SERIKALI ya Tanzania imetangaza mageuzi makubwa ya sekta ya ardhi yanayolenga kuboresha usimamizi, kuchochea ukuaji wa uchumi, na kulinda haki za wananchi wake. Akizungumza katika siku ya pili Mkutano wa Kimataifa wa Sekta ya Ardhi ulioandaliwa na Benki ya Dunia katika Makao Makuu ya Benki hiyo Jijini Washington DC, Marekani Mei 06, 2025, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi amesema mageuzi hayo yamefanywa na Serikali kupitia Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995 (Toleo la Mwaka 2023) ambayo ilizinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Machi 17, 2025 jijini Dodoma. Waziri Ndejembi amesema Sera hiyo inalenga kuboresha usimamizi wa ardhi kwa kuweka msingi imara wa haki, usawa na matumizi endelevu ya rasilimali hiyo muhimu. ‘‘Mageuzi haya yanatokana na uhitaji unaoendana na mahitaji ya sasa ya kijamii na kiuchumi, pamoja na kukabiliana na changamoto kama migogoro ya ardhi, ukuaji wa mijini na mabadiliko ...
Marato tv - Sauti ya Jamii