Serikali imeeleza dhamira yake ya kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania kupitia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku uzalishaji wa ajira ukipewa nafasi ya kipekee katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2026/27. Akiwasilisha mpango huo bungeni, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo amesema mpango huo umeandaliwa kwa lengo la kugeuza maono ya Dira 2050 kuwa miradi na programu zenye matokeo ya moja kwa moja kwa wananchi, hususan katika kukuza uchumi na kuzalisha ajira. Mpango wa mwaka 2026/27 ni mwanzo wa utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2026/27–2030/31), unaobeba dhima ya "Mageuzi kwa Ajili ya Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uzalishaji Ajira." Katika kufanikisha lengo hilo, serikali imeelekeza nguvu katika sekta zenye mchango mkubwa wa ajira ikiwemo kilimo, viwanda, madini, utalii, biashara pamoja na huduma za teknolojia na ubunifu, ambazo zinatajwa kuwa nguzo muhimu za kukuza uchumi na k...
Marato tv - Sauti ya Jamii