Skip to main content

Posts

Showing posts from September 12, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wilaya Bariadi yapata Mbinu za Kuzuia Wanyama wakali na Waharibifu

Halmashauri ya wilaya Bariadi Mkoani Simiyu imekabidhi Majengo yaliyokuwa ya shule ya Sekondari Tarajali ya wasichana Matongo kwa wizara ya maliasili na Utalii ili yatumike kufundishia Taaluma ya wanyamapori. Makabidhiano ya Majengo hayo,Mkuu wa wilaya Bariadi Simon Simalenga amesema kuwa uwepo wa Chuo cha Taaluma ya Uhifadhi wa maliasili katika wilaya ya Bariadi  kutatoa fursa kwa jamii kujifunza pamoja na kutumia mbinu za kuzuia wanyama wakali na waharibifu ikiwemo Tembo. Simalenga aliyemwakilisha Mkuu wa mkoa Simiyu kwenye hafla hiyo amesema kuwa kuwepo kwa chuo cha Taaluma ya wanyamapori wilayani Bariadi pia kunatarajia kufungua fursa nyingi zikiwemo za kiuchumi na hivyo kuchochea ongezeko la mapato yatokanayo na sekta ya uhifadhi wa wanyamapori   Kwa Mujibu wa Mkuu huyo wa wilaya Bariadi,Moja ya Mipa ngo ya Mkoa Simiyu ni kujenga uwanja wa Ndege ambao utatumika kuleta watalii wa Nje na ndani ili kuendeleza azma ya serikali ya kuufungua zaidi Mkoa huo. Shule hiyo yenye Jum...

Waziri Bashe atangaza neema Sekta ya Umwagiliaji Shinyanga

Waziri wa Kilimo Mhe. Husein Bashe ametembelea mradi wa Umwagiliaji wa Nyida uliopo mkoani Shinyanga wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na kuelekeza kuwa ndani ya mradi huo lijengwe ghala kubwa la kuhifadhi mpunga. Waziri Bashe pia ameelekeza ufanyike ujenzi wa kituo  cha pamoja cha kununua mpunga na kufungwa mashine na kinu cha kuchakata mchele,sanjari na ujenzi wa barabara ya uhakika yenye urefu wa km 7.5 itayoungana na barabara kubwa ya lami na kujenga pamoja na kujenga Mabirika ya kunyweshea wanyama. Waziri Bashe amesema hayo wakati wa ziara ya kukagua Ujenzi wa mradi wa Umwagiliaji wa Nyida uliopo mkoani Shinyanga.  Aidha Waziri Bashe amebainisha dhamira ya serikali ya kuongeza mradi mdogo wa Nyida utakaokuwa na zaidi ya hekta 400 na ambapo ujenzi skimu hiyo utatangazwa hivi karibuni.  “Mradi huu ni ndoto za muda mrefu nilikuja mwaka 2020 na  leo namshukuru Mungu tumekuja hapa kuangalia maendeleo,namshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt Samia  Suluhu Hassan kwa kuk...

MJANAKHERI APONGEZA KASI YA MAENDELEO KISIWA CHA RUKUBA KIKITIMIZA MIAKA 50

MJANAKHERI APONGEZA KASI YA MAENDELEO KISIWA CHA RUKUBA KIKITIMIZA MIAKA 50 Na Shomari Binda-Musoma KATIBU wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) mkoa was Mara Ibrahim Mjanakheri amepongeza kasi ya maendeleo inayofanywa Kisiwa cha Rukuba. Kisiwa cha Rukuba kilichopo jimbo la Musoma vijijini kilianzishwa mwaka 1974 na mwaka huu wa 2024 kinatimiza miaka 50 Akiwa Kisiwani hapo na jana septemba 11 na msafara wa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Taifa Fadhili Maganya Katibu huyo wa CCM amesema kasi ya maendeleo ikisukumwa na mbunge wa jimbo hilo Profesa Sospeter Muhongo inapaswa kupongezwa. Amesema Profesa Muhongo mchango wake ni mkubwa katika kuhamasisha maendeleo ya kisiwa hicho ikiwa ni pamoja na kwenye elimu na afya. Mjanakheri amesema bila uhamasishaji katika eneo lolote maendeleo hayawezi kupatikana na harambee zinazofanywa na mbunge Muhongo maeneo mbalimbali zimekuwa zikisaidia " Maendeleo ya kisiwa cha Rukuba ni ya kasi na yanapita maeneo mengine na hii ni kazi kubwa inayofanywa na...

Wakazi wa Kijiji cha Remng'orori Waomba kutatuliwa kwa Mgogoro wa Mpaka

Wananchi wa kijiji cha Remng’orori kata ya Magange wilayani serengeti mkoani mara wanaishi kwa hofu kufuatia ongezeko la matukio ya uvamizi pamoja na wizi wa mifugo yao. Hofu na wasiwasi ya wakazi ya kijiji hicho unatokana na uwepo wa mgogoro wa mpaka baina ya kijiji hicho pamoja na kijiji Jirani cha Mikomariro kilichoko kata ya Mihingo wilayani Bunda. Uvamizi na uporaji wa mifugo unadaiwa kutekelezwa na baadhi ya wananchi wa kijiji jirani cha Mikomariro kwa nia ya kuwashinikiza wenzao wa kijiji cha remng’orori kuhama kutoka kwenye eneo lenye mgogoro. Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara,wananchi wa Remng’orori wamesema kuwa mgogoro huo umeathiri ustawi wao kutokana na wengi wao kuibiwa mifugo ikiwemo Maelfu ya ng’ombe,Kondoo na Mbuzi,kufyekewa mazao mashambani huku wengine wakijeruhiwa na kupoteza maisha. “Tuna njaa kwa sababu hatulimi kwa ukamilifu,kila tukilima watu wa Mikomariro wanavamia mashamba yetu na kuyafyeka mazao yetu,wanatunyang’anya vifaa vya kilimo ikiwemo Majembe na w...