Skip to main content

Posts

Showing posts from July 13, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

CHATANDA: MAMA TIBAIJUKA, TUJENGE MSINGI WA UTII WA SHERIA NA SI MASHINIKIZO YA KUFUTA KESI KWA JINA LA MARIDHIANO

 NA: MWANDISHI WETU Mwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, amemshauri aliyewahi kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka, kuwa balozi wa kuhimiza viongozi na wananchi kutii sheria za nchi ili kuepuka kuingia katika mikono ya vyombo vya sheria. Chatanda ameyasema hayo Julai 14, 2026, kufuatia ujumbe alioandika Prof. Tibaijuka katika Mtandao X, kuhusiana na kesi inayomkabili Mwenyekiti Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu. Katika ujumbe wake, Prof. Tibaijuka amesema "Dkt. Samia Suluhu, Mhe. Rais naendelea kushauri kwa dhati Tundu Lissu aachiwe huru kwani kesi haikamiliki, hekima na busara iliyotufanya kuitangaza sera ya 4Rs ulipoingia madarakani ikuongoze tena katika jambo hili". "Simulizi hizi za kutisha za vyombo vya habari vya kimataifa zinainua hisia kali hasa kwa vijana, hata wazee tumekumbushwa kadhia ya operation Sogeza na iliyounda Vijiji vya Ujamaa 1974-1976, taarifa hizi z...

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA MIFUMO YA UKUSANYAJI WA MAPATO KUPITIA USIMAMIZI MAKINI WA FORODHA

 Na Mwanamkuu Mwandoro,Mkinga. Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) amesema Serikali itaendelea kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato kupitia usimamizi makini wa forodha ili kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani, kukuza biashara halali na kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Mhe. Waziri amesema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kituo cha Forodha cha Horohoro kilichopo Wilaya ya Mkinga, mkoani Tanga, ambapo alipata fursa ya kutathmini utendaji wa kituo hicho na kujionea mafanikio yaliyopatikana katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali. Alisema mafanikio yaliyofikiwa na Kituo cha Forodha cha Horohoro yanaonesha kuwa juhudi za Serikali za kuimarisha usimamizi wa forodha zinaendelea kuzaa matunda, huku mapato yanayokusanywa yakitoa mchango mkubwa katika kugharamia miradi ya maendeleo na kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi. "Serikali itaendelea kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato k...

PROF. SHEMDOE AMPONGEZA MBUNGE JACQUELINE MZINDAKAYA KURATIBU MAFUNZO YA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI

 Na OWM–TAMISEMI, Sumbawanga Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amempongeza Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacqueline Mzindakaya, kwa juhudi zake za kuwaunganisha wadau mbalimbali, ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu, Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, uongozi wa mkoa wa Rukwa na halmashauri zake, hatua iliyowezesha kufanyika kwa mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi mkoani Rukwa. Prof. Shemdoe ametoa pongezi hizo Julai 13, 2026 katika Ukumbi wa Country Hotel mjini Sumbawanga wakati akifungua mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, mafunzo ambayo yameratibiwa na Mbunge huyo kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC). Prof. Shemdoe amesema kuwa, anaamini mafunzo hayo yatafungua ukurasa mpya wa mae...

TUMIENI TAALUMA ZENU KULINDA UHURU NA MASLAHI YA TAIFA," RAIS SAMIA AWAASA MAWAKILI WA SERIKALI

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka Mawakili na Maafisa Sheria wa Serikali kuhakikisha sheria, mikataba na maamuzi ya Serikali vinalinda uhuru, usalama, rasilimali na maslahi ya Taifa. Rais Dkt. Samia ametoa agizo hilo leo jijini Arusha wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA). Amesema ushindani wa kiuchumi na kisiasa duniani unaitaka Tanzania kuwa na mfumo imara wa sheria unaolinda mamlaka ya nchi, uchumi wake na rasilimali za Taifa. Aidha, amewataka Mawakili wa Serikali kutambua vihatarishi vya kisheria mapema na kutoa ushauri kabla ya Serikali kuingia mikataba, kuanza miradi au kufanya maamuzi makubwa ili kuepusha hasara inayoweza kutokea kutokana na maamuzi hayo. "Ni wajibu wenu kugundua vihatarishi mapema, kushauri kwa wakati na kuhakikisha nchi inalindwa kwa misingi imara ya kisheria," amesema Rais Dkt. Samia. Halikadhalika, amesisitiza ushirikishwaji wa Mawakili na Maa...

ESTHER MATIKO AKABIDHI MIFUKO 120 YA SARUJI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA SHULE TARIME MJINI

 MBUNGE wa Jimbo la Tarime Mjini, Mhe. Esther Matiko, amekabidhi mifuko 120 ya saruji kwa shule za msingi zilizopo katika kata za Sabasaba na Nyamisangura, Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara, ikiwa ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuboresha miundombinu ya elimu na kuweka mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia. Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, Mhe. Matiko amesema ofisi yake imekuwa ikipokea maombi mengi kutoka kwa shule, taasisi mbalimbali pamoja na wananchi wanaohitaji msaada wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Alisema pamoja na mahitaji kuwa makubwa kuliko uwezo uliopo, ataendelea kushirikiana na Serikali, viongozi wa ngazi mbalimbali na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha changamoto zinazokabili sekta ya elimu zinapatiwa ufumbuzi. "Tumekuwa tukipokea maombi mengi kutoka shule na taasisi mbalimbali. Mahitaji ni mengi sana, lakini kwa ushirikiano wetu na wadau wa maendeleo tutaendelea kuyashughulikia hatua kwa hatua ili kuboresha mazingira ya wato...

TUMIENI TAALUMA ZENU KULINDA UHURU NA MASLAHI YA TAIFA," RAIS SAMIA AWAASA MAWAKILI WA SERIKALI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka Mawakili na Maafisa Sheria wa Serikali kuhakikisha sheria, mikataba na maamuzi ya Serikali vinalinda uhuru, usalama, rasilimali na maslahi ya Taifa. Rais Dkt. Samia ametoa agizo hilo leo jijini Arusha wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA). Amesema ushindani wa kiuchumi na kisiasa duniani unaitaka Tanzania kuwa na mfumo imara wa sheria unaolinda mamlaka ya nchi, uchumi wake na rasilimali za Taifa. Aidha, amewataka Mawakili wa Serikali kutambua vihatarishi vya kisheria mapema na kutoa ushauri kabla ya Serikali kuingia mikataba, kuanza miradi au kufanya maamuzi makubwa ili kuepusha hasara inayoweza kutokea kutokana na maamuzi hayo. "Ni wajibu wenu kugundua vihatarishi mapema, kushauri kwa wakati na kuhakikisha nchi inalindwa kwa misingi imara ya kisheria," amesema Rais Dkt. Samia. Halikadhalika, amesisitiza ushirikishwaji wa Mawakili na Maaf...

KAMBARAHE WASIRA ASHIRIKI MKUTANO MKUU WA MWAKA WA MAWAKILI WA SERIKALI JIJINI ARUSHA

 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Mhe. Kambarage Masato Wasira, leo Julai 13, 2026, ameungana na viongozi mbalimbali wa Serikali kushiriki Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), jijini Arusha. Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na umehudhuriwa na viongozi wa Serikali, mawakili wa Serikali kutoka taasisi mbalimbali, pamoja na wadau wa sekta ya sheria na haki. Ushiriki wa Mhe. Kambarage Wasira katika mkutano huo unaonyesha umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za Serikali na wadau wa sekta ya sheria katika kukuza utawala bora, kuimarisha misingi ya haki na kuendeleza maendeleo ya taifa kupitia mifumo imara ya kisheria. Mkutano Mkuu wa TPBA hufanyika kila mwaka ukiwa jukwaa la kujadili masuala ya taaluma ya sheria, kubadilishana uzoefu na kuweka mikakati ya kuimarisha utendaji wa mawakil...

SERIKALI YAAHIDI KUTUMIA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI YA JUWATA KUTENGENEZA BIDHAA MBALIMBALI

 Serikali imeahidi kuhakikisha washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali yanayotolewa na Jukwaa Huru la Wahariri Tanzania (JUWATA) wanayafanyia kazi kwa vitendo kwa kuwawezesha katika mikopo inayotolewa na Halmashauri kupitia utengenezaji wa bidhaa mbalimbali zitakazochangia ukuaji wa uchumi. Kauli hiyo imetolewa mkoani Morogoro na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Beatrice Njawa, wakati akifungua mafunzo hayo kwa wananchi. Bi.Njawa ambaye katika semina hiyo alimwakilisha Mgeni Rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima amesema Serikali inataka kuona mafunzo hayo yanazaa matokeo ya moja kwa moja kwa washiriki kuanzisha na kuendeleza viwanda vidogo, kusindika mazao ya kilimo na kutengeneza bidhaa zenye ubora wa kushindana sokoni. Mafunzo hayo ya siku tatu yanayoratibiwa na Jukwaa huru la Wahariri Tanzania (JUWATA) na kutolewa na wakufunzi wa taasisi ya MAMO ENTREPRNEURSHIP yanalenga kuwajengea wananchi mbalimbali uwezo wa kubuni miradi ya ujasiriamali ita...