✅VIJANA 5,746 WANUFAIKA NCHINI Na: Mwandishi Wetu - Mwanza Serikali imeendelea kudhihirisha dhamira thabiti ya kuwawezesha vijana kiujuzi kupitia Programu ya Taifa ya Ukuzaji Ujuzi. Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Dkt. Evaline Munisi amesema hayo leo Juni 29, 2026 Mwanza alipotembelea Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Sengerema FDC kwa lengo la kukagua maendeleo ya mafunzo ya Uanagenzi yanayotolewa kupitia programu hiyo. Amesema, Serikali inalenga kujenga nguvukazi yenye ujuzi, maarifa na ubunifu ili kukidhi mahitaji ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kuongeza ushindani katika soko la ajira la ndani na nje ya nchi. Dkt. Munisi alisema Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano inaendelea kutekeleza Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi kwa kushirikiana na sekta binafsi kupitia mfumo wa ubia (PPP), huku mafunzo ya uanagenzi yakichukua nafasi muhimu katika kuziba pengo la ujuzi kwa vijana. Vile vile, amesema kuwa mfumo huo unamw...
Marato tv - Sauti ya Jamii