Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe.Ridhiwani Kikwete amesema zaidi ya Vijana 1000 wanatarajiwa kushiriki katika Maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa mkoani Mwanza yatakayozinduliwa Oktoba 11, 2024. Aidha, Waziri Ridhiwani Kikwete amesema Wiki hiyo huadhimishwa kila Mwaka Oktoba 8 hadi 14 kwa kuwakutanisha vijana kutoka Tanzania bara na Visiwa kumuenzi Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Kujadiliana, kuonesha vipaji, bunifu na kazi wanazozifanya. Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dodoma, Mhe. Ridhiwani amesema Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuzindua wiki hiyo katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza. Waziri Ridhiwani ametaja shughuli zitakazofanyika kwenye wiki hiyo kuwa ni pamoja na kuwapo na makongamano ya kuwajengea uelewa wa fursa za ujasiriamali, ubunifu wa kidijitali katika kujifunza na kujiajiri sambamba na elimu ya Sera mpya ya maendeleo ya vijana (2007), Toleo la Mwaka 2024. Pia, amesema kut...
Marato tv - Sauti ya Jamii