kushuhudia baadhi ya wanyamapori hai ili kuongeza uelewa kuhusu urithi wa asili wa Tanzania. "Tupo hapa kwenye Maonesho ya Nanenane tukiwa tumewaletea wananchi huduma mbalimbali. Tunatoa elimu kuhusu uhifadhi na ustawi wa maliasili, lakini pia tumewaleta baadhi ya wanyamapori hai ili wananchi na wanafunzi wapate fursa ya kuwaona na kujifunza kuhusu utajiri mkubwa ambao Mwenyezi Mungu ameijalia Tanzania," ame...
Marato tv - Sauti ya Jamii