Skip to main content

Posts

Showing posts from May 30, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

BULAYA AKABIDHI QUR'AN NA VITABU VYA DINI KWA WAUMINI WA KIISLAMU BUNDA MJINI

MBUNGE wa Jimbo la Bunda Mjini, Esther Bulaya, ameendelea kusaidia shughuli za dini baada ya kutoa Qur’an, Juzuu na vitabu mbalimbali vya dini ya Kiislamu kwa ajili ya misikiti na waumini wa jimbo hilo. Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Katibu wa Mbunge huyo, Mussa Hussein, amesema msaada huo umetolewa kwa lengo la kutatua changamoto ya upungufu wa Qur’an na vitabu vya dini katika misikiti ya Bunda Mjini. Amesema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za mbunge huyo za kuimarisha nyumba za ibada na kusaidia waumini kupata nyenzo muhimu za kujifunzia dini. “Mheshimiwa Esther Bulaya amekuwa akitoa misaada mbalimbali katika misikiti ya jimbo letu na ataendelea kufanya hivyo. Mbali na msaada huu wa vitabu, pia kuna mipango mingine ya kuendelea kuboresha na kuimarisha nyumba za ibada pamoja na kutatua changamoto mbalimbali zinazozikabili,” Amesema Kwa upande wake, Sheikh wa kata ya Bunda stoo na Masjid Nuru Seif Haruna Musa Omar Kayege amepokea msaada huo kwa niaba ya waumini na kueleza k...

TANZANIA, MSUMBIJI ZASAINI MAKUBALIANO MAPYA YA KUIMARISHA ULINZI NA USALAMA

Tanzania na Msumbiji zimechukua hatua mpya ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya ulinzi na usalama baada ya mawaziri wa ulinzi wa nchi hizo mbili kukutana na kusaini makubaliano mbalimbali ya kimkakati yatakayowanufaisha pande zote. Makubaliano hayo yalisainiwa jijini Dar es Salaam wakati Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wa Tanzania, Rhimo Nyansaho, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi wa Msumbiji, Cristóvão Chume, katika Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) yaliyopo Upanga. Mazungumzo hayo yalijikita katika namna ya kuendeleza ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Msumbiji, hususan katika masuala ya ulinzi, usalama na maslahi ya pamoja ya mataifa hayo jirani. Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa sekta ya ulinzi kutoka nchi zote mbili, akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Faraji Kasidi Mnyepe, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jacob John Mkunda, pamoja na maafisa wengine waandamizi. Ziara ya Waziri Chu...

BALOZI WA TANZANIA NCHINI UFARANSA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA KATIKA ELIMU YA JUU

Paris, Ufaransa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa, Mheshimiwa Saidi Othman Yakubu, amekutana na ujumbe wa viongozi wanawake 18 kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) waliopo nchini Ufaransa kwa ziara ya kitaaluma ya kujenga uwezo na kubadilishana uzoefu kuhusu uongozi, usimamizi wa taasisi za elimu ya juu na maendeleo ya wanawake katika nafasi za maamuzi. Ujumbe huo unaongozwa na Dkt. Janeth Emanuel Kigoba, Mkuu wa Kitivo cha Elimu cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, ambaye pamoja na viongozi wengine wanashiriki programu mbalimbali za kujifunza na kutathmini mifumo bora ya uongozi na utawala katika taasisi za elimu ya juu. Akizungumza na ujumbe huo katika Ubalozi wa Tanzania mjini Paris, Balozi Yakubu alisema imekuwa jambo la kutia moyo kuona kuwa sekta ya elimu ya juu, ambayo kwa miaka mingi imekuwa nyuma katika kufikia usawa wa kijinsia ikilinganishwa na baadhi ya sekta nyingine, sasa inaendelea kupiga hatua na kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafasi za...

ZAIDI YA WASAFIRI 75,000 WAFANYIWA UCHUNGUZI NA HAKUNA KISA CHA EBOLA KILICHOBAINIKA TANZANIA HADI SASA

 Na Hassan Kimweri, WAF - Kagera  Tanzania imeendelea kuimarisha udhibiti dhidi ya ugonjwa wa Ebola kwa kushirikiana na nchi jirani ikiwemo Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Burundi na Kenya kupitia ushirikiano wa kikanda ili kudhibiti kusambaa kwa maambukizi ya Ebola. Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amesema Hayo leo Mei 30, 2026 akiwa katika ziara mkoani Kagera kwa lengo la kukagua udhibiti na utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo mipakani pamoja na vituo vya afya vya kutolea huduma za dharula akiambatana na timu kutoka Wizara ya Afya, OWM- TAMISEMI na Mkoa wa Kagera.  "Zaidi ya wasafiri elfu 75,000 wamefanyiwa uchunguzi katika mipaka mbalimbali nchini tangu kuongezeka kwa tahadhari za Ebola, huku takribani watu 45,000 wakifanyiwa tathmini ya kina zaidi kutokana na kuhisiwa lakini hakuna aliyebainika na ugonjwa wa Ebola," amesema Dkt. Magembe Amesema, Serikali imeweka mifumo ya ufuatiliaji katika mipaka yote ya nchi ikiwemo mipaka ya nch...

MASSABURI ACHANGIA SHILINGI MILIONI TISA NA LAKI NNE UJENZI WA UKUTA WA SHULE YA MSINGI KICHANGANI

Leo tarehe 30 May 2026, Mbunge wa Jimbo la kivule *OJAMBI MASSABURI* alitoa vifaa vya tehama na vifaa vya ofisini katika shule ya msingi kichangani iliopo kata ya Majohe. Aidha Mhe Mbunge *Massaburi* alipata wasaa wa kuongea na wananchi waliohudhuria katika hafla iyo huku akiwashukuru Kwa mapenzi yao makubwa licha ya mvua kubwa lakini walijotokeza Kwa wingi katika hafla iyo. Pia Mhe Mbunge *Massaburi* alimpongeza mkuu wa shule Ndugu. Kuwa mfano wa kuigwa katika Jimbo la kivule Kwakua amekua ni Mtu wa kutatua changamoto na sio kulalamika. Aidha aliwashukuru wadau mbalimbali wakiwemo *Shivuta* na wengine Kwa uchangiaji wao hasa kununua vifaa vya *TEHAMA* ambavyo amevikabidhi leo. Mwisho Mhe Mbunge *Massaburi* aliwapongeza wananchi Kwa juhudi zao za kuanza kuchangia ukuta wa shule na kwakua wamekua wazalendo aliomba uongozi wa shule ye kama Kiongozi wao atatoa kiasi cha *shilingi Milioni Tisa na laki nne ( 9,400,000)* yeye pamoja na marafiki zake. Pia Mhe Mbunge *Massaburi* alisisitiza zo...

BONANZA LA MICHEZO WANAFUNZI WA KIKE LAFANA FUNGUNI SEKONDARI

NA: MWANDISHI WETU, PANGANI Uongozi wa Shule kwa kushirikiana na Idara ya Michezo katika Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga, umeratibu Bonanza la Michezo kwa wanafunzi wa kike waishio hosteli ikiwa ni njia ya kuhimiza ushirikiano, furaha, kujenga afya, kuibua na kukuza vipaji miongoni mwa wanafunzi. Bonanza hilo limefanyika Mei 30, 2026, katika uwanja wa shule. Bonanza limejumuisha michezo mbalimbali ikiwemo riadha ya umbali wa mita 100 na 400, kuruka na mpira wa miguu. Katika mbio za mita 100, walioibuka washindi ni Fatuma Selemani, Mary Yoram, Veronica Michael na Elizabeth Paschal. Aidha, katika mbio za mita 400, washindi ni Zakatu Ramadhani, Rebeca Ngoda na Zainabu Shabani. Aidha, katika mchezo wa kuruka, washindi ni Irene Daniel na Fatuma Selemani. Katika hatua nyingine, Bonanza hilo pia lilijumuisha mechi ya mpira wa miguu ya timu ya wasichana ya Bweni A na Bweni B. Timu ya Bweni A iliibuka kidedea kwa kupata ushindi mnono wa magoli (6-0) dhidi ya Bweni B...

WAZIRI MAVUNDE ATOA WITO WAMILIKI WOTE WA LESENI ZA UCHIMBAJI WA MADINI KINYWE KUANZA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI MARA MOJA

■ Lengo ni kuifanya Tanzania kuwa kinara wa uzalishaji wa madini kinywe ifikapo Mwaka 2030 ■ Serikali yasaini mkataba wa ubia na  Kampuni za Grafica na Eminent. ■ Aitaka Timu ya majadiliano ya serikali kuanza mchakato wa majadiliano na Wamiliki wa Leseni 27 ■ Amshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha sekta ya madini, ■ Ruangwa kuwa sehemu ya mnyororo wa thamani na teknolojia ya madini kinywe duniani. *Ruangwa, Lindi* Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* ameielekeza Timu ya Majadiliano ya Serikali kwenye Sekta ya Madini (GNT) kuwaita na kufanya nao majadiliano wamiliki wote wa leseni za uchimbaji madini kinywe nchini Tanzania kujadiliana kuhusu ubia wa serikali katika Kampuni hizo na kuwataka kuanza utekelezaji wa uchimbaji kwa mujibu wa masharti ya leseni na Sheria ya Madini Sura ya 123. Ameyasema hayo leo tarehe 30 Mei, 2026 Wilayani Ruangwa aliposhiriki zoezi la utiaji saini na Kampuni za Grafica Resources na Eminent Minerals Limited zenye ubia wa...