Skip to main content

Posts

Showing posts from March 1, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mega Copper Yaongeza Thamani ya Shaba

• Yalenga uzalishaji wa cathode ya asilimia 99 📍Kilimanjaro MKAKATI wa uongezaji thamani katika Sekta ya Madini umeanza kuzaa matunda mkoani Kilimanjaro, baada ya kampuni ya Mega Copper Co Ltd kujikita katika uongezaji wa kiwango cha ubora wa madini ya shaba kutoka asilimia moja hadi kufikia kati ya asilimia 20 na 25. Akizungumza katika kijiji cha Kiruru, wilayani Mwanga, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Ally Ng’anzo, amesema maboresho hayo yameongeza ushindani wa kampuni katika soko la kimataifa, huku China ikiwa soko kuu la sasa la mauzo ya madini hayo. Amesema pamoja na kampuni kufikia hatua hiyo ya uongezaji thamani ili kuzalisha makinikia ya shaba, matarajio yao ni kufanya uwekezaji zaidi kwa kufunga mitambo maalum ya uongezaji thamani, ili kufikia ubora wa hadi asilimia 99. Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza thamani ya bidhaa hiyo, kupanua wigo wa masoko na kuimarisha upatikanaji wa malighafi ya kutengeneza bidhaa za shaba kwa viwanda vya ndani. Kwa mujibu wa Ng’anzo, kampuni hiyo i...

Rea Yatoa Rai Kwa Wananchi Wilaya ya Butiama Kujiunga na Huduma ya Umeme na Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

📌 *Wananchi wapewa elimu ya nikonekt* . 📌 *Wananchi waaswa kutumia nishati safi na salama ya kupikia* . 📍 *Butiama.*  Wakazi wa wilaya ya Butiama Mkoa wa Mara,waaswa kutumia nishati safi na salama ya kupikia, kujiunga na huduma ya umeme  pamoja na  kutunza miundombinu ya umeme ili miundombinu hiyo iweze kudumu na  kutoa huduma kwa wananchi kwa  mda mrefu. Rai hiyo imetolewa leo jumatatu Machi 02, 2026 na wataalamu wa REA na TANESCO walipofika katika wilaya hiyo kutoa elimu na uhamasishaji wa miradi ya nishati vijijini. Akizungumza wakati wa uhamasishaji Afisa maendeleo ya jamii kutoka REA , ndugu Abdulrazack Mkomi amesema,Kwa sasa taratibu za uombaji huduma ya umeme zimeboreshwa zaidi  na hakuna tena mambo ya kutumia fomu kufanya maombi ambapo kwa kutumia tu namba ya Nida mwananchi anaweza kufanya ombi la  umeme moja kwa moja TANESCO kupitia huduma ya NIKONEKT. “Kwa kutumia simu janja, mwananchi atapakua huduma ya Nikonekt na kufanya maombi au kama ...

Ambulance lagongana na Lori, mgonjwa afariki

Na Mashaka Mhando, Tanga JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga linafanya uchunguzi wa ajali mbaya ya barabarani iliyosababisha kifo cha mgonjwa mmoja na kujeruhi watu wengine wanne, baada ya gari la wagonjwa (Ambulance) kugongana uso kwa uso na lori la mizigo. Tukio hilo limetokea leo Machi 1, 2026, majira ya saa 6:10 usiku katika eneo la Saruji, Wilaya ya Tanga, kwenye barabara kuu ya Tanga kuelekea Segera. Chanzo cha Ajali Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi, ilisema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa ajali hiyo imetokana na uzembe wa dereva wa gari la wagonjwa.  Inadaiwa kuwa dereva huyo alikuwa katika mwendo kasi uliompelekea kushindwa kulimudu gari hilo na kuhama upande wake wa kushoto na kuingia upande wa kulia, kisha kugongana uso kwa uso na lori. Waliohusika na Madhara Gari la wagonjwa lenye namba za usajili STM 7202, mali ya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, lilikuwa likitokea Mombo kuelekea Hospitali ya Rufaa ya Bombo l...

Kikundi Cha amani chataka kasi iongezwe kukamata wanaotukana mitandaoni

...Yapongeza siku 100 za Rais madarakani MASHAKA MHANDO, Tanga KIKUNDI cha Amani nchini kimeitaka Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Jeshi la Polisi, kuongeza kasi ya kuwafuatilia na kuwachukulia hatua kali watu wanaojiita wanaharakati wa mitandaoni wanaotumia majukwaa hayo kupotosha ukweli na kuichafua Serikali. Kauli hiyo imetolewa jijini Tanga katika mkutano maalum wa kikundi hicho uliolenga kuhamasisha uzalendo, kuelezea mafanikio ya Serikali na kupongeza utekelezaji wa ahadi za siku 100 za Rais tangu alipochaguliwa 2025. Akisoma risala ya kikundi hicho, Mjumbe wa Kikundi cha Amani, Rehema Manyama, alisema katika kipindi cha siku 100, Rais ameonyesha dira na uthubutu wa hali ya juu kwa kufanikisha utoaji wa Bima ya Afya kwa wote, kuzalisha ajira kwa vijana 12,000, kutoa mikopo, na kuituliza nchi dhidi ya misukosuko ya kisiasa. "Rais wetu ameonyesha dira ya kweli. Ndani ya siku 100 ameweza kuimarisha mahusiano ya kimataifa na kutoa fursa za kiuchumi. Tun...

Rais Dkt Samia Kufanya Ziara ya Kikazi Mkoani Arusha

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA. Amos Makalla na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili ya Ziara ya kikazi mkoani Arusha, tarehe 01 Machi, 2026.

Waziri Mkuu Aagiza Jedwali la Utekelezaji wa Utatuzi wa Kero za Wananchi

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza watendaji wa Serikali kuandaa jedwali la kuonesha namna walivyotatua kero za wananchi katika kila wiki ya mwisho wa mwezi. Amesema hayo leo Jumapili (Machi 01, 2026) katika mkutano wa hadhara uliofanyika Stendi za Zamani, Babati Mjini mkoani Manyara. Amesema kuwa Serikali haiwezi kukubali utaratibu wa kulimbikiza matatizo ya watu kana kwamba Serikali haipo. Ameongeza kuwa Serikali imetengeneza utaratibu ndani ya nchi wa kuwa na uongozi katika kila eneo kwa ajili ya kuwarahisishia wananchi kupata ufumbuzi wa matatizo yao. “Hatukutengeneza ofisi hizi za Serikali ili kugawana vyeo. Ninawahakikishia tukianza kufuatilia tutajua nani anaweza kazi na anastahili kukaa ofisini.”

Waziri Mkuu Azindua Stendi ya Mabasi ya Dkt. Samia Wilayani Hanang

*Ataka fedha zitafutwe kujenga barabara ya Katesh - Babati *Akataza watendaji kuchukua bidhaa za wajasiriamali wadogo WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amezindua Stendi ya Mabasi ya Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyopo Katesh, wilayani Hanang, mkoani Manyara ambayo imejengwa kwa gharama ya sh. bilioni 5.69. Stendi hiyo ambayo ujenzi wake umekamilika na imeanza kutumika, imelenga kuboresha utoaji huduma za usafiri na usafirishaji.  Miundombinu iliyopo ni pamoja na jengo kuu la kituo cha mabasi, maduka 116, maeneo ya wauza vyakula, vyoo matundu 21, vituo saba vya kukusanyia taka na vituo viwili vya ukaguzi na ulinzi. Hakuna kituo cha polisi.  Akizungumza na wakazi wa Hanang waliofika kushuhudia uzinduzi huo leo (Jumapili, Machi Mosi, 2026), Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na ujenzi wa stendi hiyo ambao ni sehemu ya miradi ya kimkakati ya kuboresha miundombinu ya usafiri na kuongeza mapato ya ndani. Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumwagiza Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey K...