Skip to main content

Posts

Showing posts from July 26, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

■ *Waziri Mavunde ataka mnyororo wote wa utoroshaji wa madini hayo udhibitiwe,* ■ *Asikitishwa na upotevu wa mapato ya Serikali yatokanayo na vitendo hivyo,* ■ *Aelekeza wahusika wote wafutiwe leseni na kutoruhusiwa tena kufanya biashara ya madini,* ■ *Atoa rai kwa wananchi kufanya biashara ya madini kupitia mfumo rasmi* 📍Dar es Salaam, Kufuatia kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini unaofanywa na Wizara ya Madini kupitia Kikosi Kazi (Taskforce), madini aina ya dhahabu Gramu 4,402.20 yenye thamani ya 1,238,458,594.42 yamekatwa yakitoroshwa. Hayo yamesemwa leo tarehe 27 Julai, 2026 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* Jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari. "Serikali kupitia Wizara ya Madini iliunda Kikosi kazi ambacho kinahusisha vyombo vya dola ili kudhibiti biashara haramu ya madini na utoroshaji. Hii ni sehemu tu ya kazi ambazo zimeendelea kufanywa na Kikosi kazi hicho katika kuimarisha mfumo wa ufanyaji biasha...

KAIRUKI GREEN IVF YAFIKISHA WATOTO 160 KWA UPANDIKIZAJI MIMBA

 Na Mwandishi Wetu KITUO cha kupandikiza mimba cha Kairuki Green IVF (KGIVF), kilichoko Bunju A jijini Dar es Salaam kimefikisha jumla ya watoto 160 tangu kuanzishwa kwake miaka mitatu iliyopita. Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa kituo hicho, Dk Clementina Kairuki, wakati akizungumzia maadhimisho ya siku ya kimataifa ya IVF ambayo huadhimishwa kila tarehe 25 Julai kila mwaka. Alikuwa akizungumza na wasanii wa JUAKALI waliotembelea kituo hicho kujifunza namna kinavyofanya shughuli zake za kupandikiza mimba na kusaidia familia zenye changamoto ya uzazi. Dk Clementina alisema tarehe 25 Julai imepangwa kuwa siku ya IVF duniani kwani ndiyo siku ambayo mtoto wa kwanza alipatikana kwa njia ya upandikizaji mimba ambaye kwa sasa anamiaka 47. “Tunawapongeza sana watu waliogundua hii IVF kwasababu haikuwa rahisi kwani waligundua baada ya kujaribu mara nyingi sana, walijaribu karibu mara 103 ndipo wakafanikiwa mtoto wa kwanza akazaliwa, hata magazeti ya wa...

BRIGEDIA JENERALI MASANGURA ATEMBELEA WANAJESHI WA TANZANIA WANAOLINDA AMANI NCHINI CONGO

 KONGO:  Kamanda wa Brigedi ya kujibu ya mashambulizi (FIB) inayohudumu chini ya Mwamvuli wa Umoja wa Mataifa (MONUSCO) nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Brigedia Jenerali Alexandar Masangura amewatembelea Walinda amani wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wa Kikundi Cha Utayari (TANZQRF-05) kilichokalia eneo la Kiteule cha Mambasa kilichopo katika Jimbo la Ituri, Mashariki mwa nchi hiyo tarehe 25 Julai 2026. Lengo la ziara hiyo ni kujionea mazingira halisi ya kiutendaji wakati Kikundi hicho kikiendelea kutekeleza jukumu la ulinzi wa amani. Brigedia Jenerali Masangura amewapongeza walinda amani hao kwa namna wanavyotekeleza majukumu kwa weledi licha ya kuwa na changamoto kadhaa za kimazingira. Brigedia Jenerali Masangula wa Tanzania anaongoza Brigedi hiyo inayoundwa na vikundi kutoka nchi za Tanzania,  Malawi, Kenya na Nepal ambavyo vinaendelea kuwajibika Mashariki ya Kongo kwa kulinda raia dhidi ya mashambulizi kutoka kwa makundi ya watu wenye silaha.

MAKAMU WA RAIS BALOZI DKT. NCHIMBI, ATEMBELEA UWANJA WA AFCON ARUSHA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Uwanja wa Arusha, utakaotumika katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2027 (AFCON 2027), unaojengwa Jijini Arusha. Makamu wa Rais amepongeza maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo, ambapo amesema ni faraja kuona ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa ili kuvutia michuano hiyo kufanyika nchini Tanzania, inatakelezwa kikamilifu. Amemshukuru Mhe. Rais kwa kuendelea kutoa fedha ili kuhakikisha uwanja huo unakamilika kwa wakati. Aidha, Makamu wa Rais ameishukuru Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na mkoa wa Arusha, Wakandarasi na Mshauri Elekezi kwa kazi kubwa waliyofanya katika Uwanja huo. Makamu wa Rais amewataka Viongozi wa Wizara pamoja na Mkoa wa Arusha kusimamia vema agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha barabara zinazotumika katika kufika uwanjani hapo zinakamilika ...

WAZIRI KOMBO AKUTANA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA RWANDA

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Balozi Olivier Nduhungirehe, leo, tarehe 26 Julai, 2026, katika Ofisi Ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam. Viongozi hao walijadili masuala ya kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na maendeleo kati ya Tanzania na Rwanda, pamoja na masuala yenye maslahi ya pamoja katika ngazi ya kikanda na kimataifa, ikiwemo uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa Maji wa Rusumo unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania, Rwanda na Burundi. Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ali Bujiku; Mkurugenzi Msaidizi wa Idara hiyo, Bi. Julieth Muchunguzi; na Balozi wa Rwanda nchini, Mhe. Jenerali Patrick Nyamvumba. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Balozi Olivier Nduhu...

MBETO :KATIBA MPYA NI AHADI YA RAIS DK SAMIA,AMPONGEZA DK NCHIMBI KUWAKUMBUSHA WATANZANIA

 Na Mwandishi wetu, Zanzibar Chama Cha Mapinduzi kimesema ahadi ya kupatikana katiba mpya Tanzania iko pale pale kwakuwa ni ahadi ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kabla hajaondoka madarakani mwaka 2030. Aidha, CCM kimeupongeza msimamo uliotolewa na Makamu wa Rais Dkt Emmanuel Nchimbi kusisitiza azma kuandikwa katiba hiyo. Kauli hiyo imetamkwa na katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Idara ya itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis aliyesisitiza katiba mpya ni ahadi ya CCM kwa Watanzania. Mbeto alisema Rais Dk Samia alitoa ahadi hiyo katika mkutano wa uzinduzi kampeni za Uchaguzi Mkuu za ccm zilizofanyika viwanja vya Tanganyika Packers, Jijini Dar es Salaam.  Alisema kauli ya Dk Nchimbi ni msisitizo wa dhati kufuatia maamauzi ya ccm na serikali zake ,hivyo matamshi yake yanakwenda sambamba na ahadi ya Rais Dk Samia.  "Kwa dhati kabisa nipende kumpongeza Makamu wa Rais Dk Nchimbi kuwakumbusha Watanzania ahadi ya Katiba mpya. CCM na Kama vilivyoruhus...

WAKALA WA VIPIMO WASHIRIKI NBC MARATHON DODOMA

Watumishi wa Wakala wa Vipimo (WMA) asubuhi ya leo Julai 26, 2026 wameshiriki katika mbio za *NBC Marathon* zilizozofanyika jijini Dodoma kwa uratibu wa *Benki ya NBC*. Lengo kuu la mbio hizo ilikuwa kukusanya fedha za kusaidia matibabu kwa wagonjwa wasiojiweza, pamoja na kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa mazoezi katika kuimarisha afya. WMA imeshiriki katika mbio hizo kuunga mkono dhamira hiyo ya kibinadamu na kuonyesha mchango wa taasisi za Serikali katika masuala ya afya na ustawi wa jamii. Katika ushiriki huo, *watumishi 6 wa WMA walikimbia umbali wa Kilometa 10* wakati *mtumishi 1 alikimbia Kilometa 21*. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, *Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba* amewapongeza washiriki na waandaaji wa mbio hizo. Aidha ametoa wito kwa Watanzania kushiriki kwa wingi katika matukio kama haya ili kufanikisha malengo ya kuwasaidia wagonjwa na kuimarisha afya ya Taifa. Akizungumza kwa niaba ya watumishi wa WMA, Meneja wa Mkoa wa Dodoma, Ibrahim Saidi amesema, "Tume...

FEDHA ZA MARATHON ZILETE TIJA KWA WALENGWA ~ Dkt. MWIGULU*

_Serikali kuendelea kuboresha miundombinu wezeshi Mkoani Dodoma._ Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amezitaka wizara na taasisi zinazonufaika na fedha za NBC Marathon zihakikishe  zinatumika kwa uwazi na kwa kuzingatia thamani ya fedha, ili malengo yaliyokusudiwa yaweze kuleta matokeo, tena matokeo yanayopimika.  Amesisitiza kuwa kila shilingi inayowekezwa katika mbio hizo zinapaswa kuleta matokeo yanayoonekana, kwa sababu unaposhughulika na masuala ya afya, unaongelea uhai wa Watanzania. Aidha Waziri Mkuu amesema kuwa NBC Dodoma Marathon imeendelea kuwa zaidi ya mashindano ya riadha kwa kuwa ni jukwaa muhimu la kuhamasisha afya, kuimarisha ustawi wa jamii na kuchangia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi pamoja na kuboresha huduma za afya nchini. Dkt. Nchemba amesema hayo leo Julai 26, 2026, alipokuwa Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa msimu wa saba wa NBC Dodoma Marathon uliofanyika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma, ukiwa na kaulimbiu ya #KataWeseOkoaMaisha. Akizungumza...