Skip to main content

Posts

Showing posts from June 11, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

UBALOZI WA SLOVAKIA NCHINI WAZINDULIWA RASMI

 Jamhuri ya Slovakia imeandika ukurasa mpya katika uhusiano wake na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuzindua rasmi Ofisi ya Ubalozi wake jijini Dar es Salaam, hatua inayotarajiwa kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, kiuchumi na maendeleo kati ya Tanzania na Sovakia. Uzinduzi huo umefanywa kwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Masuala ya Ulaya wa Slovakia, Mheshimiwa Juraj Blanár na Mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Balozi Mahmoud Thabit Kombo Juni 11,2026 . Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje na Masuala ya Ulaya wa Jamhuri ya Slovakia, Mheshimiwa Juraj Blanár, amesema ufunguzi wa Ubalozi wa Slovakia ni hatua ya kimkakati inayodhihirisha umuhimu mkubwa ambao Serikali ya Slovakia inaipa Tanzania kama mshirika wake muhimu barani Afrika.  Amesema Tanzania imeendelea kuwa kitovu muhimu cha diplomasia, biashara na maendeleo katika ukanda wa Afrika Mashariki, jambo linaloifanya kuwa lango la kuimarisha ushiri...

JKT YATOA SIKU NNE ZA MWISHO KWA VIJANA WALIOSHINDWA KURIPOTI MAKAMBINI

 Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limetoa fursa ya mwisho kwa vijana waliohitimu Kidato cha Sita mwaka 2026 na kuchaguliwa kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria, lakini wakashindwa kuripoti katika makambi waliopangiwa awali, kuripoti katika makambi yaliyo karibu na maeneo wanayoishi kuanzia Juni 12 hadi Juni 15, 2026. Akitoa taarifa hiyo leo Juni 12, 2026 katika Makao Makuu ya JKT Chamwino jijini Dodoma, Mkuu wa Tawi la Operesheni na Mafunzo JKT, Brigedia Jenerali Peter Mnyani, amesema hatua hiyo inatekeleza maelekezo ya Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele, ya kuhakikisha vijana wote waliochaguliwa wanapata nafasi ya kushiriki mafunzo hayo muhimu ya uzalendo, uzingatiaji wa sheria na ujenzi wa taifa. Amesema awali JKT liliwataka vijana hao kuripoti katika makambi waliopangiwa kuanzia Juni 1 hadi Juni 7, 2026, lakini baadhi yao walishindwa kufanya hivyo kutokana na sababu mbalimbali. Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa JKT ameelekeza vijana wote ambao bado hawajaripoti k...

CHATANDA: BAJETI 2026/27, IMETHIBITISHA RAIS SAMIA NI MJENGA NCHI

 NA: MWANDISHI WETU, DODOMA Uwasilishwaji wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2026/27, uliofanywa na Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Omar, Juni 11, 2026, Bungeni, Jijini Dodoma, umetoa mwelekeo wa nchi katika juhudi za maendeleo na kutatua kero za wananchi katika sekta mbalimbali. Katika bajeti hiyo, serikali inatarajia kukusanya na kutumia shilingi trilioni 62.33 ambapo ni ongezeko la asilimia 10.3, ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2025/2026. Akizungumzia bajeti hiyo, Juni 12, 2026, Jijini Dodoma, Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mwenyekiti wa Umoja na Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mary Chatanda amesema ni dhahiri Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amejipambanua kwa vitendo kuwa ni mjenga nchi. Chatanda amesema bajeti hiyo inaakisi mahitaji ya wananchi katika kuwaletea maendeleo na imegusa sekta muhimu za kijamii na kiuchumi. "Bajeti hii ni ya namna yake, mikopo ya vijana, wanawake na wenye mahitaji maalum imeongezeka kutoka asilimia kumi hadi 15. Pia, fedha nyingi ...

TRC YAONGEZA SAFARI YA EMU DODOMA-DAR KUTOKANA NA WIMBI LA WASAFIRI

 Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeongeza safari maalum ya treni ya umeme ya Mchongoko (EMU) kati ya Dodoma na Dar es Salaam kufuatia kuongezeka kwa idadi ya wasafiri wanaohitaji huduma hiyo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa TRC, Fredy Mwanjala,leo Jun 12,2026 Jijini Dar es salaam, amesema treni hiyo ya ziada itaondoka katika Stesheni ya Dodoma kuelekea Dar es Salaam saa 1:00 usiku leo Ijumaa, Juni 12, 2026. Amesema uamuzi wa kuongeza safari hiyo umetokana na ongezeko kubwa la mahitaji ya usafiri kwenye njia hiyo, huku TRC ikiendelea kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, salama na yenye uhakika. Mwanjala amewahimiza wasafiri kukata tiketi mapema kupitia mfumo rasmi wa ukataji tiketi wa shirika hilo ili kuepusha usumbufu unaoweza kujitokeza kutokana na ongezeko la mahitaji ya usafiri. Hatua hiyo inaendelea kuimarisha huduma za usafiri wa reli ya kisasa nchini, huku TRC ikijitahidi kukidhi mahitaji ya wananchi wanaotum...

BAJETI 2026/27 YAPANDA 10%, TRILLIONI 62.33 KUKUSANYWA

 Akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2026/27 Bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Fedha, Dkt. Khamis Mussa Omar ametangaza kuwa Serikali inatarajia kukusanya na kutumia jumla ya shilingi trilioni 62.33, ikiwa ni ongezeko la asilimia 10.3 ikilinganishwa na mwaka 2025/26. Ameeleza kuwa mapato ya Serikali yanakadiriwa kufikia shilingi trilioni 46.79, ambapo mapato ya kodi ni trilioni 36.99, mapato mengine trilioni 9.24 (ikiwemo trilioni 1.97 za Mamlaka za Serikali za Mitaa), huku misaada ya maendeleo ikiwa shilingi bilioni 563.1. Serikali imesisitiza kuwa asilimia 74.2 ya bajeti hiyo itagharamiwa na mapato ya ndani, hatua inayoimarisha uwezo wa kujitegemea kiuchumi. Aidha, misaada ya maendeleo imepungua kwa asilimia 39.1 kutokana na mabadiliko ya sera za baadhi ya washirika wa maendeleo, ambapo Serikali imewashukuru kwa mchango wao na kusisitiza umuhimu wa kuongeza uzalishaji na ulipaji kodi. Kwa upande wa matumizi, Serikali inakadiriwa kutumia shilingi trilioni 54.50 ka...

SERIKALI YAOMBA AWAMU YA PILI YA MRADI WA MAZIWA FAIDA KUANZIA MWAKA 2027

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeomba kuendelea kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Ireland kupitia utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Maziwa Faida kuanzia mwaka 2027 hadi 2032, ili kuendeleza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kuimarisha uzalishaji wa maziwa, kuongeza tija na kuboresha maisha ya wafugaji nchini. Ombi hilo limetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Fabian Madele, wakati akifungua rasmi Maonesho ya Ubunifu na Teknolojia katika Sekta ya Maziwa (TALIRI Open Day 2026) yaliyofanyika katika Kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Kanda ya Mashariki, jijini Tanga. Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Madele amesema Mradi wa Maziwa Faida unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania kupitia TALIRI na Taasisi ya Maendeleo ya Kilimo na Chakula ya Ireland (TEAGASC), kwa ufadhili wa Serikali ya Ireland kupitia Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania, umeleta mageuzi makubwa ...

MAVUNDE: SERIKALI ITAENDELEA KUVUTIA UWEKEZAJI SEKTA YA MADINI

 WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kuvutia na kuwezesha miradi zaidi ya madini nchini. Mavunde ameyasema hayo baada ya kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Marvel Gold ya Australia, Timothy Strong, ambaye alifika kutoa taarifa ya maendeleo ya mradi wa uchimbaji wa dhahabu unaotarajiwa kuanzishwa katika Wilaya ya Hanang, Mkoa wa Manyara. Amesema Serikali imefurahishwa na kasi ya utekelezaji wa hatua za awali za mradi huo, ambao kwa sasa upo katika hatua ya uchorongaji baada ya kukamilisha utafiti wa awali kwa kutumia teknolojia ya ndege zisizo na rubani (drones). “Tunapongeza wawekezaji kwa kasi wanayoionesha katika kuendeleza mradi huu muhimu. Serikali itaendelea kushirikiana nao kuhakikisha sekta ya madini inachangia kikamilifu katika uchumi wa taifa,” amesema Mavunde. Kwa upande wake, Strong amesema kampuni hiyo imeipongeza Serikali ya Tanzania k...

SERIKALI YAANZA HATUA MPYA ZA KUONGEZA MAPATO, WADAI RISITI KUNUFAIKA NA TUZO MAALUM

 SERIKALI imeweka mkazo katika kuongeza mapato ya ndani na kuimarisha uchumi wa kujitegemea kupitia utekelezaji wa mikakati mipya ya ukusanyaji kodi, huku ikitangaza kuanzishwa kwa Programu ya Tuzo ya Uzalendo itakayowazawadia wananchi na wafanyabiashara wanaoshiriki kikamilifu katika matumizi ya risiti za kielektroniki. Akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2026/2027 Bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Fedha, Dkt. Khamis Mussa Omar, amesema Serikali itaendelea kupunguza utegemezi wa misaada na mikopo ya nje kutokana na changamoto zinazoendelea kujitokeza ikiwemo kupungua kwa misaada ya maendeleo na kuongezeka kwa gharama za mikopo. Amesema katika mwaka wa fedha 2026/2027, Serikali itatekeleza hatua mbalimbali za kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani, zikiwemo kuvutia uwekezaji wa ndani na nje, kupanua wigo wa kodi, kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na walipakodi, pamoja na kusimamia matumizi sahihi ya mashine za kutolea risiti za kielektroniki (EFD)....

UCHUMI WA KIDIJITALI WAPEWA KIPAUMBELE BAJETI 2026/27

 Serikali imeweka mkazo katika kujenga uchumi himilivu unaotegemea mageuzi ya kidijitali, uwekezaji wa kimkakati na usimamizi madhubuti wa fedha za umma kupitia Bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 inayolenga kuharakisha maendeleo jumuishi na kuongeza ustawi wa wananchi. Akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali Bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar amesema bajeti hiyo imeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji ya wananchi wengi wanaoishi vijijini pamoja na kundi kubwa la vijana, huku ikilenga kuimarisha uchumi wa wananchi na kupunguza tofauti za maendeleo kati ya mikoa. Amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika maendeleo ya vijijini, kuendeleza mageuzi ya sekta ya kilimo, kuboresha huduma za jamii na kutekeleza mikakati maalumu ya kuinua uchumi wa maeneo yaliyobaki nyuma kimaendeleo. Katika mwaka 2026/27, Serikali imejipangia kukuza uchumi kwa asilimia 6.3 kutoka asilimia 5.9 mwaka 2025, kuongeza mapato ya ndani kufikia asilimia 17.1 ya Pato la Taifa na kudhibiti mfumuko wa...

DENI LA TAIFA BADO NI HIMILIVU

 SERIKALI imesema deni la Taifa linaendelea kuwa himilivu na salama licha ya kufikia shilingi trilioni 114.34 hadi Machi 2026, kutokana na usimamizi madhubuti wa deni na matumizi ya mikopo katika miradi ya maendeleo yenye tija kwa uchumi wa nchi. Akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2026/2027 Bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, amesema kati ya deni hilo, shilingi trilioni 38.45 ni deni la ndani sawa na asilimia 33.6, huku shilingi trilioni 75.89 zikiwa ni deni la nje sawa na asilimia 66.4. Amesema mikopo hiyo imeelekezwa katika sekta za kimkakati zinazochochea ukuaji wa uchumi, ikiwemo miundombinu ya usafirishaji, nishati na mawasiliano. Kwa mujibu wa tathmini ya uhimilivu wa deni iliyofanyika Novemba 2025, viashiria vyote vya deni vinaendelea kubaki ndani ya viwango vya kimataifa vinavyokubalika, jambo linaloonesha uwezo wa Tanzania kuhimili deni lake bila kuhatarisha uthabiti wa uchumi. Waziri Omar amesema tathmini za mwaka 2026 zili...