Misungwi yaadhimisha Miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika Kwa Kufanya Usafi wa Mazingira Kwenye Maeneo ya Umma
Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza imeadhimisha sherehe za miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika kwa kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya umma ikiwemo Kituo cha Magazine Misungwi,Solo kuu la Misungwi na Soko la Jioni la Gwambina. Akizungumza na Wananchi na Watumishi walioshiriki kufanya usafi kati tarehe 9 Disemba 2024, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Johari Samizi amewataka wananchi kuendelea kufanya usafi katika maeneo yao sanjari na kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa na kuonya kuwa watakaopuuzia zoezi la usafi watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria. Mhe. Samizi ameongeza kuwa tangu kipindi cha Hayati Mwalimu Julius Nyerere hadi hivi sasa yametendeka mengi ikiwemo Ujenzi wa Daraja la JPM, Shule za msingi na Sekondari, miradi ya maji, Vituo vya afya na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya iliyopo Iteja, pamoja na Barabara. Kupitia awamu ya sita ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuna mabadiliko sana ambapo asilimia kubwa ya watu ni vijana ambao hawakushiriki haraka...