Skip to main content

Posts

Showing posts from January 30, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Diamond aipongeza JAB, aahidi vyombo vyake kufuata matakwa ya Sheria

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi wa Wasafi Media, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz, ameipongeza Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kwa utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, huku akiahidi kuwa tayari kufuata matakwa yote ya kisheria yanayohusu sekta ya habari na watumishi wake.  Akizungumza baada ya kufika katika ofisi za Bodi hiyo kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya kisheria, Diamond amesema Wasafi Media haina nia ya kukwepa utekelezaji wa Sheria, bali iko tayari kushirikiana kikamilifu na wasimamizi wa taaluma hiyo. Amesema licha ya Sheria ya Huduma za Habari kuathiri vyombo vya habari kwa namna moja au nyingine, haiwezi kupingwa kwani ilitoa muda wa kutosha kwa wadau kujipanga na kutimiza vigezo vilivyowekwa ikiwemo Waandishi wake kuwa na kiwango cha Elimu cha Diploma na kuendelea. Diamond amekiri kuwa ujio wa Bodi ya Ithibati umeleta nidhamu kubwa katika taaluma ya habari, akisisitiza kuwa Wasafi Media inaunga mkono...

Dkt. Mwigulu Ashiriki Azania Bank Bunge Bonanza 2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 31, 2026 ameshiriki kwenye Azania Bank Bunge Bonanza 2026 linalofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya John Merlin jijini Dodoma. Bonanza hilo ambalo limedhaminiwa na AZANIA BANK limewahusisha Waheshimiwa Wabunge, Watumishi wa Ofisi ya Bunge, Taasisi mbalimbali pamoja na  wananchi. Kaulimbiu ya bonanza hilo ni “UMOJA WETU NI NGUVU YETU.”

Burkina Faso Yatangaza Kufuta Vyama Vyote Vya Siasa

 Serikali ya kijeshi ya Burkina Faso imetangaza kufuta vyama vyote vya siasa na kuhamisha mali zao zote kuwa mali ya serikali, kufuatia amri iliyopitishwa na mamlaka za nchi hiyo. Uamuzi huo ulifikiwa jana tarehe 29 Januari mjini Ouagadougou, katika kikao cha Baraza la Mawaziri kilichoongozwa na Kiongozi wa Taifa hilo, Kapteni Ibrahim Traoré. Waziri wa Mambo ya Ndani, Émile Zerbo, amesema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za kuijenga upya dola, akieleza kuwa mfumo wa vyama vingi uliokuwepo awali ulikuwa na matatizo makubwa, ikiwemo matumizi mabaya ya madaraka na kukosa ufanisi. Kwa mujibu wake, tathmini ya serikali imebaini kuwa kuongezeka kwa idadi ya vyama vya siasa kulichochea migawanyiko ndani ya jamii na kudhoofisha mshikamano wa kitaifa. Kabla ya mapinduzi ya mwaka 2022, Burkina Faso ilikuwa na zaidi ya vyama 100 vya siasa vilivyosajiliwa, huku 15 kati yao vikishikilia viti katika Bunge baada ya uchaguzi wa mwaka 2020. Msemaji wa serikali, Pingdwendé Gilbert Ouédraogo, amesema r...

Siku Mia Moja Za Rais Samia,Aridhia Tena Kibali Cha Ajira ya Watumishi 41,500 Kada Mbalimbali

 DODOMA. katika kutekeleza Maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan,Serikali imetoa kibali cha ajira Kwa nafasi 12,000 za ajira zikiwemo nafasi 5,000 za kada za Afya na nafasi 7,000 za Walimu wa Masomo ya Sayansi na Hisabati ikiwa ni Sehemu ya utekelezaji wa ahadi za Rais Samia ndani ya siku 100 za Serikali ya Awamu ya Sita. Akizungumza na Waandishi wa Habari Leo January 30,2026 Jijini Dodoma,Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwan Kikwete, amesema kuwa kibali hicho cha ajira kilitolewa baada ya Rais  Samia kuapishwa tarehe 3 Novemba 2025. Amesema hadi sasa jumla ya watumishi 8,416 wameripoti katika halmashauri mbalimbali nchini, wakiwemo watumishi 3,694 wa kada ya elimu na watumishi 4,722 wa kada ya afya. Sambamba na Hayo, amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia tena kibali cha Ajira ya Watumishi 41,500 za watumishi wa Kada mbalimbali kama vile watumishi wa Kada za Afya, Walimu, Kilimo, Afya, Uvuvi, Wahandisi, Zima...
  MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUONGEZEKA MARA* . 📌  📌 *Wilaya Sita kunufaika na mradi*  📍 *Mara*  Serikali ya Mkoa wa Mara Kaimu katibu tawala wa mkoa wa Mara ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji, Mhandisi Mwita Chacha Okayo leo Januari 30, 2026 imepokea mradi wa kupitia na kumaliza majiko banifu kwa bei ya ruzuku. Taarifa za utoaji wa taarifa ya mradi, Mhandisi Mwandamizi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Deusdedith Malulu amesema, Kupitia tafiti iliyofanyika mwaka 2016 inakadiria kuwa takribani watu 33,024 hufariki kabla ya wakati kila mwaka kutoka na magonjwa ambayo yanachangiwa na uchafuzi wa hewa ndani ya nyumba wakati wa upikaji kwa kutumia nishati safi na ya kupikia na hii ni sawa na asilimia 8.49 ya vifo vyote nchini. Hivyo, kwa kutambua hilo Serikali kupitia REA imekuja na mpango wa matumizi na matokeo ya majiko bani kwa bei ya ruzuku ili imani za kiafya na mazingira zitokanazo na matumizi ya nishati salama ya kupikia. H...